Uchaguzi 2020 Kwa mambo haya 10, mimi kama Mtumishi wa Umma (mwalimu), John Pombe Magufuli sikupi kura yangu asilani

Siyo mwalimu huyo dalali tu, annual increment kila mwaka imekuwa ikiingia. Madaraja walimu tunaostahili tumepandishwa wale waliostahili kupandishwa halafu hawakupandishwa pasipo sababu walipolalamika maafisa utumishi waliwajibishwa.

Acha kudandia taaluma za watu mimi ni mwalimu niko pamoja na Magufuli.Jikite kwenye siasa zako siyo kuwasemea waalimu.
You are crazy for accepting tsh 7800 from lumumba
 
Nikuwekee check number yangu ya nini kama huamini endelea kuamini falsafa za kinyumbu kwamba ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa ndege, ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahati havina manufaa kwa watu.
Wewe endelea tu kutumikishwa na hao walio kuweka hapo Lumumba. Siku akili yako ikikukaa vizuri utanielewa tu nilichomaanisha. Yaani Uvccm tu eti unajiita mtumishi wa umma!
 
Mwalimu Mwenzangu wewe nimuongo sana tumeongezewa mshahara mwaka huu
Wewe umedanganyika kirahisi sana, haujaongezewa mshahara, isipokuwa umepunguziwa Kodi kidogo,(basic salary yako ipo vile vile) na madhara ya hiyo kitu ni kwamba, michango yako ya mifuko ya hifadhi ya jamii haijaongezeka hata mia moja, na kuongeza kodi ni swala la sekunde tu, lakini angeongeza basic salary kupunguza ni ngumu!

Mchagueni tena muone kundi la watumishi masikini litakavyoongezeka kwa kasi...
 
*HAWA NDO CHADEMA WANAOTAKA KUCHUKUA NCHI*

Ni hivi, tangu wameingia madarakani, Chadema wamekuwa wakipokea ruzuku ya Shilingi Milioni 336,000,000/= kwa mwezi. Kwa mwaka (336,000,000/= x 12) = 4,032,000,000/=. Kwa miaka mikano (2015-2020) Chadema wamekusanya Jumla ya Shilingi *20,160,000,000/= (Bilioni Ishirini na Milioni Mia Moja na Sitini).*

Chadema walikuwa na jumla ya wabunge 70, kati ya hawa 34 wa kuchaguliwa, na 36 wa Viti Maalum. Kila mbunge wa kuchaguliwa alikuwa anachangishwa Shilingi Milioni Moja 520,000/= kwa mwezi na kila mbunge wa Viti Maalum alikuwa anachangishwa Shilingi Laki Tano (1,500,000/=) kwa mwezi.

Hivyo, idadi ya michango ya wabunge wa kuchaguliwa kwa mwezi ilikuwa (520,000/= x 34) = 17,680,000/=; na idadi ya michango ya wabunge wa Viti Maalum kwa mwezi ilikuwa (1,500,000/= x 36) = 54,000,000/=. Kwa ujumla wake, Chadema walikuwa wanakusanya kiasi cha shilingi 71,680,000/= kwa mwezi kutokana na michango ya wabunge. Kwa mwaka (71,680,000/= x 12 = 860,160,000/=. Kwa miaka mitano (2015-2020) Chadema wamekusanya Jumla ya *Shilingi 4,300,800,000/= (Bilioni Nne Mia Tatu Milioni na Laki Nane)*

Twende sawa hapa

Ruzuku 20,160,000,000/=
Michango ya wabunge 4, 300,800,000/=

Jumla 24,460,800,000/= *(Bilioni Ishirini na Nne Milioni Mia Nne na Sitini na Laki Nane)*

Licha yah hii;
· Chadema wanakusanya fedha kutoka kwenye ada za wanachama kila mwaka,
· Chadema wamefanya harambee ya nchi nzima mara kadhaa, nakumbuka ipo iliyofanyika Dar es Salaam (Serena hotel) na Arusha (hotel ya Mrema nimeisahau jina), na Mwanza kwa kuwataka Watanzania kuwachangia electronically. Hata mara moja hawajawahi kutoa ‘feedback’ kwa Watanzania hawa waliochanga. Kama wanabisha na ni wawazi kama wanavyojinasibu, watoe taarifa kwa kila tukio.

Hapo hatujaweka michango ya wanachama nchi nzima kila mwaka, Hivyo haya ni sehemu ya makusanyo yao ya miaka 5 tu kama Chama ambacho kimekuwa Chama kikuu cha upinzani nchini kwa miaka takribani 20, bado hii leo:

i. Hakina ofisi yao kama jengo, pamoja na kununua eneo miaka ya nyuma ili kuweka jengo la ghorofa 11kwa minajili ya kujenga ofisi yenye hadhi ya chama kikuu cha upinzani na kupangisha maeneo mengine. Ni kama Milioni 150 zilizotumika kununua eleo zilitupwa tu. Ofisi hii ya Chama inayotumika leo ilinunuliwa na Bob Makani. Kina Mbowe na Lissu wanaojinasibu kuwaletea Maendeleo Watanzania hawajawahi kufanya lolote pamoja na kujikusanyia mabilioni ya pesa kila mwaka.
ii. Makatibu wake wa wilaya wengi (kama sio wote) nchi nzima hawalipwi mishahara wala posho,
iii. Leo hii kampeni zinaendelea Chama hakina pesa za kuendesha kampeni, badala yake wanapitisha kofia kuwachangisha wananchi katika mikutano ya kampeni.

