Calnde
JF-Expert Member
- Oct 7, 2008
- 1,373
- 277
Uonapo viongozi wanaonesha dhahiri ni wavivu wakufikiri na wepesi wa kusahau,uonapo migongano ya wenyewe kwa wenyewe ndani ya chama chao 'tukufu',uonapo wananchi wanamdhihirishia mkuu wao kuwa wamemchoka hata kufikia hatua ya kutaka kumbonda mawe,uonapo wezi wanabembelezwa kurudisha fedha ili wasifikishwe mahakamani ili hali walioongoza migomo vyuoni kudai wanachoamini ni haki yao wanapandishwa kizimbani hata kabla ya uchunguzi kuanza,uonapo kila kundi katika jamii limechoka na diplomasia na kuona migomo ni njia sahihi,uonapo nchi imefikia mahali swala la kitaifa linakabidhiwa kwa chama tawala kwa ajili ya utekelezaji na kila mtu hata katibu mwenezi wa chama anaouwezo wa kutoa tamko la kitaifa,unonapo vyuo vinafungwa na watawala wanaimba tunaboresha elimu kufuta ujinga,uonapo maisha yanakuwa magumu na wakuu wanaimba uchumi unapaa,uonapo yote yanatukia na mkuu wa kaya yupo kama vile hayupo......
Kisha uonapo kauli tamu kama vile MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA zinatoweka......
Binafsi naona mwisho mbaya wa chama tukufu kuparanganyika,kuanguka,kuvunjika na kuteketea hata kama si leo basi ni kesho.Sioni matumanini yaliyoujaza uso wa JK mwaka 2005,sioni ujasiri wa Kina Lowassa walioanza nao,naona mwisho mbovu uliojaa aibu na fedheha kwa wakuu hawa...
wewe waona nini?
Kisha uonapo kauli tamu kama vile MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA zinatoweka......
Binafsi naona mwisho mbaya wa chama tukufu kuparanganyika,kuanguka,kuvunjika na kuteketea hata kama si leo basi ni kesho.Sioni matumanini yaliyoujaza uso wa JK mwaka 2005,sioni ujasiri wa Kina Lowassa walioanza nao,naona mwisho mbovu uliojaa aibu na fedheha kwa wakuu hawa...
wewe waona nini?
Last edited: