Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 80,836
- 93,614
Mkuu hiyo ipo tangu kitambo sn, watendaji wanatakiwa kusimamia tatizo linakuja kwenye urasimu wa utaoaji vibali vya ujenzi, pia gharama za michoro kwa mtu ambaye anajenga kwa kuunga unga chumba kimoja au viwili hawezi kwenda kuomba kibali + ramani zaidi ya laki 1 ambayo ataitumia kununua materialAmani iwe nanyi wadau!
Leo nimeona taarifa Azam Tv, waziri wa Ardhi akiongelea suala la watendaji wa kata/ serikali za mitaa kupewa mamlaka ya kusimamia ardhi/ makazi.
Suala hili wana JF humu tuliwai kutoa ushauri kwa serikali hii Kama hatua wanayopaswa kuchukua katika kukabiliana na tatizo la makazi holela na ujenzi mbovu unaoharibu mipango miji.
Uzi mmoja wapo ni huu👇
Ni nini kimeifanya CCM kushindwa kabisa kufanya lolote juu ya Mipango Miji?
Solution yake inaanzia waizarani kulete mpango kazi ambao mpaka mwenyekiti, mtendaji na mjumbe wa kaya anafahamishwa jinsi viwanja au maneno yanavyotakiwa kuendelezwa. Ilikuwa rahisi tuu mjumbe wa shina amuonye mangi fulani anayejenga mpaka nje ya mawe pale mabibo opposite NIT. Au aple sinza...www.jamiiforums.com
Kwa taarifa hii niliyoiona Leo, napenda kwa Mara ya kwanza kumpongeza ndugu William Lukuvi kwa kuchukua ushauri huu murua ambao kwa hakika ninaamini tukiusimamia vizuri ndo itakuwa dawa kuu na ya kudumu wa makazi holela na ujenzi mbovu usiozingatia mipango miji hapa Tanzania.
Napenda kusisitiza kwa Lukuvi, hili alilolianzisha wala asirudi nyuma maana ndo Litaondoa ujenzi holela na makazi holela hapa Tanzania.
====
WATENDAJI WA MITAA KUPEWA RUNGU KUSIMAMIA ARDHI:
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri nchini kuwapatia mamlaka maafisa watendaji wa mtaa ili wawe na uwezo wa kusimamia masuala yote ya uendelezaji ardhi na kuwachukulia hatua watu wanaokiuka taratibu za ujenzi kwenye mitaa yao.