Kwa mara ya kwanza watazania wala ugali sikukuu ya iddi

mdukuzi

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
15,978
35,627
Chakula ni sehemu ya utamaduni,ndio maana ukienda china unaweza kukuta wanakula konokono,nyoka kenge mamba nk ndio utamaduni wao
tangu nazaliwa miaka kadhaa baada ya yesu kuzaliwa huku kwetu uswahilini Tandika,Mbagala,Manzese ,Mwananyamala Tandale.siku za sikukuu za kidini iwe iddi,pasaka ,au krismasi lazima pilau lipikwe .ndio utamaduni wetu hauzuiwi kula pilau siku ambazo sio za sikukuu ila sikukuu kukosa pilau ni nje ya utamaduni wetu
Kwa mara ya kwanza kuna jirani zangu tena waislamu ambapo leo ndio sikukuu yao ila leo wamekula ugali kwa mara ya kwanza ,watoto wakambana baba akatoa sababu kuwa iddi imekuja ghafla mno walitarajia iwe kesho so watakula pilau keshosie watu wazima tukawa tumeshaelewa anamaanisha nini ,masikini watoto wamekula ugali na kesho huenda wakala tena ugali, kusema ukweli maisha yamekuwa magumu wafanya biashara wa kariakoo nao wanashangaa mauzo ya mwaka huu kipindi cha sikukuu yamevuja rekodi kwa kuwa chini
 
e1b9d004bdea4b6b5764fd8da44f8652.jpg
 
Mwanaume wa dar ktk ubora wako. Yaani umbea mtupu. jirani yako kula ugali, wewe inakuhusu nini? Familia moja imekula ugali siku ya Idd lakini hapa unasema watanzania wamekula ugali siku ya Idd. hiyo fsmilis moja ndio inawakilisha watanzania wote?
 
Unaweza ukala Ugali na ukaifurahia sikukuu yako ila kidogo kwa watoto lazima wajisikie vibaya maana mtoto anaitafsiri sikukuu kwa Kula Wali/Pilau na mapochopocho mengine hata kama huwa anayala kila siku pamoja na kuvaa nguo mpya.
 
Mwanaume wa dar ktk ubora wako. Yaani umbea mtupu. jirani yako kula ugali, wewe inakuhusu nini? Familia moja imekula ugali siku ya Idd lakini hapa unasema watanzania wamekula ugali siku ya Idd. hiyo fsmilis moja ndio inawakilisha watanzania wote?
nyie wamikoani hii haiwahusu kwa ufupi hali ya maisha ngumu
 
Mwanaume wa dar ktk ubora wako. Yaani umbea mtupu. jirani yako kula ugali, wewe inakuhusu nini? Familia moja imekula ugali siku ya Idd lakini hapa unasema watanzania wamekula ugali siku ya Idd. hiyo fsmilis moja ndio inawakilisha watanzania wote?


Nilichomuelewa mtoa mada kwamba si kawaida na anataka kuijumuisha hali hii na Ugumu wa Kifedha kwa hii "Tanzania ya Viwanda na kuwa ni moja ya donors country"..
 
Nilichomuelewa mtoa mada kwamba si kawaida na anataka kuijumuisha hali hii na Ugumu wa Kifedha kwa hii "Tanzania ya Viwanda na kuwa ni moja ya donors country"..
kula kulala hawawezi kuelewa fasihi mpaka uwatafunie kila kitu,hali ni mbaya sikukuu utadhani msiba
 
Haya yote ni maisha, uki force sana utafanywa vibaya, iwe kifedha, kimwili na hata kiroho.

Kubali hali tafuta namna ya kutoka, chakula ladha yake inaishia kwenye ulimi
 
Hilo si jambo geni labda wewe tu kwa ujinga wako ndio unaona jambo geni
 
Huyo sio mzazi bora hafai kuwa tegemeo, inamaana sikukuu ingekuwa kesho, ndiyo ndiyo leo angeandaa hela ya mchele na hela ya viongo vya pilau, ninavyojua mimi ramadhani huchukua siku 30, 29 hivi na mwisho wake huja sikukuu, maandalizi ya sikuu ni lazma uanze nayo mapema. Wazizi wenzangu tujiandae mapema, inamaana huyo angepata dharula majuzi akasafiri mkoa, familia iingelala njaa kabisa, ndio maana watu huchukuliwa wake zao kwa uzembe. Kwa wenye watoto ambao huvarishwa nguo mpya kila sikukuu, baada ya sikukuu hii, anza maandalizi ya kununua nguo moja moja hivi sasa ili kukwepa kutumia hela nyingi kwa wakati mmoja kwa ajili ya sikukuu, hali inayopelekea mambo mengine huushindikana.
 
Tulizoea kuletewa chakula chekwa chekwaa na majirani kama zawadi ya Idd, leo loooooo!!!!!, majanga. Hakuna kitu , hali ngumu! Kweli Magu amefunga mirija na njia zote!
 
Mtaani kwetu kumenuna balaa, utafikir watu wamehama, lingine sikukuu zote nyama dukani ikifika mchana hukuti, lakini Leo naona maduka ya nyama yote hadi midaa hii bado Yana nyama
 
Back
Top Bottom