Kwa mantiki ya kisheria DC Kihongosi amekosea, lakini kwa mantiki ya kiuwajibikaji yuko sahihi

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Jul 17, 2019
322
645
KWA MANTIKI YA KISHERIA DC KIHONGOSI AMEKOSEA, LAKINI KWA MANTIKI YA WAJIBIKAJI YUKO SAHIHI

Na Elius Ndabila
0768239284


Jana na leo kuna mjadala mkubwa juu ya uhalali wa Mh DC wa Arusha Mh Kihongosi kuwatandika fimbo watu wanaotajwa kuwa ni wafanyabishara kwa kosa la kuiba viti vya shule.

Staki kuingia kwenye hoja ya uwizi, hii ni kwa kuwa tukianza kujadili hili tutaingia kwenye mambo mengine ya kisheria ambayo si wajibu wangu leo kuyazungumzia. Mimi nataka tuzungumze facts in issue iliyopelekea wao kuchapwa. Tujikite kuangalia makosa na usahihi wa hizi fimbo kwa mkutadha wa kinadharia ili kujenga Taifa.

Unapokuwa kiongozi unakuwa na malengo yako, hasa unapofanya kazi. Unatamani kama ni shamba ulime kwa wiki moja. Unapokuta mtu mliyekubaliana naye kuwa alime kwa wiki moja kuna siku hajaenda shambani na yupo kilabuni bila shaka utavunja mkataba naye kwa kuwa utakwazwa na kitendo cha kunywa pombe badala ya kwenda Shambani. Ijapo pengine ungemsikiliza huenda angekuwa na hoja.

Unapokuja kwenye issue ya Kihongosi kuwachapa fimbo, yule ni DC na amepewa kazi pia ya kuhakikisha shule zinakuwa na madawati. Unapotengeneza Dawati then unasikia kuna watu wameziiba na kuharibu lazima kama DC utachukua hatua kali kabla ya mamlaka zingine kwa kuwa ni ready heanded. Umewachapa viboko kwa kuwa yeye ni kiongozi na halali usingizi kwa sababu ya kazi hizi. Lakini hata Mh Rais alisema bora kufanya kosa kwenye kuwajibika, kuliko kuto fanya maamuzi. Kihongosi amefanya uamuzi yanayoonyesha alikerwa na jambo hili.

Kuchapa viboko watuhumiwa bila kuwafikisha kwenye vyombo vyenye maamlaka hiyo ni kosa, lakini kufanya kosa ambalo lina maslahi mapana ya Taifa ni jambo la kupongezwa na linaonyesha namna serikali ilivyo serious na watovu wa nidhamu.

Sasa tukubaliane kuwa kuiba ni kosa kwa mjibu wa sheria ya nchi lakini hata kuchapa bila kuzingatia sheria ni kosa. Lakini kuchapa fimbo kwa kupeleka ujumbe kwa wezi wengine ni jambo la baraka. Kwa mstari huu ninaungana na Kihongosi kwa watu wanaosadikiwa ni wezi. Ninaungana na Kihongosi kwa mkutadha wa Uwajibikaji na si kwa mkutadha wa Kisheria.
 
KWA MANTIKI YA KISHERIA DC KIHONGOSI AMEKOSEA, LAKINI KWA MANTIKI YA WAJIBIKAJI YUKO SAHIHI.

Na Elius Ndabila
0768239284

Jana na leo kuna mjadala mkubwa juu ya uhalali wa Mh DC wa Arusha Mh Kihongosi kuwatandika fimbo watu wanaotajwa kuwa ni wafanyabishara kwa kosa la kuiba viti vya shule...
Two wrongs don't make up a right. Kama kweli wameiba wapelekwe mahakamani wafunguliwe kesi uletwe ushahidi na wahukumiwe, tena itakuwa safi wapewe adhabu kali viboko havitoshi na walipe zaidi ya walichoiba.

Kuchapana viboko siyo poa, ikiendelea utakuja shangaa watu wanaanza pigwa vibao hovyo hovyo, watoto wamefail kutokana na ukosefu nyenzo za ufundishaji unashangaa DC anawatandika vibao walimu.

halafu mkuu naomba unijuze, hivi siku hizi watu kuweka namba za simu kwenye post zao wanaweka ili waigiwe simu au watumiwe msg na wasomaji?
 
