Kwa msimamo huu wa spika Makinda; Naamini CCM inawatoa kafara la damu watanzania!

hayo mambo yanahusiana vipi na shughuli za bunge? Ajali ikitokea vikosi vya uokoaji, polisi wanajeshi na wafanyakazi wengine wanaohusika ndio wanaoshughulikia. Sasa wabunge waahirishe kikao ili wafanye nini?.. Itasaidia nini? Kama hamad alikuwa na udhuru si angeenda tu kuwapa pole wanajimbo wake, haijalishi saa nne asubuhi au saa kumi na mbili jioni.
Ni mambo ambayo kusema kweli hayana maana yeyote zaidi ya kuleta mtafaruku ndani ya bunge...... Pointless!

kapime akili faza....
 
Kobello may be you are right in your own context maana ila ulipokosea ni kuwa unajenga hoja ambayo ni internal inherited or yours is backed by any school of thought. Maana hata watu wanaofuata Hegelian philosophy ambayo huamini mwafrika si mali kitu nao wanao wafuasi japo their context ni prejudiced, biased, inhuman and contains highest degree of segregation. Sasa turudi kwenye msimamo wako kuwa hakukuwa na haja ya kuahirisha bunge ili kuwapa wawakilishi nafasi ya kwenda kulia na wenzao, kuokoa na kufariji. Huu ni ufinyu wa kufikiri nje ya box. Inawezekana falsafa yako inakufanya kuyaona mambo katika umbali wa pua. Hivi wabunge kama binadamu unaona hawana msaada wanaoweza kuutoa wakati wa maafa/majanga hata kama yametokea mbali. Hawewezi kutao damu kwa yule mwenye kuhitaji? Wengine ni madaktari kwa taaluma, wengine wana ujuzi wa uokozi na wengine wanaweza kutoa mawazo endelevu ya kutatua tatizo as long as they in the field. Najua umependa sana ideology yako na unataka kila mfuasi wa ideology hiyo asiguswe na uamuzi wake ni sahii lakini huku ni kuifanya ideology iwe dead if not existinct. Lakini hata hivyo bunge linegeendelea kujadili nini wakati watu wanakufa? Chombo cha usafiri ni mtakuja ni ufinyu wa fikra ukidhani madhali walitokea Dar kwenda Zanzibar basi walikuwa ni wa upande mmoja wa nchi kwa hiyo hawakuwepo wa Kongwa, Gairo, Dodoma kiasi cha kuwafanya wabunge wajumuike na wapiga kura wao. Amka, toka ndani ya box na kuwa karibu na watu
 
Last edited by a moderator:
Hayo mambo yanahusiana vipi na shughuli za bunge? Ajali ikitokea vikosi vya uokoaji, polisi wanajeshi na wafanyakazi wengine wanaohusika ndio wanaoshughulikia. Sasa wabunge waahirishe kikao ili wafanye nini?.. Itasaidia nini? Kama Hamad alikuwa na udhuru si angeenda tu kuwapa pole wanajimbo wake, haijalishi saa nne asubuhi au saa kumi na mbili jioni.
Ni mambo ambayo kusema kweli hayana maana yeyote zaidi ya kuleta mtafaruku ndani ya bunge...... Pointless!

This reflects the apex of your analytical capacity and understanding of the political mathematics and acrobatics!! Pole. Wabunge ni wanasiasa, katika matukio ya aina hiyo wanasiasa wanayo moral obligation ya kuwa karibu sana na wapiga kura wao; majanga kama haya huibua hisia kali na yaweza kusababisha uvunjifu wa amani ikihisiwa kuwa viongozi wao hawajali shida zao, majuzi tumemshuhudia Prezo Obama akiweka pembeni kila shughuli ya taifa hilo kubwa kwenda kuwafariji wananchi wake wa jimbo la Colorado ambao walipata janga la moto wa kiangazi, a week ago Preso Putin wa Russia aliacha kazi zote katika taifa hilo kubwa pia kwenda kuwafariji wanachi wake kusini mwa nchi hiyo waliokumbwa na janga la mafuriko na maporomoko ya ardhi; hiyo ni kazi muhimu kwa wanasiasa vinginevyo hawataeleweka kwa wapiga kura wao hata kidogo.
tatizo la makinda lilikuwa kudhani waluiokufa ni wana Chadema kwa hiyo sio kitu!!!!!!!!!!!!!! kawatambua wazenj.
 
