matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 6,542
- 15,206
Jamaa kauliza
'' Kanisa la shetani ninawezaje kujiunga na Illuminati? ''. '' nataka kuwa tajiri'''.
JIBU LA KANISA LA SHETANI
'' Illuminati inamaanisha kuwa na akili au mwangaza, Hivyo soma vitabu, Jielimishe hivyo utakuwa Illuminati, kama bonasi kujielimisha kutakufanya kuwa na hatua nzuri ya kupata kazi ambayo inaweza kukufanya kuwa tajiri na kupata bahati mahiahani.''
(Nimetafsiri kienyeji kidogo)
Hivyo kama unataka kuwa illuminati au freemason ili uwe tajiri basi ushauri huu wa kanisa la shetani unafaa zaidi ...
Kuwa somasoma
Jiongezee elimu mbalimbali
Tafuta fursa komaaa
Basi tayari wewe ushakuwa illuminati.
Kimsingi hakuna cha vyama vya siri vinavyoitwa illuminati au freemason ni kutishana tu, kikubwa bukua jitume maishani basi ushakuwa illuminati hii sio kwa mujibu wangu bali kwa mujibu wa kanisa la shetani mwenyewe.
Kwa mara ya kwanza Shetani katoa ushauri wa maana