Samahani kati ya washangiliaji wasichojua wanashangilia nini kumbe na wewe upo.

Tuanzie hapa aliyechapwa kwa kuhisiwa tu angekuwa baba yako, mkeo au mama yako haya ungeyaandika?

Pili kuwajibika siyo kuchukuwa sheria mkononi as such ni ujinga usio na kifani kwa mtu kama DC.

Ni aibu kuona serikali kupitia DC bado inatekeleza copral purnishment bila kufuata sheria ambazo wao ni wasimamizi wake.

Tusifu tusifu sana ila jamani tusisifu ujinga kama huu eti kupiga watu wazima hadharani tena kwa majivino makubwa ndiyo uwajibikaji. I am saying no non and with big NOOOOOOOOOOO!!!!!!!!!!!
 
A good philosopher does not contradict himself.Kwani Sheria za ki-uwajibikaji si ndizo zilezile zitokanazo na Sheria za nchi? Huwezi ukawajibika kinyume na Sheria za nchi.Nasikitika sana,Kama mitandao ya kijamii imejaa watu Kama hawa.

Sheria ndizo hutoa mipaka ya ki-uwajibikaji, kuna vitu huruhusiwi kuvifanya, hata kama wewe ni mkuu wa nchi. Labda niulize, umemsikia Mh. Rais Magufuli amechapa mtu viboko, pamoja na kwamba yuko strict sana? Ni watu wajinga tu ndio wanaochapa watu viboko, mtu smart hawezi fanya hivyo.
 
Yaani watu mnaotetea ujinga kama huu huwa nashindwa niwaweke kundi gani!
 
Nchi yetu imeshaharamisha, kisheria, corporal punishment.

DC kaleta mashtaka, kaprove na kahukumu.

Sheria pia hairuhusu mtu kuhukumiwa mara mbili kwa kosa lile lile moja. Wakipelekwa mahakamani na wakisema walishahukumiwa na DC itakuaje?

Ikisemwa haikua sahihi huyu DC anatakiwa afanywe nini?
 
Mfuatilie vizuri huyu DC, huko nyumbani hana katabia ka kupiga mke na watoto, uende akawa mtu wa namna hiyo, basi juwa ni mtu dhaifu sana hawezi kujiongoza mwenyewe!
 
Ni Mataga tu, ndiyo watakubari kuchakazwa viboko, tena na mtoto mdogo,ni Kama wale Mataga wa wanyama pori, walivyokubali kuchapwa viboko na Kigwa.
Na hata wakipelekwa mahakamani watashinda tu kesi maana tayari wamekwisha pewa adhabu ya fimbo... mahakamani hawawezi kuadhibiwa mara mbili sijui kama siku hizi, hizi adhabu za fimbo ndio mtindo wao maana tangu speaker ndugua alipo mchapa fimbo mpinzani wake hadi kupoteza fahamu, ndio umekuwa mtindo wao hadi huko Mbeya itafikia mahali watu watafanya makosa na watajua kwamba adhabu ni fimbo tu na yanaisha.

Kuwachapa watu fimbo ni kuingilia mhimiri mwingine wa nchi. Tangu lini adhabu ikawa ni kazi ya serikali? adhabu hutolewa na mahakama tu na igefaa sana huyo DC ageuziwe kibao maana ame-exceed scope of his authority....yabidi afutwe kazoi haraka sana kwa kuinajisi mahakama
 
Kuna wakati sisi Watanzania tukikamata mwizi wa kuku, simu au saa tunamchoma moto kwa jina la wananchi wenye hasira.

Watoto wa shule wamekwiba viti ambavyo ni mali ya umma kosa la kwanza;

Vijana wa kitaa wananunua kwa sh. 500 mali ya wizi. Mali ya thamani ya laki moja inapouzwa kirahisi rahisi na jamii akachukulia poa; hapo kuna nakisi kubwa sana ya maadili/uwajibikaji wa umma kulinda mali ambayo imenuliwa kwa kodi zetu.
Kosa la pili;

Taratibu mwizi ilitakiwa achukuliwe na kupelekwa mahakamani ili "ikithibitika pasi chembe ya mashaka" basi wahukumiwe kwa mujibu wa sheria.

