Kwa moyo mkunjufu kabisa, IGP Sirro shtuka. Kuna hatari mbele yako!

polokwane

JF-Expert Member
Dec 16, 2018
3,359
5,808
IGP siro nimekufahamu tangu kitambo sana na hasa tulipo kuwa depo miaka fulani.

Ukiwa kama brother wangu kwani umenipita miaka kadhaa, Tafadhari sana tupia jicho haya mauaji na matukio ya unyanyasaji raia yanayofanywa na askari wako kila uchao kwa kisingiazio cha uhalifu.

Brother unatupiwa jicho tena jicho kali sana na nadhan hujagundua hilo na kama hujagundua basi nimekuibia kidogo kajambo haka.

Kuna hatari iliyoko mbele yako brother wangu.

Brother taarifa zinakusanywa kwa kasi sana tena zenye maelezo na vielelezo huku zikiambatanishwa na utetezi wa ma RPC wako wa mikoa.

Unakusanyiwa data brother na hatua unazo chukua dhidi ya hawa askari wako.

Vipigo vya askari dhidi ya raia vina kusanywa tena kwa maelezo ya Pande zote mbili yaani upande wa askari wako kupitia MA RPC NA OCD na upande wa raia walio shuhudia matukio.

Wakusanya taarifa wanaenda mbali zaidi maana wana kusanya hadi picha na video kama zipo kutoka kwa raia walio kuwepo maeneo ya matukio.

Brother fanya mikakati brother wangu nakupenda sana kwani ulinipa ujuzi mwingi sana wa kikazi maeneo mengi tuliyo kutana kikozi na kikazi

Kaka achana na wana siasa hawa jaribu wakati mwingine kusimamia weledi na miiko ya kazi kwani natabiri kuna muda utaachwa peke yako kujibia mambo mengi na wana siasa hao hawata kuwa na namna ya kukusaidia.

Brother sirro mimi nipo nawe na unajua hilo nakupa kipande tu cha yajayo ambayo hayata furahisha.

"Nakala"
 
Huyu, kamanda yupo huku jamvini mkuu?
Maybe pengine anapita huku, kama ndio hivyo basi ujumbe umefika.


Sent using Vertu Signature Cobra
Yupo mkuu tena yupo yeye na vijana wake wengi mkuu.

Na haiwezekani akakosa kuwepo humu hasa kwa kazi yake na nafasi yake kwani jamiiforum huwafaa sana jeshi la polisi hasa katika investigations.

Maana kuna matukio mengine wanaweza kupata pa kuanzia kupitia jamiiforum, hivyo usijali kuhusu hilo.
 
Ni heri kwake aelewe ulichosema!
Walikuwepo kina Mahita, mwema n.k
 
Hujamsaidia huyo rafiki yako kama kweli unampenda zaidi kupika tu majungu then awaone wasaidizi wake yaani ma RPC kuwa ni wabaya kwake. Ningekuwa mimi Sirro ningeanza na wewe kwanza kukushughulikia.
 
Hujamsaidia huyo rafiki yako kama kweli unampenda zaidi kupika tu majungu then awaone wasaidizi wake yaani ma RPC kuwa ni wabaya kwake....ningekuwa mimi Sirro ningeanza na wewe kwanza kukushughulikia
Kwa akili ya mjinga yeyote na aliye mpumbavu wa akili, mali, hekima, na busara hakika ni lazima awe na mawazo ya mfano wako

Si vibaya kwani msafara wa mamba kenge wamo pia na hili jukwaa linakusanya aina zote za watu.

Nilidhani ungekuwa na busara tena sana kama ungeniuliza hivi, "kwanini umeamua kuleta huu uzi huku ili hali IGP SIRRO mnafahamiana??"" Kidogo hapo ningekuona una kichwa, lakini kwa ujinga ulio toa wewe hakika yafaa nilivyo kujibu
 
HUU sio muandiko wa kiaskari. Hujawahi ata kupitia mafunzo ya mgambo, askari huwa aandiki kama mtu anae kimbizwa na tembo. Hakuna lolote litakalo mkuta IGP kwa maana kila lifanywalo na mtoto jua fika lina baraka kutoka kwa BABA yake.
 
