MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,975
Rais Magufuli ninakupongeza wewe na wale wote waliokushauri ili kumteua Prof. Kabudi katika nafasi ya Waziri wa Katiba na Sheria.
Prof. Kabudi na timu yake ya wanasheria wameanza kutoa matunda yao mema kwa taifa kupitia kazi zao kama zilivyobainika kwenye miswada hii.
Kwa miswada hii iliyopelekwa bungeni ili kujadiliwa na kuwa sheria haina maneno mengi lakini yaliyopo yamejaa umuhimu mkubwa kisheria kwa maslahi ya taifa, sina shaka kwa kiwango kikubwa taifa litakuwa limeingia katika ukurasa mpya katika safari ya kulinda maliasili zake ili zinufaishe taifa kwa kizazi hiki na kijacho.
Kama Rais Magufuli alivyosema, ‘’tulichelewa lakini kama taifa tumeamua kufika’’ na kwa miswada hii ninatumaini tutafika.
Yaliyopo katika miswada hii ya sheria ni pamoja na;
>>Bunge kupitia mikataba yote ya maliasili za nchi kuangalia maslahi ya Watanzania na baada ya kubaini masharti hasi katika mikataba hiyo Bunge linaweza kuitaka Serikali kufanya majadiliano upya na upande wa pili wa mkataba ili kuondoa masharti hayo.
>>Kuweka utaratibu wa bunge kufanya mapitio na maridhiano ya mikataba.
>>Kufanya mapitio madaraka ya Waziri na Kamishna wa madini.
>>Kuimarisha mifumo ya uthibiti na uwajibikaji katika sekta ya madini na petrol.
>>Kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato kwenye sekta ya madini na petrol.
Kwa wale wanataka kuisoma hiyo miswada Gonga hapa;
LINK>>Miswada ya marekebisho ya sheria za maliasili
Hizi ni baadhi ya contents zilizoko kwenye miswada.
Prof. Kabudi na timu yake ya wanasheria wameanza kutoa matunda yao mema kwa taifa kupitia kazi zao kama zilivyobainika kwenye miswada hii.
Kwa miswada hii iliyopelekwa bungeni ili kujadiliwa na kuwa sheria haina maneno mengi lakini yaliyopo yamejaa umuhimu mkubwa kisheria kwa maslahi ya taifa, sina shaka kwa kiwango kikubwa taifa litakuwa limeingia katika ukurasa mpya katika safari ya kulinda maliasili zake ili zinufaishe taifa kwa kizazi hiki na kijacho.
Kama Rais Magufuli alivyosema, ‘’tulichelewa lakini kama taifa tumeamua kufika’’ na kwa miswada hii ninatumaini tutafika.
Yaliyopo katika miswada hii ya sheria ni pamoja na;
>>Bunge kupitia mikataba yote ya maliasili za nchi kuangalia maslahi ya Watanzania na baada ya kubaini masharti hasi katika mikataba hiyo Bunge linaweza kuitaka Serikali kufanya majadiliano upya na upande wa pili wa mkataba ili kuondoa masharti hayo.
>>Kuweka utaratibu wa bunge kufanya mapitio na maridhiano ya mikataba.
>>Kufanya mapitio madaraka ya Waziri na Kamishna wa madini.
>>Kuimarisha mifumo ya uthibiti na uwajibikaji katika sekta ya madini na petrol.
>>Kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato kwenye sekta ya madini na petrol.
Kwa wale wanataka kuisoma hiyo miswada Gonga hapa;
LINK>>Miswada ya marekebisho ya sheria za maliasili
Hizi ni baadhi ya contents zilizoko kwenye miswada.