Sasa hawa jamaa mbona wanagongana na figure za waliokufa............ kila moja ana namba yake. Hizo source ni akina nani?? Inakuwaje waziri, serikali na vyombo vya habari vinatoa namba inayotofautiana kiasi hicho?? CCM wanaweza kuishia na hiyo namba 6 ili kuonyesha umma kuwa maafa hayakuwa makubwa.


BOTI YAZAMA NA ABIRIA 250, KATI YAO 60 WAHOFIWA KUFARIKI DUNIA
Waandishi Wetu
WATU 60 wanahofiwa kufa maji na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya boti iliyokuwa imebeba abiria wanaokadiriwa kufikia 250 ikitokea Dar es Salaam kwenda Unguja, Zanzibar kuzama baharini.Hii ni ajali ya pili mbaya kutokea katika kipindi cha miezi 10 tangu ilipotokea nyingine ya Meli ya Mv Spice Islander ambayo inakadiriwa kuwa watu wapatao 200 walifariki dunia.Boti hiyo iliyoondoka jana Dar es Salaam majira ya saa 6:00 mchana na kutarajiwa kufika Bandari ya Malindi, Zanzibar saa 9:30 jioni, ilizama eneo la Pungume karibu kilomita 48 kutoka Bandari ya Zanzibar.
Inaelezwa kuwa, ilianza kuzama saa 7:30 mchana kutokana na kupigwa na mawimbi mazito ya bahari.

Hata hivyo, Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Zanzibar, Hamad Masoud Hamad alithibitisha vifo vya watu 12 hadi vilivyoripotiwa ilipotimu saa 12:30 jioni jana wakati kazi ya uokoaji ikiwa inaendelea.

Baadaye saa 1:00 Ofisa Habari na Mawasiliano wa Wizara hiyo, Nafisa Madai aliwaambia waandishi wa habari kuwa idadi hiyo ilikuwa imeongezeka hadi kufikia 24 na majeruhi walikuwa 145.Madai alisema wakati boti hiyo inaondoka Dar es Salaam, ilikuwa na abiria 250 wakiwamo watoto 31 na wafanyakazi tisa.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Said Shaaban akizungumzia ajali ya boti hiyo ya Mv Skad, inayomilikiwa na Kampuni ya Meli Seagull alisema: "Vikosi vya uokoaji tayari vinaelekea katika eneo hilo ili kusaidia majeruhi na kufuatilia yaliyotokea."

Maofisa kadhaa wa Serikali wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi walifika Bandari ya Malindi na Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu Zanzibar, Hamad Masoud Hamad aliongoza msafara wa viongozi wengine kwenda katika eneo la tukio.

Awali, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema kuwa, hadi alipopata taarifa, watu waliokuwa wamefariki dunia ni saba na 124 ndiyo waliokuwa wameokolewa. Alisema meli hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 300 na waliosafiri siku ya tukio hawazidi 250.

Awali, taarifa zilieleza kuwa watu 10 waliokolewa na maiti zaidi ya 60 zimenasa katika boti hiyo na kuvifanya vikosi vya uokoaji vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi na KMKM kupata wakati mgumu kwenye zoezi la uokoaji.Kazi ya kuokoa maisha ya watu waliozama kwenye boti hiyo na kuopoa maiti ilifanywa kwa kutumia boti nne zikiwamo za Serikali na zile zinazomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine.Hata hivyo, ilielezwa kwamba boti za polisi zilichelewa kwenda katika eneo la tukio kutokana na kukosekana kwa mafuta.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufika bandarini, Balozi Seif aliwataka wananchi kutulia na kusubiri wakiwa nyumbani wakati Serikali ikifanya juhudi za uokoaji.
Shughuli nyingi za usafiri zilivurugika kutokana na tukio hilo na Meli ya Mv Sea Bus ililazimika kufuta safari zake kupisha kazi hiyo ya uokoaji.
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imesema inafuatilia tukio hilo kwa karibu ili kubaini chanzo.
Ofisa Uhusiano wa Sumatra, David Mziray alisema jana muda mfupi baada ya ajali hiyo kuwa, wanawasiliana na Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini (MRCC), ili kupata taarifa kamili kabla ya kuujulisha umma.
Spika Makinda achafua hali ya hewa