Hii pesa yote iko wapi? Kama imewekezwa, imewekezwa wapi? Mbona wabunge wao wanalalamika wakihoji haya wanaambiwa hakuna kuhoji?

Haya matumizi mabaya yote ya pesa yanafanyika wakati Tundu Lissu (eti mpenda haki huyu, na mtetezi dhidi ya ukandamizaji, na mwanademokrasia) akiwa ‘amebandikwa’ nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Chama, na Makamu Mwenyekiti wa Chama. Wanachama wanalalamikia haya yote, mwanasheria anateyakiwa kuwatetea, Bwana Tundu Lissu ametulia tulii kama vile hakuna kilichotokea yaani! Eti leo anaimba uhuru, haki na maendeleo wakati Chadema yake hakuna Uhuru, Chadema yake hakuna Haki, Chadema yake hakuna Maendeleo!, nay eye ni Kiongozi mwandamizi wa Chadema.

Ni huyuhuyu Tundu Lissu na Chadema wake wanataka Watanzania wawape ridhaa ya kusimamia utajiri wote wa nchi, waratibu matumizi ya matrilioni ya kodi zote zinazokusanywa nchini, wasimamie miradi yote ili eti walete ustawi kwa Watanzania.

Ni huyu huyu Tundu Lissu na Mbowe ambao ni viongozi wakuu wa Chadema miaka nenda rudi bado wanapanga makao makuu ya chama taifa kwenye nyumba ya mtu (mtaa wa Ufipa-Kinondoni), ndo wanasema eti watawasomesha bure Watanzania, eti watawatibu bure Watanzania wote.


Sasa ona hii, Lissu anajiita eti ni mwanasheria anayesimamia katiba na sharia. Hivi hiyo nafasi ya Mwanasheria wa Chama aliyonayo ndani ya Chadema iko kikatiba? Atoke huko atuonyeshe kwenye katiba kama kuna nafasi ya mwanasheria wa Chama kikatiba. Huyu huyu ameshindwa kusimamia haki ndani ya Chama, ameshindwa kutetea uhuru wa wanaokandamizwa ndani ya chama kiasi cha anayehoji tu anafukuzwa uanachama, ameshindwa kusimamia na kuheshimu katiba ya chama; eti leo hii anataka kusimamia haya akiwa Rais wa Tanzania?

Wahenga walisema “sumu haijaribiwi kwa kuionja”, Chadema hii ya Lissu na Mbowe ni sumu kwa Watanzania.

Ripoti ya CAG inasemaje kuhusu CCM na CDM. Tuanzie hapo ili kupata chama bora kupewa nchi.

Pia CCM iweke wazi inakopata hela za kujengea majengo ya kisasa na magari ya kifahari etc

Hakika naapa, CCM sheria ya utakatishaji fedha inaihusu. Mbele ya chombo huru cha uchunguzi, CCM haina uwezo wa kuelezea chanzo chake cha mapato kilicho halali mbele ya sheria.
 
hahahaaa ndio umejitahidiiii kuorodhesha...kwani kama hizo zote ni kero sasa si uache hiyo kazi uje huku kitaa uone kama hujarudi faster? Wewe ukiona kazi mbaya na haina maslahi kwako achana nayo. Hivi unajua kuna kina mama mtaani wanatembeza mboga na mtoto mgongoni na jua kali na faida kwa siku haifiki hata buku 3? Leo wewe nyau unalilia hela ya likizo kwani ulipoomba kazi kazi hukujua utatakiwa kurudi kwenu? Acha kazi kama mbaya.
Nyie ndio ccm wajinga jiwe anaowahitaji
 
Wapo walimu kibao watampigia wanaipenda CCM na JPM wewe kura yako moja haitabadili kitu!
Ulitakiwa kujibu hoja kwa vipengele ... sasa haya mambo ya kulazimisha kumpigia kura mtu huku mkilazimisha apendwe hayapo tena, mapenzi kwa mgombea yatoka moyoni sio kulazimishana hatumpi kachemka

Tunapiga na kumpa mgombea kura kulingana na sera na ahadi sio kwa mapenzi ya kulazimisha wapumbavu mmeng'ang'ania miundo mbinu, flyover, ndege ... matatizo kama hayo ya waalimu ndio vitu vya kipaumbele ili kuboresha maisha ya watu na sio vitu

#NI YEYE TU 2020 !!!
 
Kwa nyongeza tu kuonyesha ubabe na ukatili wa JPM, baada ya sheria mpya ya bodi ya mikopo iliyopitishwa makato ya asilimia 15 kutoka 8, kuna watumishi wanapokea mshahara hadi elfu tisini kwa kuwa walikuwa wamekopa kwenye benki kabla huku wakiacha 1 ya 3 kama sheria inavyohitaji, kwa lugha rahisi sheria mpya ya bodi ya mikopo imekiuka hata miongozo wa mtumishi kubaki na kiasi cha moja ya tatu baada ya makato!
 
