Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

1. Tengenezesha tololi afu ufanye mobile genge, unauza vitu mboga mboga, I mean karoti, vitunguu, nyanya, hoho, etc yaani mamboga mboga in general

2. Tafuta bustani ulime mboga mboga za biashara, kama mchicha, chainizi, sukuma wiki, cabbage etc afu unaziuza

3. Nenda karikakoo kanunue urembo urembo waakina dada na uanze biashara ya umachinga unapitisha kwenye masaloon maofisin etc
 
Fanya hivi ndugu...tafuta mtu anaefuga kuku WA mayai kwa wingi halafu muombe akuuzie bei ya jumla..huku nilipo mm Ni 5000 bei ya jumla halafu WW tafuta wateja wa chips wauzie 6500 sabab maduka mengi wanauza 7000 hiyo itakuwa imekupa WW competitive advantage...kwahiyo bas utaanza na tray 10 ambazo zitagharimu 50000 Tu..

ukienda kununua tray ya kubebea hayo mayai bei yake haizidi 10000...mpaka hapo umetumia 60000... Hapa cha kuangalia Ni kuhakikisha unapata faida ya sh 1000 kwa Kila tray na usambaze kumi kila siku...ile sh 500 inayobaki kwa kila tray ifanye kama running cost...cha muhim hakikisha sehem unayotolea mayai haipo mbali na wateja Wako kusudi upunguze gharama zisizo za lazima na mayai kuvunjika...

mimi nilianza na mtaji wa elfu 80000 na sasa Nina uwezo wa kusambaza tray 150 kwa siku....usikubali mtu yeyote akukatishe tamaa eti mpaka uwe na mamilion ya pesa ndio ufanye biashara inayoeleweka...jiamin na mshirikishe Mungu hiyo pesa Ni nyingi sanaaa...go big...
 
kama upo jirani na shamba la miwa nenda ukanunue ya tsh 5000 harafu kaa pembeni ya barabara katakata vipande weka kwenye mfuko, kila kimfuko tsh 500, itakulipa na utakuza mtaji.

Unaweza fanya biashara ya kuuza juice, we nenda soko kuu nunua maparachichi, changanya na yale yalioregea kabisa ambayo hayafai kununua, blenda nunua ya elfu 40, garoni ya lita 5 utanunua tsh 1000 au omba kwa mtu, umeme tumia kwa kificho hapo unapoishi ukipata mtaji mkubwa changia luku, barafu nunua 1 buku liponde ponde kisha changanya kwenye juice.

Soko la juice beba garon lako la juice na glass zunguka nalo kwenye mikusanyiko ya watu hasa muda wa mchana.

NB ; matunda usinunue mazima nunua yale yanayokaribia kuharibika(munapatana bei) kisha unanunua kitunguu swaumu kwaajili ya kukata harufu.
 
Hongera sana mtoa mada kwa mawazo endelevu. Nilikuwa nafanya kazi ya kuajiriwa, sikuwahi kuona thamani ya pesa na nilikuwa na kipato kizuri tu.

Cha ajabu niliyekuwa namtuma na kumlipa ujira kidogo alihenga kinyumba chake kabla yangu na akahamia ndo nikashtuka kuwa kumbe hata mimi naweza!

Hakuna hela ndogo ukiwa na malengo. Nakushauri usikatishwe tamaa huo ni mtaji mkubwa sana tu. Cha msingi uwe makini na kila senti utakayoipata.

Kila la heri!
 
wachina wanatuuzia taka nyingi sana, ukipata wazo la taka utakayoweza kuisafisha na kuiza tena malipo ni mara mia.

laki ni pesa ndefu!
 
Habari zenu wakuu,

Naombeni ushauri wenu wakuu, nina mtaji wa shilingi laki mbili lakini sijui nifanye biashara gani.

Asanteni.
 
Fungua banda la chips mkuu, cjui upo wap kama ni dar itakutoa braza, fanya utafiti wamazingira mazuri
 
Makazi yako ni wapi? Angalia mazingira yanayokuzunguka huduma gani inapatikana kwa uhaba halafu angalia na kiasi ulichonacho kama kinaruhusu tumia fursa. Usiogope changamoto kwani hakuna jambo lolote lisilokuwa na changamoto hapa duniani
 
Back
Top Bottom