Kutokana na ajali hiyo, muda mfupi baada ya kipindi cha jioni kuanza, Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed alisimama na kuomba mwongozo kwa kutumia Kanuni ya 47(3) kulitaka Bunge lipitishe Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mafungu bila ya kutolewa ufafanuzi ili wabunge waweze kupata muda wa kujadili tukio hilo.
Hata hivyo, Spika Anne Makinda alipinga hoja ya Hamad na kutaka Bunge liendelee akieleza kwamba kanuni hiyo imekuwa ikitumiwa vibaya na kwamba tayari ameshawasiliana na waziri husika na kwamba taarifa kamili zitakapopatikana angelitaarifu Bunge.
Baada ya kauli hiyo Spika Makinda aliruhusu shughuli za Bunge ziendelee na kumwita Silima kutoa ufafanuzi wa hoja za wabunge.

Lakini wakati Naibu Waziri huyo akielekea kutoa hotuba yake, wabunge wote wa CUF, Chadema na baadhi wa CCM walitoka nje na kwenda katika Ukumbi wa Msekwa ili kupeana taarifa za ajali hiyo na kupanga mikakati ya jinsi ya kutuma ujumbe wa haraka kwenda Zanzibar kushirikiana na waokoaji.
Ukumbi huo uligeuka kuwa wa maombolezo kwa muda baada ya wabunge wengi kuangua vilio pale walipopewa taarifa rasmi za ajali hiyo.

Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid alieleza kwa ufupi tukio lilivyo na kwamba wangemwomba Waziri Mkuu, Mizengo Pinda awasaidie ndege ya Serikali ili waweze kwenda Zanzibar kujumuika na wenzao katika tukio hilo.

Baada ya Hamad kumaliza alisimama Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia ambaye alijaribu kuwatuliza wabunge akisema kuwa, meli inaweza kuzama lakini watu wasipoteze maisha kutokana na kuchukua muda, kauli ambayo ilipingwa na wabunge wengi.Mbunge wa Mji Mkongwe (CUF), Ibrahim Sanya alimshutumu Spika Makinda akisema, amekosa hisia na hajui kwamba kuzama kwa meli ni janga la kitaifa.
"Kwa hili hata nikikutana na Spika nitamwambia kweli ameniudhi. Sihitaji ubunge kama hali yenyewe ndiyo hii na tutapiga kura ya kutokuwa na imani na Spika," alisema Sanya.

Wakati hayo yakitokea, katika Viwanja vya Bunge baadhi ya wabunge na mawaziri walionekana wakiwa katika vikundi wakijadili suala hilo, huku wengine wakipinga uamuzi huo wa Spika.

Wakati hayo yakiendelea katika Ukumbi wa Msekwa, Bunge lilikuwa likiendelea kumsikiliza Silima akijibu hoja za wabunge na baada ya kumaliza, Spika Makinda alimwita mtoa hoja, Waziri Nchimbi naye kujibu.Lakini badala yake, alitumia fursa yake kuondoa hoja ya Makadirio ya Matumizi ya wizara yake ili kutoa fursa kwa Bunge kujadili ushiriki wake katika tukio la kuzama kwa boti hiyo.

Dk Nchimbi alitumia Kanuni ya 58 (5) ambayo inamtaka mtoa hoja kusimama na kutoa hoja ya kuondoa mezani hoja yake kama kuna jambo la dharura.