Siyo mwalimu huyo dalali tu, annual increment kila mwaka imekuwa ikiingia. Madaraja walimu tunaostahili tumepandishwa wale waliostahili kupandishwa halafu hawakupandishwa pasipo sababu walipolalamika maafisa utumishi waliwajibishwa.

Acha kudandia taaluma za watu mimi ni mwalimu niko pamoja na Magufuli.Jikite kwenye siasa zako siyo kuwasemea waalimu.
Wewe sio mwalimu ni kanjanja tu!
 
Duuu umeandika kwa Uchungu,poleni walimu jmn.Hapo bado makundi mengine hapo hayajatoa kero zao_Oct.28 kampeni delete CCM#Twendeni tukapige kura.
 
Kila siku watu wanakilmbilia ualimu wanapenda .ualimu ni wito
Hii kazi yako ni ya "wito" pia?
Bila shaka anayekulipa kwa kufanya kazi unayofanya hapa jukwaani siku si nyingi ataona pesa yake imepotea bure. Utakuwa huna kazi tena.
 
We sio mwalimu no kanjanja flani usie jua unacho kiongea natamani ata nikutafune mzima mzima
Kama ni kutetea ugali wako kiivyo umefeli kabisa afu ukute we ni kula kulala hujui ata adha ya kutafuta mkate wa kila siku
Watu wanaugua mafua kila siku unashindwa at a hela ya maziwa we unaleta porojo zako hapa pumbafu kabisa
Huoni hata aibu?
Hebu linganisha tu hata uandishi wako na wake..., hata hili hujui ninachoandika hapa?
 
Pamoja na kujipitisha mashuleni kutuomba kura za huruma, mie nimeamua kura yangu sitampa mgombea wa ccm kama nilivyofanya 2015 hii ni kutokana na mambo 10 niliyoyaona kipindi hiki cha miaka mitano

1. Makato ya bodi ya mikopo toka 8% hadi 15% bila sababu maalum tena kwa ubabe.

2. kutunyima nyongeza ya mshahara (annual increment) kwa miaka takribani mitano wakati ni haki ya msingi ya mtumishi.

3. Kutopandishwa daraja mwaka wa 6 huu unakwenda wa 7. Mie nimeajiriwa mwaka 2014 mwezi Aprili, mpaka leo Oktoba 2020 takribani miaka sita imepita huku nikilipwa mshahara wa TGTS D ambao ndio nilioanza nao mwaka 2014 na hata anayeajiriwa leo naye atalipwa hivyohivyo. Halafu wasanii wa bongo fleva wanatanua na kuchezea hela ya serikali kwenye kampeni zako.

4. Kutolipa hela ya likizo kwa wakati. Mfano mie likizo ya malipo nimeenda juni 2017 na juni 2019 JPM ukiwa madarakini, likizo zote nimesafiri toka Lindi hadi Mwanza bila kulipwa hata senti, mwaka huu ndio nimepewa hela ya likizo ya mwaka 2017 tena nusu tu.

5. Hela ya usimamizi wa mitihani ya Taifa kidato cha 4, 2 na 6 kutolipwa yote ya mwaka 2018 na 2019 huku siku za usimamizi (za malipo) kwa wataalamu wa maabala zikishushwa kuanzia mwaka huu toka siku 6 hadi moja.

6. Sheria mpya ya wastaafu ambayo umejifanya Kuibatilisha hadi 2022 ni geresha tu kupisha uchaguzi mkuu huu ufanyike na baada ya hapo kikokotoo kipya kianze kazi. malipo ya mkupuo kwa wastaafu (Lumpsum) kwa Kikokotoo kipya kinataka mstaafu apewe 25% ya mafao yake yote, na 75% zinazobaki apewe kidogokidogo hadi kufa kwake mfano milioni 100 upewe milioni 25 halafu milioni 75 nilipwe kidogokidogo. Mie kama mtumishi hii kwangu haiingii akilini na ili isiniumize ni kukunyima tu kura yangu

7. Ulituahidi Laptop kila mwalimu 2015 lakini muda wako wa awamu ya kwanza unaenda mwishoni bila dalili yoyote ya kupewa hiyo Laptop.

8. Uzalilishaji unaofanywa na wateule wako kama Ma-RC na ma-DC mbele ya wanafunzi wetu na wewe umekuwa kimya. Mfano kutulazimisha kulala kwenye mwenge tena kwa kuitwa majina kama watoto.

9. Ninachangia bima ya afya (3%) kila mwezi halafu dawa za muhimu zimeondolewa na unapoenda hospitali tunalazimika kujinunulia kwa hela yetu.

10. Sababu za Kutoa kufundisha walimu wa masomo ya sanaa wa sekondari kwenda shule za msingi ni za ajabu sana
Mkuu umeongea kwa hisia kali...pole sana.

Watanzania wamekusikia na watakuunga mkono wiki ijayo.
 
109 Reactions
Reply
Back
Top Bottom