MJINI CHAI
JF-Expert Member
- Dec 12, 2010
- 2,196
- 1,218
Heshima Wakuu....kwa mara ya kwanza tangu nizaliwe nimesikia maneno ya Faraja na ya kizalendo kutoka kwa kiongozi wa ngazi ya juu wa Wilaya, Huyo si mwingine ni DC wa wilaya ya KISARAWE mama KARAMAGE bila kujali kuwa leo 28.05.2011 ni siku ya Jumamosi ambapo alitakiwa apumzike lakini aliamua kufanya ziara katika kijiji cha KAZIMZUMBWI majira ya saa 14:26 akaaza mkutano na wanakijiji na kumtaka mwenyekiti wa kijiji kusoma ripoti ya mapato na matumizi ya kijiji ili wanakijiji wafahamu, vilevile alimtaka mwenyekiti kutoa vipaumbele vya kijiji. cha kushangaza uongozi wa kijiji walimweleza DC kuwa wataiandaa ripoti.......
Ndipo mhe DC aliwaeleza wananchi ya kuwa Wilaya ya KISARAWE ni kongwe tangu enzi za mkoloni na ina takribani zaidi ya miaka 100 lakini ipo nyuma kimaendeleo, yeye akiwa kama DC wa 13 baada ya uhuru hatakubali wilaya hiyo ambayo ilianzishwa wakati mmoja na jiji la NAIROBI kenya iwe nyuma kimaendeleo..........
Aliwataka wanakijiji kuwa na moyo wa kupenda maendeleo.....kwani yeye kama DC WAMEKAMILISHA MCHAKATO wa kuishanya wilya kuwa Mji Mdogo sambamba na kupima viwanja vya makazi na viwanda na tayari kiwanda cha cement kinaendelea kujengwa nakuwataka wanakijiji kujitokeza kuomba kazi mara kitakapoanza kufanya kazi......
Aliwataka uongozi wa kijiji kumpa taarifa za wanafunzi ambao kwa njia moja au nyingine wameshindwa kwenda shule ili kuona anawasaidia vipi na aliwapa rai wazazi ya kuwa wasiwaachie wanafunzi kuendesha BODABODA wakaacha kwenda shule...........
Kwa vile mji unapanuka aliwaasa watendaji wa wilaya ya kuwa kuna maeneo ambayo yameainishwa kwa kuyaendeleza hivyo ni vizuri wanakijiji wakashirikishwa ili kuondoa migogoro ya aridhi na hatimae wanakijiji watakao chukuliwa maeneo yao watafidiwa.......
Kwa maoni yangu na baadhi ya wanakijijitumemkubali huyu mama na laiti kama ****** angekuwa na timu kama hii basi miji yetu ingekuwa mbali..licha ya mkutano kwisha saa 16:30 bado DC alichukua kama nusu saa tena kubadilishana mawazo na wanakijiji......it was very interesting........... Je wakuu huko kwenu MaDC wanabadilishana mawazo na wanakijiji?......
Ndipo mhe DC aliwaeleza wananchi ya kuwa Wilaya ya KISARAWE ni kongwe tangu enzi za mkoloni na ina takribani zaidi ya miaka 100 lakini ipo nyuma kimaendeleo, yeye akiwa kama DC wa 13 baada ya uhuru hatakubali wilaya hiyo ambayo ilianzishwa wakati mmoja na jiji la NAIROBI kenya iwe nyuma kimaendeleo..........
Aliwataka wanakijiji kuwa na moyo wa kupenda maendeleo.....kwani yeye kama DC WAMEKAMILISHA MCHAKATO wa kuishanya wilya kuwa Mji Mdogo sambamba na kupima viwanja vya makazi na viwanda na tayari kiwanda cha cement kinaendelea kujengwa nakuwataka wanakijiji kujitokeza kuomba kazi mara kitakapoanza kufanya kazi......
Aliwataka uongozi wa kijiji kumpa taarifa za wanafunzi ambao kwa njia moja au nyingine wameshindwa kwenda shule ili kuona anawasaidia vipi na aliwapa rai wazazi ya kuwa wasiwaachie wanafunzi kuendesha BODABODA wakaacha kwenda shule...........
Kwa vile mji unapanuka aliwaasa watendaji wa wilaya ya kuwa kuna maeneo ambayo yameainishwa kwa kuyaendeleza hivyo ni vizuri wanakijiji wakashirikishwa ili kuondoa migogoro ya aridhi na hatimae wanakijiji watakao chukuliwa maeneo yao watafidiwa.......
Kwa maoni yangu na baadhi ya wanakijijitumemkubali huyu mama na laiti kama ****** angekuwa na timu kama hii basi miji yetu ingekuwa mbali..licha ya mkutano kwisha saa 16:30 bado DC alichukua kama nusu saa tena kubadilishana mawazo na wanakijiji......it was very interesting........... Je wakuu huko kwenu MaDC wanabadilishana mawazo na wanakijiji?......