"Mheshimiwa Spika, natumia Kanuni ya 58 (5) ambayo inamtaka Waziri kusimama na kutoa hoja ya kuondoa mezani hoja yake kama kuna jambo la dharura," alisema Dk Nchimbi.Dk Nchimbi aliendelea: "Ikumbukwe Mheshimiwa Spika, muda mfupi kabla ya kuingia hapa ndani uliniita mimi na Naibu Waziri ukataka tukueleze hali ya ajali hiyo na kwa wakati huo Kamishna wa Matukio Zanzibar alikuwa eneo la tukio. Sasa basi, kutokana na agizo lako, ni imani yangu kwa muda aliotumia Naibu Waziri unatosha kuendelea kufuatilia jambo hilo."

Baada ya kutoa maelezo hayo, Wabunge wote 49 waliokuwa wamebaki katika ukumbi walisimama kuunga mkono hoja.
Baada ya hapo, Spika Makinda aliwahoji na kwa kauli moja waliridhia kuahirishwa kwa kikao hicho wakati huo ikiwa saa 11:31 hadi leo saa 3.00 asubuhi, huku akiitisha kikao cha dharura cha Kamati ya Uongozi ya Bunge jana hiyohiyo kujadili suala hilo.

Akizungumza baada ya kikao hicho cha Kamati ya Uongozi, Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel alisema, limeamua kufuta kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu na kwamba kikao cha Bunge kitaendelea leo asubuhi kuanzia saa 2:00 kupokea taarifa ya Serikali kisha watajadili mustakabali wa vikao vya Bunge.Kamati hiyo pia iliamua kutuma ujumbe wa wabunge kwenda Zanzibar kuwafarijiwa wale wote walioathiriwa na ajali hiyo.

Ni ajali ya pili
Ajali Mv Spice Islander ambayo ilitokea Septemba 10, 2011 ikitokea Unguja kuelekea Pemba, ilizama kutokana na kuzidisha abiria ambao kwa mujibu wa tume iliyoundwa kuchunguza ajali hiyo, ilikuwa na abiria 2,470 na mizigo wakati uwezo wake ulikuwa kubeba abiria 600 tu.
Tume hiyo iliyoundwa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ilibaini kwamba ajali hiyo ilisababishwa na uzembe, kutofuata sheria na rushwa katika Bandari ya Zanzibar.

Tume hiyo ilipendekeza wahusika wa ajali hiyo kuchukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu.
Nohodha wa meli hiyo, Said Abdallah Kinyangite, wamiliki wa meli, watendaji wa Bandari ya Zanzibar walifikishwa katika Mahakama Kuu ya Zanzibar ambako kesi zao zinaendelea.

Imeandikwa na Salma Said, Zanzibar, Neville Meena, Habel Chidawali na Boniface Meena, Dodoma; Raymond Kaminyoge, Aidan Mhando, Dar es Salaam.
 
Kwa reasoning hii basi hata msibani tusiwe tunaenda
maana kwenda kwetu hakuwezi kumsaidia marhem
Bora tuwaache wachimba kaburi na waosha maiti tu
Sisi tuendelee na shughuli zetu za kawaida. wasemaje?

Unajua mwali tatizo ni wabunge kutaka umaarufu wakati watu wanaumia. Kuahirisha bunge siyo kuonyesha kwamba wabunge ndiyo wanajali. Maana baada ya hapo walianza kuzurura tu pale nje. Suala lilikuwa kuahirisha hoja ya bajeti ya wizara mambo ya ndani halafu waziri anayeshughulikia na hayo masuala ya usafiri atoe statement (wenzetu wa kenya huita ministerial statement). Hapo wabunge wangetaka Waziri aseme hadi wakati ule kuna juhudi gani za uokozi zinazofanyika, kwa wakati ule kuna wangapi wamefariki na wangapi wamejeruhiwa na nini kinafanyika kuokoa maisha ya majeruhi nk. Pia Waziri angetakiwa kueleza kwa nini hizi ajali zinatokea mara kwa mara na hatua zipi zitachukuliwa ili kuzuia hayo mambo. Hapo wabunge wangekuwa wamewasaidia sana wananchi badala ya wao kutoka na wananchi kuanza kutegemea vyombo vya habari.

