Tukiwaachia tu na wao hawaaminiani, Pemba itakuwa nchi huru pia Unguja nayo, sasa hayo yoote ya nini?Ulaya kulikuwa kuna nchi inaitwa Czechoslovakia. Sehemu moja ilipoona kuwa hairidhiki na hali ilivyo ikafanywa referendum kuhusu ushirika huo. Sharti likikuwa nchi itabaki ilivyo kama tu pande zote zitaridhia. Pande moja ikakataa, wakaheshimu maamuzi, wakapeana talaka. Matokeo ni nchi ya Czech na Slovakia. Mpaka sasa wanaishi kwa amani.
Huko huko kulikuwa na Yugoslavia. Slovenia na Croatia wakalalamika kuwa Serbia inawanyima haki zao na inajifanya yenyewe ndio Yugoslavia. Serbia wakakataa kuwasikiliza. Slovenia na Croatia zikajitangaza kuwa ni nchi huru. Serbia wakashambulia Croatia kupinga uamuzi huo. Matokeo ni vita ambamo raia wengi walipoteza maisha na unyama mkubwa ulifanyika. Hatimaye Yugoslavia ikasambaratika na sasa kuna Slovenia, Croatia, Serbia, Bosnia na Herzegovina, Macedonia ambazo kila moja ni nchi huru.
Uingereza mpaka leo kuna wa Scot wanaotaka waondokane na uUK . Spain hivyo hivyo.
Hauwezi kulazimisha umoja. Mmoja akichoka ni heri kutengana kwa amani kuliko kulazimishana.
Amandla...