Kwa malezi haya, ndoa nyingi zitaendelea kuvunjika!

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Kuna ndugu yangu wa kike 18 miaka, anasoma chuo karibu na ninapoishi. Yeye anaishi kwa mama yake mdogo mbali na chuo. Nilimkaribisha awe anakuja mchana anapika na kula kwangu ili kupunguza gharama za kununua chakula na ufunguo nikampatia. Chakula chote nanua naweka ndani ikijumuishwa na mboga huwa naipika na kuhifadhi kwenye kafriji kangu. Tatizo sasa, atakuja atapika na kula na vyombo anaviacha vichafu. Nikirudi kutoka kazini naviosha. Kuna siku nilisafiri na niliporudi nikaona vyombo vyote vichafu na nikaviosha. Siku moja nikamueleza kistaarabu awe anaosha vyombo anavyovitumia. Kuanzia siku hiyo hajakanyaga tena kwangu. Ninajiuliza, kumsisitiza usafi ni kosa? Hili mara nyingi linajitokeza hata kwenye ndoa kutokana na watu kushindwa kufanya vitu vidogo kama kuosha vyombo, kupika, kutandika kitanda, kupiga deki nk na kupelekea ndoa kuwa na migogoro. Wito wangu kwenu wazazi: wafundisheni watoto wenu wazijue kazi ndogo ndogo hata kama wanasoma boarding! Wakirudi likizo wajifunze hata kuosha vyombo na kufua.
 
Nakumbuka tukiwa wadogo mama yetu alikuwa anasisitiza sana kuhusu usafi. Kikionekana chombo kichafu mnachapwa wote aafu mwenye zamu anaongezewa juu. Akiingia chumbani hakujatandikwa au kupigwa deki mnawajibishwa wote mnaolala humo. Watoto wenu wa siku hizi mnavyowalea mnajua wenyewe.! Dijitali isitufanye tukawa wa ajabu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ni kweli kuna wazazi uwa wanajisahau..mtoto akisoma basi afanyi kazi kisa anasoma...

Kusoma kusifanya watoto wakashindwa hata kufua nguo za. Kipindi nasoma advance kuna jamaa alikuwa anavaa nguo zikichafuka anakusanya zote kwenye begi na kwenda kuagiza hood ili zikafuliwe aafu anarudi na begi jingine lenye nguo safi. Chuoni ndio nikakutana na wadada wanaowapa wale wafanya usafi mpaka chup.i wawafulie.! Nikawa najiuliza ikilowekwa na kutolewa si wanavaa uchafu hawa? Na familia zao zitakuja kuwaje? Je, kupika ataweza huyu?
 
huyo ndugu yako ana asili ya uchafu tuu.Chunguza vizuri ukoo wenu utaliona tatizo hilo
 
huyo ndugu yako ana asili ya uchafu tuu.Chunguza vizuri ukoo wenu utaliona tatizo hilo

Mkuu sikubaliani na wewe. Suala la usafi halina ukoo wala undugu. Vile mnavyolelewa tangu utotoni na ukubwani kwenu mtakuwa hivyo kama hamtajifunza na kubadirika. Mtu kama hajafundishwa kuuchukia uchafu tangu akiwa mdogo ataendelea kuwa hivyo hata akiwa mkubwa. Na mtoto asipofundishwa kufanya kazi ndogo ndogo akija kuwa na familia yake ataona maisha magumu sana! Ndio maana malalamiko ya kuibiwa wanaume na house girls hayaishi kwani wanawake wanawaruhusu sana hg kuingia chumbani kwao.
 
yaweza kuwa tunamlaumu lakini watoto wakike wengi hawajui kazi za nyumbani, kuanzia kupika, kuosha vyombo, usafi wa nyumba na hata wao wenyewe pia....
 
  • Thanks
Reactions: BAK
wewe pia ulimuendekeza...

Unajua mwanzoni nilijua labda atabadilika lakini nikagundua ni mtu asiyekerwa na kuona vyombo vichafu! Nilipomuelekeza ndio amekacha hata kuja kwangu! Kumbe ni mmoja wa masistaduu ambao wanaonekana safi kwa nje tu!
 