Kwangu mimi nadhani wabunge walitakiwa kuchukua jukumu la kiuongozi ili kuifanya serikali iwajulishe wananchi badala ya wao kuanza kukimbilia kutoa pole na kuiacha serikali itoe taarifa tu pale inapojisikia. So they were wrong, they are just doing a moral blackmail.
 
Hayo mambo yanahusiana vipi na shughuli za bunge? Ajali ikitokea vikosi vya uokoaji, polisi wanajeshi na wafanyakazi wengine wanaohusika ndio wanaoshughulikia. Sasa wabunge waahirishe kikao ili wafanye nini?.. Itasaidia nini? Kama Hamad alikuwa na udhuru si angeenda tu kuwapa pole wanajimbo wake, haijalishi saa nne asubuhi au saa kumi na mbili jioni.
Ni mambo ambayo kusema kweli hayana maana yeyote zaidi ya kuleta mtafaruku ndani ya bunge...... Pointless!

Ubongo wako utakuwa "shake before use"
 
Jamani Wana JF, msimshambulie sana huyu mama Makinda ni MGUMBA hawezi kuwa na uchungu wa wana wa Nchi.
Wagumba waliokosa watoto bila mapenzi yao wana uchungu na wana wa nchi. Huyu ni tofauti na hao.
 
Nianze kwenye nyekundu, how?
Kama unazungumzia bunge kwa sababu limechaguliwa directly na wananchi,je limechaguliwa ili likafanye nini?
Kumbuka kuwa mbunge siyo kiongozi wa wananchi wa jimbo lake, ni mwakilishi tu kwenye utungaji wa sheria. Zaidi ya hapo, ni mwananchi kama wananchi wengine. Sasa kama hakimu mkazi wa mahakama ya kisutu anafanya kazi (as a regular citizen) kwanini mbunge asifanye kazi?
Mbunge siyo kiongozi, siyo mtekelezaji na wala siyo mfanyakazi wa utendaji. Kuhudhuria kwake msiba ni kama wananchi wengine .... baada ya kazi unless awe anahitajika kwenye kikao cha halmashauri ya wilaya/manispaa/jiji husika.
Mbunge huwakilisha jimbo na wanajimbo wake na rais huwakilisha taifa as a whole. Kwa hiyo Ndesamburo kususa kwa sababu hakupewa off ya kwenda unguja msibani (I doubt if he'd have gone newayz) haileti mantiki. Labda kama mnataka ku-force mambo, but nah!,.... sorry.
Acha kujenga hoja zisizo na tija wewe nyangau gamba mkubwa usiye na huruma na roho za watu shwain
 
This reflects the apex of your analytical capacity and understanding of the political mathematics and acrobatics!! Pole. Wabunge ni wanasiasa, katika matukio ya aina hiyo wanasiasa wanayo moral obligation ya kuwa karibu sana na wapiga kura wao; majanga kama haya huibua hisia kali na yaweza kusababisha uvunjifu wa amani ikihisiwa kuwa viongozi wao hawajali shida zao, majuzi tumemshuhudia Prezo Obama akiweka pembeni kila shughuli ya taifa hilo kubwa kwenda kuwafariji wananchi wake wa jimbo la Colorado ambao walipata janga la moto wa kiangazi, a week ago Preso Putin wa Russia aliacha kazi zote katika taifa hilo kubwa pia kwenda kuwafariji wanachi wake kusini mwa nchi hiyo waliokumbwa na janga la mafuriko na maporomoko ya ardhi; hiyo ni kazi muhimu kwa wanasiasa vinginevyo hawataeleweka kwa wapiga kura wao hata kidogo.
tatizo la makinda lilikuwa kudhani waluiokufa ni wana Chadema kwa hiyo sio kitu!!!!!!!!!!!!!! kawatambua wazenj.
President = head of the executive.
Wabunge, waliendelea na vikao vyao.
Sana sana umejidhihirisha kuwa wewe ni limbukeni anayefikiri anajua sana .... very dangereous combination
 
Tujifunze katika hili, Makinda hakuwa sahii kwa maneno bali alikuwa sahii wa decision aliyochukua, japo watanzania hawawezi elewa! Tunajijua sie wabongo tunapenda sana unafiki! Sioni logic ya mtu kukurupuka kutoka bungeni, then akaishia kaunta. Dom Hotel anapiga simu tuu!

