Kwa mambo kama haya umaskini lazima utawale

Orketeemi

JF-Expert Member
Feb 12, 2013
4,313
10,017
Siku hizi kila mtu wa chama tawala anajipa usemaji wa serikali, wanakurupuka wakina jery Muro kujibu tuhuma zozote zinazoelekezwa serikalini, lakini cha ajabu hakuna wanachojibu badala yake wanapiga porojo tu.

Huu ni ujuha wa kiwango cha ajabu kabisa,, nchi inaharibika kizembe kabisa hii kwa kuendekeza "kujibebisha" kwa mheshimiwa Rais ili anagalau awakumbuke katika teuzi zake zisizokwisha.

Naomba kusisitiza kwamba kama mheshimiwa Rais akirudi nyuma kidogo tu lazima atatambua kwamba anawahitaji zaidi wakosoaji wa utawala na sera zake kiujumla kuliko anavyowahitaji wakina Jerry Muro and the likes.

Tunapopinga baadhi ya mambo ieleweke kuna haja ya ufafanuzi kutolewa maana mambo yote yanayofanywa na serikali raia kwa ujumla wetu ndio tunaogharamia.

Mfano, binafsi nimekuwa siafiki vitendo vya utawala huu kuwekeza sana kwenye usafiri wa anga kiasi cha kupunguza nguvu uwekezaji katika masuala yanayogusa maisha ya kila siku ya watanzania wengi mfano kilimo, afya n.k

Hatusemi serikali isinunue ndege wala isinunue treni za kisasa hapana bali tunasema ununuzi wa vitu hivyo usitetereshe uwekezaji katika sekta muhim zaidi kwa mtanzania kama kilimo na afya. Tunaangalia Ethiopia na kujifunza kwamba ndege na treni za umeme si kila kitu katika maendeleo hasa ya wananchi. Au ninyi wenzetu mnafanya mambo bila kuwa na key study?

Lakini pia tunakerwa na tabia ya kutokuwa na taratibu za kisheria na kikanuni katika manunuzi na matumizi ya fedha za serikali. Maadam taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za umma tunazo kwenye makabrasha basi ni afya zaidi sheria hizo zikazingatiwa badala ya kuendelea kutumia matamko na utashi wa mtu mmoja. hii itapelekea nchi kuwa na dira ya kueleweka.

Mwisho natoa rai ya hiari kwamba hakuna shortcut kwenye maendeleo ya kweli na kama ndege na treni za kisasa hata Ethiopia wapo vizuri lakin maisha ya raia wa Ethiopia ni magum kuliko ya Mtanzania hivyo serikali isifanye mchezo na uwekezaji katika kilimo.
 
Anataka atoke awe kama Mkapa kujuta kuwa alikosea ubinafsishaji wakati ameshatuingiza cha kike kwenye mikataba mibovu!
Siku hizi kila mtu wa chama tawala anajipa usemaji wa serikali, wanakurupuka wakina jery Muro kujibu tuhuma zozote zinazoelekezwa serikalini, lakini cha ajabu hakuna wanachojibu badala yake wanapiga porojo tu.

Huu ni ujuha wa kiwango cha ajabu kabisa,, nchi inaharibika kizembe kabisa hii kwa kuendekeza "kujibebisha" kwa mheshimiwa Rais ili anagalau awakumbuke katika teuzi zake zisizokwisha.

Naomba kusisitiza kwamba kama mheshimiwa Rais akirudi nyuma kidogo tu lazima atatambua kwamba anawahitaji zaidi wakosoaji wa utawala na sera zake kiujumla kuliko anavyowahitaji wakina Jerry Muro and the likes.

Tunapopinga baadhi ya mambo ieleweke kuna haja ya ufafanuzi kutolewa maana mambo yote yanayofanywa na serikali raia kwa ujumla wetu ndio tunaogharamia.

Mfano, binafsi nimekuwa siafiki vitendo vya utawala huu kuwekeza sana kwenye usafiri wa anga kiasi cha kupunguza nguvu uwekezaji katika masuala yanayogusa maisha ya kila siku ya watanzania wengi mfano kilimo, afya n.k

Hatusemi serikali isinunue ndege wala isinunue treni za kisasa hapana bali tunasema ununuzi wa vitu hivyo usitetereshe uwekezaji katika sekta muhim zaidi kwa mtanzania kama kilimo na afya. Tunaangalia Ethiopia na kujifunza kwamba ndege na treni za umeme si kila kitu katika maendeleo hasa ya wananchi. Au ninyi wenzetu mnafanya mambo bila kuwa na key study?

Lakini pia tunakerwa na tabia ya kutokuwa na taratibu za kisheria na kikanuni katika manunuzi na matumizi ya fedha za serikali. Maadam taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za umma tunazo kwenye makabrasha basi ni afya zaidi sheria hizo zikazingatiwa badala ya kuendelea kutumia matamko na utashi wa mtu mmoja. hii itapelekea nchi kuwa na dira ya kueleweka.

Mwisho natoa rai ya hiari kwamba hakuna shortcut kwenye maendeleo ya kweli na kama ndege na treni za kisasa hata Ethiopia wapo vizuri lakin maisha ya raia wa Ethiopia ni magum kuliko ya Mtanzania hivyo serikali isifanye mchezo na uwekezaji katika kilimo.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa hapa tulipo hakuna ajuaye tunaelekea isipokuwa kiongozi wetu mkuu. Kila siku mipango ya mabilioni ya shilingi inaasisiwa, lakini vyanzo vya mapato ya mipango hiyo hatuambiwi. Mpango wa bajeti unachomekewa matumizi katika ya utekelezaji. Nini maana ya mipango na bajeti kama haifuatwi?
 
Back
Top Bottom