Kwa mpango huu nini hatima ya TRA juu ya biashara yangu

Hawawezi kufunga.
Wakifunga wapeleke mahakamani.
Acha uoga. Pambana nao. Waambie napenda kulipa kodi. Ila makadirio yenu ya kodi ni makubwa kwangu. Tukaeni tufanye tena tathmini.
UKIONA WANAZINGUA WAAMBIE NATAKA KULIPA KODI KWA MFUMO WA EFDS.
WAKIKUPA AKILI KICHWANI KWAKO.
Pamoja mkuu
 
Sio kukwepa mkuu shida inakua kwenye makadirio km mimi nilikadiriwa kikubwa mpaka nikashindwa kulipa
Yaani kama ulishaingia kwenye system jitahidi tu ulipe kadri unavyochelewa deni linaongezeka...lipa kodi kwa maendeleo ya nchi
 
Kwenye mwezi wa tatu mwaka huu baada ya kujimeki sana niliamua kufungua biashara fulani baada ya vyuma kukaza sana.
Ila changamoto ikaja baada ya kuanza bishara eneo nililopo ikawa tra kila iitwayo leo lazima watie tim kiasi kwamba nililazimika niwe nafunga hali iliyopelekea maisha yazidi kua magumu zaidi na hapo ukizingatia hela yote niliyonayo niliingiza ktk biashara.
Nikaamua nifatilie tin ikiwezekana na hata leseni ili niweze kupambana na hali yangu vizuri ila nilipoenda tra ndipo nilipochoka maana msingi wangu ulikua ni laki 7 na wao wakanikadiria nilipe laki 6 na 20 na senti kadhaa kwa mwaka na wakanipa document zao kiasi ambacho inabidi nilipe kwanza baada ya kugawa huo mwaka kua kila baada ya miezi mitatu nikalipe,kwa awamu ya kwanza ilibidi nilipe laki mbili na mashilingi kibao kitu ambacho kwangu ulikua mlima mrefu nisioweza kuupanda.

Mwisho wa siku niliamua kuendelea na biashara maana sikua na namna nyingine ya kuniingizia kipato,biashara iliendelea japo kwa kukimbizana sana na tra kila ukiskia wanakuja ilinibidi nifunge ili kuepusha shari.Baada ya kukomaa sana kwa takribani miezi nane sasa nataka nifatilie tena ili niweze kupata tin na leseni yake.
Hapa ndipo ninapotaka kujua je?nikijepeleka na kusema nilikuja ila sikurudi tena kwa kua documents bado ninazo si nitalundikiwa mikodi kibaaao na penat za kutosha kiasi nitashindwa kumudu kulipa na je? ni vp nikisema nianze process upya si nitagundulika maana kule hadi picha nilipigwa kipindi kile nilivyofuatilia kabla ya kula chochoro kwa kipindi chote hiki.

Nawasilisha na pia msaada kwa mjuvi wa haya mambo
Pole sana mkuu
Anyway nicheki hapa email:iconsultbuzness@gmail. com! Hotline: 0659211222\0777 777 766
 
Sijui utaratibu wa kodi upoje mtaji laki 7 kodi laki 6
Mtaji wa lakini 7 (kama huuzi madawa ya kulevya) ni mdogo mno hata faida unayopata haistahili kulipiwa kodi. Unapaswa kujiandikisha kama mlipa kodi (TIN) na unapaswa kupeleka taarifa (return) kila baada ya miezi mitatu. Katika hiyo return unajikadilia faida utakayopata ambayo ndiyo inalipiwa kodi. Kwa kiwango chako cha mtaji nahisi faida yako itakuwa ndogo na hivyo kuwa nje ya wigo wa kutozwa kodi. Kuwa na leseni ni lazima lakini unaipata baada ya kumalizana na TRA.
 
Shida ya huu mpambano mimi nimeshika kwenye makali na ukisema uwaache wafunge biashara naona hasara itakua upande wangu zaidi kuliko kwao
Kama hujawahi kupeleka maombi ya TIN, yaani huna failing TRA, nenda kama vile unataka kuanza biashara. Labda awepo mtu anayejua kuwa unayo biashara tayari. Vinginevyo anza upya. Watu wa TRA wanakadiria kodi kubwa wakiona huna uelewa wa kutosha na mambo ya kodi. Pata msaada/ushauri wa kitaalamu. Utaulipia.
 
Back
Top Bottom