Sidhani hata ukiwa ofisini ukaambiwa baba yako kafa unakimbia hovyo bila kuuliza vizuri na ku handle over kazi za watu!

Au kama mama yako anafanyiwa operesheni utashinda umesimana mlango wa theatre unasubiria tuu!
 
Tuachwe tupumue hamuna udugu,ajali hii ni janga la taifa ililazimika kikao kimalize au kifungwe wabunge wakaungane na wananchi wao,lakini wapii ? Kwa wale wazanzibari wenye kuukumbatia muungano sasa wamejionea wenyewe,watanganyika sio ndugu zetu ni majirani zetu tu,muungano basi.
 
Unajua mwali tatizo ni wabunge kutaka umaarufu wakati watu wanaumia. Kuahirisha bunge siyo kuonyesha kwamba wabunge ndiyo wanajali. Maana baada ya hapo walianza kuzurura tu pale nje. Suala lilikuwa kuahirisha hoja ya bajeti ya wizara mambo ya ndani halafu waziri anayeshughulikia na hayo masuala ya usafiri atoe statement (wenzetu wa kenya huita ministerial statement). Hapo wabunge wangetaka Waziri aseme hadi wakati ule kuna juhudi gani za uokozi zinazofanyika, kwa wakati ule kuna wangapi wamefariki na wangapi wamejeruhiwa na nini kinafanyika kuokoa maisha ya majeruhi nk. Pia Waziri angetakiwa kueleza kwa nini hizi ajali zinatokea mara kwa mara na hatua zipi zitachukuliwa ili kuzuia hayo mambo. Hapo wabunge wangekuwa wamewasaidia sana wananchi badala ya wao kutoka na wananchi kuanza kutegemea vyombo vya habari.

Kwangu mimi nadhani wabunge walitakiwa kuchukua jukumu la kiuongozi ili kuifanya serikali iwajulishe wananchi badala ya wao kuanza kukimbilia kutoa pole na kuiacha serikali itoe taarifa tu pale inapojisikia. So they were wrong, they are just doing a moral blackmail.

Uko sahihi kuhusu ministerial statement na Hamad Rashid alikuwa anaongea along those lines. Aliomba Spika aruhusu bunge lipitishe bajeti ya Home Affairs kwa mafungu ili kuruhu bunge lijadili jambo la dharura lililotokea na lenye manufaa kwa umma then baadae wabunge wengine wapate pia fursa ya kwenda kwenye tukio.

Kanuni zinaruhusu lakini Spika si tu alikataa ila kubwa alikataa kwa kutumia kauli ya kuudhi sana (na hii italeta shida ngoja watu wamalize kuzika).

Baada ya kukataa wabunge wa upinzani na baadhi CCM-zanzibar wakatoka nje. Huku nyuma wakawa wamebakia wabunge 49 tu, idadi ambayo ni chini ya threshold inayotakiwa kupitisha hoja.

Still, Spika na mawani yake hakuliona hilo hadi pale Nchimbi alipogundua idadi ndogo ya wabunge na kuindoa hoja yake mezani kwa kutumia kanuni za bunge.

Hivyo, technically speaking Spika hakuahirisha bunge, ila bunge lilikosa cha kujadili kwa sababu serikali iliondoa hoja yake mezani! Na hakukuwa na kitu kingine cha kujadili kwa siku hiyo so they had to go home/hotel rooms etc.

Hili kosa la Spika linaweza kutumika kama case study nzuri kuelezea umuhimu wa kuwa mtu mwenye ujuzi wa sheria kuongoza legislatures.lakini hata kwa kutumia busara ndogo sana bunge haliwezi kuendelea na kama kawaida in the midst of a national disaster. Walitakiwa wabadilishe hoja na kujadili ajali ya meli pamoja na hatua za haraka ili kukabiliana na mkasa huo.