Unajua mwanzoni nilijua labda atabadilika lakini nikagundua ni mtu asiyekerwa na kuona vyombo vichafu! Nilipomuelekeza ndio amekacha hata kuja kwangu! Kumbe ni mmoja wa masistaduu ambao wanaonekana safi kwa nje tu!

mtu anapokuja kukaa kwako ni shurti afahamu kanuni zako za maisha na azifuate INSTANTLY...siku ya kwanza tu alivyoacha vyombo vichafu.,ulipaswa ficha vyakula vyote hadi aoshe vyombo...no more kupikika.
 
mtu anapokuja kukaa kwako ni shurti afahamu kanuni zako za maisha na azifuate INSTANTLY...siku ya kwanza tu alivyoacha vyombo vichafu.,ulipaswa ficha vyakula vyote hadi aoshe vyombo...no more kupikika.

Hakai kwangu. Nilimpa nafasi ya kupika na kula chakula cha mchana ili kupunguza bajeti yake ya mchana. Hivyo alikuwa anapika, anakula na kuondoka.
 
yaweza kuwa tunamlaumu lakini watoto wakike wengi hawajui kazi za nyumbani, kuanzia kupika, kuosha vyombo, usafi wa nyumba na hata wao wenyewe pia....

Wazazi wengi wamekuwa wakiwaachia watoto wao hata kujifunza mambo ya muhimu. Wanawafanyia kitchen part ya kimbea, sendoff na baada ya mwezi mmoja binti anarudi nyumbani kisa mume anataka apike, hawezi kutandika kitanda, etc. Anachojua yeye ni kujipamba tu kutwa nzima.
 
^^
Nyalotsi
Unakuta wengi nguo anafuliwa na housegirl,vyombo housegirl,Mama wa familia akimkuta anapika chakula siku hiyo housegirl asipopigwa bahati yake,
Kazi ya binti wa Mama ni kula,kujisomea,kuchart facebook na kujifunza kubana pua huku akifanya majaribio ya kutembea kimiss chumbani kwake!
Mguse kidogo tu atazira,atanuna,ataona unamtesa..
MTOTO ANADEKEZWA UTADHANI NI AGIZO LA SANGOMA
^^
 
Last edited by a moderator:
^^
Nyalotsi
Unakuta wengi nguo anafuliwa na housegirl,vyombo housegirl,Mama wa familia akimkuta anapika chakula siku hiyo housegirl asipopigwa bahati yake,
Kazi ya binti wa Mama ni kula,kujisomea,kuchart facebook na kujifunza kubana pua huku akifanya majaribio ya kutembea kimiss chumbani kwake!
Mguse kidogo tu atazira,atanuna,ataona unamtesa..
MTOTO ANADEKEZWA UTADHANI NI AGIZO LA SANGOMA
^^

Mkuu ndo ukweli kabisa. Ukisikiliza visa wanavyosema wananyanyaswa ni kwa sababu ya vitu vidogo tu! Kuna dada mmoja namfahamu walitengana na mumewe kwa sababu ya kushindwa kupika. Mwanzani alikuwa akipika hg baada ya kuondoka akawa anamnunulia mumewe chipsi. Mume alipomlazimisha apike akawa anapika kibichi. Alipoona jamaa anakomaa akaamua kuondoka kisa anateswa.
 
Last edited by a moderator:
Kuna ndugu yangu wa kike 18 miaka, anasoma chuo karibu na ninapoishi. Yeye anaishi kwa mama yake mdogo mbali na chuo. Nilimkaribisha awe anakuja mchana anapika na kula kwangu ili kupunguza gharama za kununua chakula na ufunguo nikampatia. Chakula chote nanua naweka ndani ikijumuishwa na mboga huwa naipika na kuhifadhi kwenye kafriji kangu. Tatizo sasa, atakuja atapika na kula na vyombo anaviacha vichafu. Nikirudi kutoka kazini naviosha. Kuna siku nilisafiri na niliporudi nikaona vyombo vyote vichafu na nikaviosha. Siku moja nikamueleza kistaarabu awe anaosha vyombo anavyovitumia. Kuanzia siku hiyo hajakanyaga tena kwangu. Ninajiuliza, kumsisitiza usafi ni kosa? Hili mara nyingi linajitokeza hata kwenye ndoa kutokana na watu kushindwa kufanya vitu vidogo kama kuosha vyombo, kupika, kutandika kitanda, kupiga deki nk na kupelekea ndoa kuwa na migogoro. Wito wangu kwenu wazazi: wafundisheni watoto wenu wazijue kazi ndogo ndogo hata kama wanasoma boarding! Wakirudi likizo wajifunze hata kuosha vyombo na kufua.

una uvumilivu wa hali ya juu!!!!
 
Kusoma kusifanya watoto wakashindwa hata kufua nguo za. Kipindi nasoma advance kuna jamaa alikuwa anavaa nguo zikichafuka anakusanya zote kwenye begi na kwenda kuagiza hood ili zikafuliwe aafu anarudi na begi jingine lenye nguo safi. Chuoni ndio nikakutana na wadada wanaowapa wale wafanya usafi mpaka chup.i wawafulie.! Nikawa najiuliza ikilowekwa na kutolewa si wanavaa uchafu hawa? Na familia zao zitakuja kuwaje? Je, kupika ataweza huyu?

Kwa kweli kwa sasa ni janga unakuta msichana yupo chuo hata kupika hajui anasubiri apate ajira aweke housegirl mi naona wanaume nao waamke watumie kigezo cha mwanamke kujua domestic work kama kigezo cha kuoa kama ilivyokuwa zamani.Jamani inakera na mimi daima namchukia msichana mvivu wa kufanya shughuli za nyumbani,utakuta mdada mkubwa tu mpangilio wa nguo zake tu hawezi zimetupwa kila kona sasa itakuwaje akija kuwa na watoto yani kwa kweli inasikitisha
 
^^
Nyalotsi
Unakuta wengi nguo anafuliwa na housegirl,vyombo housegirl,Mama wa familia akimkuta anapika chakula siku hiyo housegirl asipopigwa bahati yake,
Kazi ya binti wa Mama ni kula,kujisomea,kuchart facebook na kujifunza kubana pua huku akifanya majaribio ya kutembea kimiss chumbani kwake!
Mguse kidogo tu atazira,atanuna,ataona unamtesa..
MTOTO ANADEKEZWA UTADHANI NI AGIZO LA SANGOMA
^^

wakute wanavyo nata kwa nje sasa na nyie wanaume mbadilike wachunguzeni katika kipindi cha uchumba ikiambatana na makavu laivu hakuna kumwonea aibu maana utakuwa unaharibu kizazi chako kijacho
 
Last edited by a moderator:
Hicho kigezo baadhi ya wanaume wameshaanza kukitumia. Ni wanaume wachache sana wanapenda vyakula vinavyopikwa na HG siku nenda siku rudi. Na kujua kupika vyakula vingi vya Kitanzania ikiwemo mahanjumati hicho nacho ni kigezo kinachozidi kutumiwa miaka ya karibuni. Miaka ya nyuma ilikuwa si rahisi kumkuta binti wa Kitanzania wa miaka kuanzia 14 hajui kupika lakini siku hizi wako wa kumwaga.

Kwa kweli kwa sasa ni janga unakuta msichana yupo chuo hata kupika hajui anasubiri apate ajira aweke housegirl mi naona wanaume nao waamke watumie kigezo cha mwanamke kujua domestic work kama kigezo cha kuoa kama ilivyokuwa zamani.Jamani inakera na mimi daima namchukia msichana mvivu wa kufanya shughuli za nyumbani,utakuta mdada mkubwa tu mpangilio wa nguo zake tu hawezi zimetupwa kila kona sasa itakuwaje akija kuwa na watoto yani kwa kweli inasikitisha
 
wakute wanavyo nata kwa nje sasa na nyie wanaume mbadilike wachunguzeni katika kipindi cha uchumba ikiambatana na makavu laivu hakuna kumwonea aibu maana utakuwa unaharibu kizazi chako kijacho

^^
The secretary asilimia kubwa ya wasichana wa aina hii wanageuzwa sex toys na mashorobaro wao! Niliwahi kuleta mada humu MMU inayosema 'Unavuta watu wa aina yako'
Binti wa aina hiyo ni mzigo wa baba yake na aibu ya mama yake
^^
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom