Kwa matokeo haya ya wajumbe wa NEC, kipo kitu nyuma ya Pazia, Mwenyekiti shtuka

Kadoda nguku

JF-Expert Member
Apr 22, 2019
332
475
Uchaguzi umekwisha , na wajumbe wa NEC wamechaguliwa.
Itoshe kusema kanda ya ziwa ndio walio shinda kwa kurudi na wagombea wao wote.

Matokeo Uchaguzi wa Wajumbe wa NEC-CCM Kwa Upande wa Tanzania Bara

👇🏼👇🏼👇🏼👇🏼👇🏼
Mkutano wa kumi wa CCM umefanyika na haya ndio majina ya wajumbe waliochaguliwa kuwa wajumbe wa NEC-CCM kwa Tanzania bara.

Wanawake
1. Dkt Angelina S Mabula Kura 770
2. Dkt Ashatu Kijaji Kura 764
3. Christina Solomon Mndeme Kura 761
4. Hellen Makungu Kura 755
5. Fenela A. Mukangara Kura 747
6. Angellah J. Kairuki Kura 730

Wanaume
1. Mahenda Leonard 845
2. Bashungwa Innocent 720
3. Wasira Steven 680
4. Msome Jackson William 591
5. Kasheku Msukuma 587
6. Kasesela Richard 574
7. Wambura Chacha Mwita 545
8. Bashe Hussein 510
9. Nnauye Nape Mosses 508
10. Gwajima Josephat 497
11. January Makamba 452
12. Mwigulu Nchemba 450
13. Macha 435
14. Msengi Ibrahimu 428

Kimsingi washindi karibu wote wametoka kanda moja huku maeneo mengine wakirudi mikono mitupu na wagombea wao, wakiendelea kulaumiana kwamba wapiga kura wao wamekosa umoja lakini kikubwa nilichokiona ni mshikamano wa wajumbe toka kanda ya ziwa kuamua kuwabeba watu wao, lakini pia kikubwa wasukuma wameamua kushikamana na kuonyesha kwamba wao ni wengi nchi hii na kuamua watu wao waingie katika chombo cha maamuzi. Pamoja na kutumia nguvu ya pesa. Lakini umoja na mshikamano wao umeonyesha dhahiri wakidhamiria kitu wanaweza, Hivi sasa wanapongezana kwamba wamefanikiwa mission yao kwa 100%

Swali la kujiuliza ni nani aliye nyuma ya hii kadhia, Mimi na wewe hakuna anayejua, lakini kuanzia sasa hadi 2025 tutaona kila aina ya rangi.

Mikoa ya kanda ya kusini kwa maana ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Njombe aliyepita ni Nape pekee. Tafsiri yake mikoa hiyo inabaki na wawakilishi wachache mno kwenye chombo hicho chenye mamlaka ya kupiga kura ya kumchagua Rais.

Mikoa ya Mbeya, Katavi, Rukwa, Iringa na Morogoro nadhani wameambulia patupu, wameondoka wakilaumiana.
Matokeo haya yanaashiria nini, mikoa ya kusini ndio ambayo imekuwa ngome kuu ya CCM, wamenyang"anywa rasmi ukuu huo, kwa kuwa hawana wawakilishi wengi. Kanda hiyo iliyoongoza kwa kutoa makada wakuu kama akina Nchimbi na wengineo sasa sio kitu tena.

Tutegemee nini?
Hawa wajumbe wa mkutano mkuu kwa matokeo haya tutegemee kwamba lolote linaweza kutokea 2025, kwa sababu wajumbe walio wengi ni ukanda ambao wamebezwa mno baada ya kifo cha mpendwa wao. Mikoa mingine kura walizonazo ni chache mno,hazitaweza kupingana na walio wengi kama tulivyoona.
Nini kifanyike

Kwa sasa anachoweza kufanya mwenyekiti ni kuhakikisha analichota kundi kubwa toka ukanda wenye wajumbe wengi ili kuvunja makundi, na kuhakikisha anapata uungwaji mkono mkubwa ili kujiweka katika mahali salama.
Hivi sasa maamuzi ya nani awe Rais yanategemea maamuzi ya kanda moja tu, kanda nyingine ni wasindikizaji tu. Maamuzi yanategemea mikoa michache yenye uwingi wa wajumbe.

Hii ni tafakuri fupi, itakayokusaidia kukuonyesha nguvu ya akina msukuma, Gwajima, Mabula, Bashiru ndani ya CCM.

Itoshe tu kusema kanda ya ziwa mmeupiga mwingi
 
Pole pole ile dhambi aliyoikataa Nyerere imeanza kushamiri. Watu wanajadili kuhusu Kanda ya Ziwa, nakujionesha kwamba Kanda ya Ziwa Ina nguvu.

Kesho tutanza kuchsgua Rais kwa Kanda zetu. Naona tunawaiga wakenya kwa Kasi, ambapo Rais hutoka rift valley na Central pekee.
 
Mleta mada hayo ni mawazo Yako tu wala hakuna MTU Yuko nyuma ya pazia. Ninachokijua mimi ni Kanda ya ziwa TU utakuta mchaga ni Mnec au Mwenyekiti wa chama ni Muha au mmakonde. Hakuna ktk nchi ambapo wenyeji wanapenda Wageni kama Kanda ya ziwa labda kidogo kwa mbaaaali Mkoa wa Kagera.

CCM ni chama cha kihistoria Kwa maana kitaendelea kujitanua vizazi hata vizazi. Mfumo wake wa Upatikanaji wa uongozi pamoja na uandaaji wa viongozi wa siku za mbeleni umekifanya kuwa imara zaidi.

Vyama vya upinzani nchini mbali na viongozi Wake kuwa walamba asali pia wamejisahau kabisa Kuweka mfumo wa kulea na kuwaandaa vijana kuwa viongozi baadae. Tunayoyaona ya kanda ya ziwa ni matokeo hayo ya mfumo tu mzuri wa kuandaa vijana
 
Uchaguzi umekwisha , na wajumbe wa NEC wamechaguliwa.
Itoshe kusema kanda ya ziwa ndio walio shinda kwa kurudi na wagombea wao wote...
Halafu ikija issue ya Kenya, mnadai ukabila. Kama hatuna Ukabila Bongo, hii hoja ni ya nini. Mambuzi acheni ujinga.
 
Uchaguzi umekwisha , na wajumbe wa NEC wamechaguliwa.
Itoshe kusema kanda ya ziwa ndio walio shinda kwa kurudi na wagombea wao wote...
Kwa izi kauli za kina Mzee Makamba za kejeli na kufuru kwa Mungu, hawamsaidi Dkt Samia. Wanamjengea chuki maana utake usitake Hayati Magufuli alitufumbua watanzania na tunajua A is A, not A is not A. Wee Leo Msukuma Kasheku wakumzidi kura Mwigulu?
 
Mwenyekiti alisha zungumza jana... pia ni mkakati kwa ajili ya 2025... tume azimia jana kwa pamoja hivyo ni wakati wa kwenda kutekeleza tuliyo ya azimia

Kama ukusikia au kuelewa maazimio, neno la shukran toka kwa wajumbe (wazee), kutoka kwa wajumbe kila mkoa, na mwenyekiti aliye funga zoezi

Basi huta elewa na kubaki na zaania zako kama alivyo eleza jakaya jana...
 
Uchaguzi umekwisha , na wajumbe wa NEC wamechaguliwa.
Itoshe kusema kanda ya ziwa ndio walio shinda kwa kurudi na wagombea wao wote...
Hii nchi tunaenda kupigana vita ya wenyewe Kwa wenyewe soon, na Imani yangu huku kusini tutaitumia vizuri hiyo chansi kwasababu serikali imetupuuza nasema tutazichakaza Kanda zote Kwa kipigo ndoige na hapo ndo mtafahamu nafasi yetu katika taifa hili iko mahali gani.
 
Mtoa mada pia ujikumbushe kilichomtokea lowasa 2015.

Hakuna aliye juu ya Rais aliyopo madarakani Tz.
Huwajui watu wakanda ya ziwa, wajumbe zaidi ya 75% wanatoka ukanda huo, halafu kamati kuu wakate jina la Mtu wao, halafu NEC watoke nje wajumbe zaidi ya 75%, wabaki kina nape peke yao ukumbini , unafikiri kuna kitu kitafanyika ndani humo, huwajui akina Gwajima ,msukuma wanapokuwa na mission town zao.

Mshikamano walio uonyesha kwenye huu uchaguzi, unafikiri wakiamua kuuonyesha 2025 watashindwa, Kwenye system kwenyewe Magufuri aliwajaza vijana kibao sana, kuanzia juu hadi chini
 
Back
Top Bottom