Expedito Mduda
JF-Expert Member
- Sep 22, 2009
- 522
- 239
Tazameni ndugu zangu,
Huko CCM palikuwa na watu wachache waliokuwa ni watetezi wa watu. Mmojawapo niliyemwona akifanya hiyo kazi pamoja alikuwa bado kwenye chama cha mafisadi alikuwa mheshimiwa Sitta.
Mheshimiwa Sitta alikuwa anasimamia maslahi ya ya watu. Mwisho wa bunge lililopita kila mtu alitamani bunge linalofuata liwe kama lililopita na hata kulishinda kwa umahiri wa kusimamia maslahi ya taifa.
Katika kusimamia maslahi ya taifa kuna mambo kadhaa wa kadhaa ambayo mtu lazima ujitoe sadaka. Mmojawapo ni kuhakikisha unakuwa na msimamao wako binafsi na hasa nguvu ya kuwapinga mafisadi. Sitta aliweza kufanya hivyo na kwa maana hiyo alikuwa kwenye kundi la wapiganaji.
Kwa msimamo huu, bunge lilichangamka sana na lilifanya kazi kubwa kiasi kwamba liliwafunua mafisadi wengi mpaka wengine katika serikali wakatakiwa kujihudhuru na serikali kuvunjwa na nyingine kuundwa upya.
Bunge jipya limeundwa na spika mpya madam Anna Makinda yule aliyesema hakuna kupunguza posho za wabunge na pengine atahakikisha inaongezwa.
Kwa sasa Sitta alikuwa anahitajika kuwa spika wa bunge. Kwa kuwa alikuwa mwiba kwa mafisadi, wamefanya njama na kuhakikisha hapiti tena katika nafasi hiyo ili mafisadi waendelea kula nchi kwa uma na mrija.
Leo hii wanakuja na kisingizio cha jinsia. Kwani hiyo jinsia ni kwenye uspika tu? Kwa nini jinsia leo na siyo juzi au kesho? Jamani Kwa Tanzania ukiwa mtetezi wa wanyonge mafisadi wanakutoa kafara: Sitta ametolewa kafara.
Walipoona kumpeleka bungeni ili wabunge wasema kama bado wanamhitaji atapita, basi wakaona waje na ujinsia! Lakini hivi nyie Watanzania mmella usingizi wa mtindo gani?
Lakini pia watu kama Sitta mnasubiri nini huko mliko? Kwani huko mliko ndo mama yenu na baba yenu? Ondokeni!!
Ndugu zanguni mafisadi tunaomba mtuhurumie, Watanzania wenzenu tunakufa. Mwache hao watetezi wetu waendelee kututetea.
Anna Makinda umefurahi sana kuchaguliwa sijui kama unamjua aliyekuweka hapo! Ni juu yako kuamua kumtumikia na kuwatosa Watanzania wenzako au kumtosa huyo na kuwatumikia Watanzania wenzako.
Ni jukumu letu sote kuwa macho na mtindo huu mchafu na kuhakikisha tunakemea haya tusije tukaporwa nchi yetu kweupe mchana. Tuwe waangalifu sana na madaraka tunayowapa watu maana itategemea na uwezo wao wa kufikiri. Hayo nayo wanaweza wakawa hawayajui. Wanauza nchi bila kujua.
Mimi nasema kwa sasa Watanzania tuamke tuilinde nchi yetu.
Huko CCM palikuwa na watu wachache waliokuwa ni watetezi wa watu. Mmojawapo niliyemwona akifanya hiyo kazi pamoja alikuwa bado kwenye chama cha mafisadi alikuwa mheshimiwa Sitta.
Mheshimiwa Sitta alikuwa anasimamia maslahi ya ya watu. Mwisho wa bunge lililopita kila mtu alitamani bunge linalofuata liwe kama lililopita na hata kulishinda kwa umahiri wa kusimamia maslahi ya taifa.
Katika kusimamia maslahi ya taifa kuna mambo kadhaa wa kadhaa ambayo mtu lazima ujitoe sadaka. Mmojawapo ni kuhakikisha unakuwa na msimamao wako binafsi na hasa nguvu ya kuwapinga mafisadi. Sitta aliweza kufanya hivyo na kwa maana hiyo alikuwa kwenye kundi la wapiganaji.
Kwa msimamo huu, bunge lilichangamka sana na lilifanya kazi kubwa kiasi kwamba liliwafunua mafisadi wengi mpaka wengine katika serikali wakatakiwa kujihudhuru na serikali kuvunjwa na nyingine kuundwa upya.
Bunge jipya limeundwa na spika mpya madam Anna Makinda yule aliyesema hakuna kupunguza posho za wabunge na pengine atahakikisha inaongezwa.
Kwa sasa Sitta alikuwa anahitajika kuwa spika wa bunge. Kwa kuwa alikuwa mwiba kwa mafisadi, wamefanya njama na kuhakikisha hapiti tena katika nafasi hiyo ili mafisadi waendelea kula nchi kwa uma na mrija.
Leo hii wanakuja na kisingizio cha jinsia. Kwani hiyo jinsia ni kwenye uspika tu? Kwa nini jinsia leo na siyo juzi au kesho? Jamani Kwa Tanzania ukiwa mtetezi wa wanyonge mafisadi wanakutoa kafara: Sitta ametolewa kafara.
Walipoona kumpeleka bungeni ili wabunge wasema kama bado wanamhitaji atapita, basi wakaona waje na ujinsia! Lakini hivi nyie Watanzania mmella usingizi wa mtindo gani?
Lakini pia watu kama Sitta mnasubiri nini huko mliko? Kwani huko mliko ndo mama yenu na baba yenu? Ondokeni!!
Ndugu zanguni mafisadi tunaomba mtuhurumie, Watanzania wenzenu tunakufa. Mwache hao watetezi wetu waendelee kututetea.
Anna Makinda umefurahi sana kuchaguliwa sijui kama unamjua aliyekuweka hapo! Ni juu yako kuamua kumtumikia na kuwatosa Watanzania wenzako au kumtosa huyo na kuwatumikia Watanzania wenzako.
Ni jukumu letu sote kuwa macho na mtindo huu mchafu na kuhakikisha tunakemea haya tusije tukaporwa nchi yetu kweupe mchana. Tuwe waangalifu sana na madaraka tunayowapa watu maana itategemea na uwezo wao wa kufikiri. Hayo nayo wanaweza wakawa hawayajui. Wanauza nchi bila kujua.
Mimi nasema kwa sasa Watanzania tuamke tuilinde nchi yetu.