Travis Walker
JF-Expert Member
- Apr 10, 2017
- 323
- 332
Kuna mtu alinifunza kuipenda haki. Kwa kuyapitia maumivu na mazito nilijifunza kuwa na huruma. Kwa mara ya kwanza nikamuamini mwanamke. Ama kweli mapenzi ni matamu mno, nilijikuta nazama zaidi kwenye penzi zito. Nikampa moyo wangu nikampenda kupita maelezo. Kabla ya hapo sikutaka kabisa kumuamini mwanamke yoyote ila akanibadilisha mtazamo wangu.
Nikaamini yupo kwa ajili yangu nikachagua kumfanya wa maisha. Niliamini ananipenda kweli ila yote yalikuwa ni maigizo. Alikuja kuharibu karibu na mwisho. Ilikuwa ni muda mchache tufunge pingu ya maisha pamoja.
Niliumia zaidi ya kuteseka mpaka nikajiuliza yawaje mimi mwanaume nimenasa kwenye mtego wa kitoto. Alifanya kuigiza kila kitu, nikajisahau uongo nikauwona ni ukweli mtupu.
Nikaamini yupo kwa ajili yangu nikachagua kumfanya wa maisha. Niliamini ananipenda kweli ila yote yalikuwa ni maigizo. Alikuja kuharibu karibu na mwisho. Ilikuwa ni muda mchache tufunge pingu ya maisha pamoja.
Niliumia zaidi ya kuteseka mpaka nikajiuliza yawaje mimi mwanaume nimenasa kwenye mtego wa kitoto. Alifanya kuigiza kila kitu, nikajisahau uongo nikauwona ni ukweli mtupu.