Kwa kumalizia, spika na team yake wanatakiwa sasa wakubali udhaifu wao na wajifunze kutumia lugha za heshma bungeni. Wabunge wote wako pale kwa nujibu wa sheria na ni watu wazima, haiwezekani spika na wenzake kuendelea kuwa-treat kama watoto au watu wasioelewa mambo. Hasa Spika anatakiwa aachane kabisa na huu mtindo wa kudhani kuwa ni yeye pekee mwenye uwezo wa kuelewa kanuni za bunge. Zile kanuni sio manual ya kutengeneza rocket, zinaeleweka kirahisi sana. Lakini pia huwezi kusoma kanuni in isolation bila kuzingatia katiba. Bunge la sasa lina udhaifu mkubwa kwenye uelewa/appreciation ya sheria. Busara (or lack of it) ndio inaonekana kushika usukani. Matokoeo yake ndiyo haya tunayoona sasa kwamba bunge linaanza kupoteza ligitimacy mbele ya wananchi. Nani anatakiwa kuwajibika kwa hapa tulipofikia?
 
More than 100 missing after Zanzibar ferry sinks

Rescue workers fought rough seas on Thursday to search for more than 100 people missing after an overcrowded ferry sank near the Indian Ocean archipelago of Zanzibar, but hopes of finding survivors were slim.

At least 38 people, including an American citizen, were confirmed dead and 145 were rescued after the MV Skagit/Kalama passenger boat capsized on Wednesday around midday near Chumbe island, west of Zanzibar.

Zaidi hapa More than 100 missing after Zanzibar ferry sinks | Top News | Reuters
 
Hivyo, technically speaking Spika hakuahirisha bunge, ila bunge lilikosa cha kujadili kwa sababu serikali iliondoa hoja yake mezani! Na hakukuwa na kitu kingine cha kujadili kwa siku hiyo so they had to go home/hotel rooms etc.

Hili kosa la Spika linaweza kutumika kama case study nzuri kuelezea umuhimu wa kuwa mtu mwenye ujuzi wa sheria kuongoza legislatures.lakini hata kwa kutumia busara ndogo sana bunge haliwezi kuendelea na kama kawaida in the midst of a national disaster. Walitakiwa wabadilishe hoja na kujadili ajali ya meli pamoja na hatua za haraka ili kukabiliana na mkasa huo.
Mkuu unaweza ku-fabricate story ili i-fit maoni yako, and I can do the same.

Kusema kuwa "Technically bunge liliahirishwa based on quorum unaweza ukawa sahihi, ila hansards hazitaonyesha hilo na bunge liliahirishwa kutokana na ajali iliyokuwa inaendelea, ambayo ilimhusu waziri aliyeleta hoja.Speaker alishaongea na waziri kuhusu kuwapo kwa ajali na wakakubaliana kuwa taarifa kamili (kiserikali) itakapotoka, wanaweza kuliongelea hilo bungeni( hiyo ni kabla ya Hamad kutoa hoja).

Kabla ya taarifa kutoka serikalini, mbunge wa Wawi akatoa taarifa kuhusu ajali hiyo.

Sasa hapo ndipo siasa na utekelezaji vinapogongana. Kwa kuwa umepigiwa simu au umeona tukio kwenye Tv, haimaanishi kuwa officially hilo tukio limetokea, kuna logistics ambazo kama wewe upo serikalini unatakiwa uzijue na ufuate protocols zilizopo.
Ukipigiwa simu haimaanishi kuwa ndiyo taarifa rasmi. Kwa mfano mzee Paw angempigia simu Hamad kuwa Tanzania imevamiwa na Comoro na Hamad akataka kusitisha hoja kisa amepata simu kutoka kwa mzee Paw, atakuwa amekosea.

Speaker alikuwa na habari hiyo, ila ilibidi waziri baada ya kupata taarifa rasmi ndiyo angeomba bunge lijadili cha kufanya (kupiga picha kwa ajili ya facebook). Na siyo mbunge aliyepewa taarifa na jirani yake.

Kwa hiyo kususa kwa wabunge ni ulimbukeni wa sheria na taratibu za kazi (uswahili mwingi) kwa upande wa wabunge. Hasa wa CHADEMA.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom