mkaruka ataja rinu
JF-Expert Member
- Aug 27, 2016
- 3,309
- 2,218
Kumbe Chadema bado wapo, me nilishawasahau aisee!!!!!!!!!!Nimepita mkoani Iringa na sasa niko Mbeya, kiukweli Chadema bado wapo tena bado ni " jeuri" zaidi ya vilevile.
Mtazamo wangu hiki chama kinaweza kufufuka au kuzaliwa upya na safari hii kikiwa na wagumu watupu. CCM lazima itumie njia mbadala kukabiliana nao maana mchungaji Msigwa na Sugu bado wanatamalaki na kung'aa kana kwamba bado ni wabunge.
Trump pamoja na kupigwa chini kwenye uchaguzi kuna wananchi bado wanamlilia.
Maendeleo hayana vyama!