So far, kwa ni aibu kama taifa hatujaonekana kukerwa na kukemea wizi tumebaki ku-focus kwenye adhabu ya viboko ambayo DC kaitoa kwa "watuhumiwa"

Nadhani umma iko haja ukawa na mechanism za kudhibiti mali za wizi kuingia kitaa na kugeuzwa then tukazinunua tena.

Juzijuzi hapa watu walikwiba vyuma vya SGR na OCD mmoja akihusika kwenye saga hili.

Ili tupige hatua, mambo ya watu kukwiba tubachukulia poa sio sawa.

Hata mchonga alikuwa anachapa watuhumiwa/washtakiwa 6 mtu akiingia lupango na 6 mtu akamwonyeshe mkewe. Ila alihifadhi utu wa mtu kwenye kutekeleza adhabu.
 
Hakuna pahala uwajibikaji unahalalishwa na uchapaji mtu viboko, hii hoja yako ya pili nayo uliyojaribu kumtetea huyo DC ni feki.

Hao waliotandikwa viboko wakamshtaki huyo DC mahakamani, either afungwe au awalipe fidia.
 
Ni siku kadhaa sasa zimepita toka mkuu wa wilaya ya Arusha,acharaze watu viboko.Wakati mwingine watanzania wanajiuliza; mbona mkuu wa nchi yeye hatoi adhabu za kikatili kama za hawa wa chini yake? Ikumbukwe hili haliharibu tu utawala wa Sheria, Bali linabadilisha kabisa sura ya utamaduni wetu.

Watoto wanaokua leo wataamini kabisa kuwa Mtu yeyote akikosea adhabu yake mahususi ni viboko.Sehemu pekee ambapo mkosaji huadhibiwa bila kiathiri matakwa mengine ni mahakamani. Hata wanafunzi na wafungwa huadhibiwa kwa utaratibu maalum,sembuse na watu wazima.

Kwa mfano:

Kulingana na Sheria zetu za elimu,mwalimu kumwadhibu mwanafunzi shuleni, kunachukua mlolongo mrefu mno,ili kuhakikisha kwamba anaadhibiwa kulingana na utaratibu, Kumbe Kuna viongozi hapa nchini,wao wanamuadhibu mtu (Tena mtu mzima) popote, vyovyote kwa kosa lolote.Hapana,vyeo visitumike kutufanya tuumizane. Tunaomba sana mheshimiwa rais, viongozi kama hawa wawajibishwe.

Tunakumbuka mkuu wa wilaya ya Bukoba enzi zile(Albert Mnari) alipowachapa walimu kwa utoro,Rais mstaafu JK alimuachisha kazi. Tunaomba sana mheshimiwa rais, chukua hatua dhidi ya hivi vitendo, vinavyoumiza watu, vinavyotumiwa na baadhi ya viongozi uliowateua kutafuta SIFA ZA ZIADA.

Nawasilisha

Ni mimi mtanzania, PILIPILI--MBUZI.
 
Ni siku kadhaa sasa zimepita toka mkuu wa wilaya ya Arusha,acharaze watu viboko.Wakati mwingine watanzania wanajiuliza;mbona mkuu wa nchi yeye hatoi adhabu za kikatili kama za hawa wa chini yake?Ikumbukwe hili haliharibu tu utawala wa Sheria, Bali linabadilisha kabisa sura ya utamaduni wetu...
Aisee wewe jamaa hujielewi unaita viboko kuwa adhabu ya kikatili?
 
Ni siku kadhaa sasa zimepita toka mkuu wa wilaya ya Arusha,acharaze watu viboko.Wakati mwingine watanzania wanajiuliza;mbona mkuu wa nchi yeye hatoi adhabu za kikatili kama za hawa wa chini yake?Ikumbukwe hili haliharibu tu utawala wa Sheria, Bali linabadilisha kabisa sura ya utamaduni wetu...
🙄
 
Back
Top Bottom