HUU sio muandiko wa kiaskari....hujawahi ata kupitia mafunzo ya mgambo....askari huwa aandiki kama mtu anae kimbizwa na tembo....hakuna lolote litakalo mkuta IGP kwa maana kila lifanywalo na mtoto jua fika lina baraka kutoka kwa BABA yake.
Wakati huo rudi darasani kamuulize mwalimu wako je? kila Askari ni mwandishi wa habari? Ukikosa jibu hapo nenda kituo chochote cha polisi kilichopo karibu nawe uliza swali hilo hilo . Ukipata jibu njoo tuendelee na mjadala

Wakati huko kumbuka au pitia upya uzi wangu wooote ukipata maha nilipo andika mimi ni askari njoo nikupe 60% ya mali zangu

Na kingine nukuondoe tu ujinga si kila aliyepo depo anachukua mafunzo ya uaskari.
 
Wakati huo rudi darasani kamuulize mwalimu wako je? kila Askari ni mwandishi wa habari? Ukikosa jibu hapo nenda kituo chochote cha polisi kilichopo karibu nawe uliza swali hilo hilo . Ukipata jibu njoo tuendelee na mjadala

Wakati huko kumbuka au pitia upya uzi wangu wooote ukipata maha nilipo andika mimi ni askari njoo nikupe 60% ya mali zangu

Na kingine nukuondoe tu ujinga si kila aliyepo depo anachukua mafunzo ya uaskari.
Huna mali yoyote, wenye mali huwa atujitapi...narudia tena ata mlango wa depo wewe hujawahi kuukanyaga. Hakuna lolote litakaloweza kumpata IGP. Na ni kuhakikishie tu kuwa IGP Sirro atastaafu salama kama watangulizi wake walivyostaafu kwa heshima, hivi kuna IGP aliyepata kashfa kama OMARI MAHITA? yupo wapi hivi sasa? kuna baya lililowahi kumkuta?
 
Hizi kauli za MaRPC wengi eti alijeruhiwa kwa kupigwa risasi alipoenda/walipoenda kuonyesha silaha na akafariki/wakafariki akiwa njiani akipelekwa hospitali wakati a au mtuhumiwa alijaribu kunyang'anya silaha akiwa kituoni ni nyimbo za Makamanda wengi na zina ukakasi mkubwa
 
huna mali yoyote...wenye mali huwa atujitapi...narudia tena ata mlango wa depo wewe hujawahi kuukanyaga...hakuna lolote litakaloweza kumpata IGP...na ni kuhakikishie tu kuwa IGP sirro atastaafu salama kama watangulizi wake walivyostaafu kwa heshima....ivi kuna IGP aliyepata kashfa kama OMARI MAHITA...? yupo wapi hivi sasa...? kuna baya lililowahi kumkuta?
Mkuu usimdharau Binadamu aliye hai. Kuna siku atakuwa na msaada kwako. Yeye katoa ushauri wake kwa mtu wake. Sio ajabu ni miongoni mwa wale wanaokusanya data. Lkn kwa moyo wake wa upendo kwa mtu wake akaona amtonye. Sasa ni wajibu wake kuchukua ushauri na kuufanyia kazi au kuacha humu humu JF.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huna mali yoyote...wenye mali huwa atujitapi...narudia tena ata mlango wa depo wewe hujawahi kuukanyaga...hakuna lolote litakaloweza kumpata IGP...na ni kuhakikishie tu kuwa IGP sirro atastaafu salama kama watangulizi wake walivyostaafu kwa heshima....ivi kuna IGP aliyepata kashfa kama OMARI MAHITA...? yupo wapi hivi sasa...? kuna baya lililowahi kumkuta...?
Umezoea na unapenda kuishi kimazoea.Mimi huwa naanzisha ubishi kwa nia ya kuchokoza jambo lakini weye umejaa bezo,majigambo na uhuniuhuni wa akili na fikra.Usipende kukaza kiuno kubisha tu ili mradi umebisha.Ulipaswa kumchokoza kwa maswali ili upate nini anamaanisha na wala si kwa ulichokiandika.
 
Back
Top Bottom