Patriot
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 5,698
- 4,693
Ulitaka afanye nini? Au unaamini PCCB wangeweza kumkamata mgombea wa CCM? Tupo wengi ambao tumeshuhudia rushwa za uchaguzi. PCCB walinywea na waliambiwa wakae kimya ili kulinda heshima ya chama. Wewe unatoa maoni gani juu ya hilo? Kumbuka kuna kundi kubwa la wajumbe linasusibiri kupata chochote kipindi hiki baada ya kukaa kijiweni kwa miaka mitano iliyopita.Waafrika ndiyo tulivyo. Angalia huyu ni mwanachama wa CCM kindakindaki, ameona rushwa ya 30.000/= mpaka 100,000/= inatolewa kwa wajumbe. Cha ajabu amekaa kimya hakuna hatua aliyochukua ili uchaguzi uendelee wakimaliza aje JF aeleze alichokiona
Huu ni mtindo wa kizembe kwa Chama kinachojinadi kuwa kikongwe.