Hivi karibuni kumekuwa na mjadala kwenye jukwaa hili kuhoji uhalali wa Mke wa Rais kutumia rasilimali za walipa kodi kumfanya kampeni za kumrejesha mumewe madarakani. Ninatoa rai kwa wanajukwaa kujadili kama ni halali kwa mgombea tena ambaye hana nafasi yoyote kwenye serikali hivi sasa kupewa ulinzi wa serikali na kupambwa na wateuliwa wa Mh. Rais kufanya ukaguzi wa miradi inayotekelezwa kwa fedha za walipa kodi. Picha hii inajieleza yenyewe