Kwa maisha ya sasa sio ya kuokota/ kununua kwa mtu simu aina ya smartphone; ni bora ukaokota 'Nokia Tochi'

mkuu IMEI ya simu inabadilika kweli? Basi kipindi kile simu feki zinafungiwa watu si wangebadili IMEI?
Ukibadili TCRA inaonekana fake. Kuna simu yangu nilishabadili baadaye ilifungiwa mpaka nikarudisha IMEI zake og.
 
Sikuzote mtu wa IT huwa hafanyi mambo kwa kubahatisha na huwezi kujiwekea imei tu ovyo ovyo. Kuna vyanzo vingi vya kupata imei ila huwa ni trusted na ukiweka hakuna mtu atakayegundua au TCR.
Unawezaje kuthibisha kwamba hata TCRA hawawezigundua?
 
Kwa maisha tuliyo fikia sasa siyo ya kuokota/kununua kwa mtu simu aina ya smart phnone.

Ndugu zanguni katika mahangaiko yenu huko njiani/barabarani ukikutana na simu aina ya SMART PHONE imedondoshwa, usithubutu kuokota we ipite tu endelea na safari yako.

Kuna mtu huku mtaani kwangu wiki moja iliyo pita katika harakati zake za mizunguko njiani aliokota simu aina ya SMART PHONE alifurahi sana alihisi bahati imemdondokea kwa siku hiyo. Jamaa alianza kuitumia ile simu, hiyo ni baada ya kuweka details zake zote zikiwemo line na email address yake.


Baada ya siku kadhaa, jamaa alishangaa anafuatwa na watu walio jitambulisha kuwa wao ni askari na yupo chini ya ulinzi anahitajika police. Huko police aliambiwa kuna mama mmoja alivamiwa nyumbani kwake na kuibiwa pesa nyingi sana ikiwemo na simu yake, na simu yenyewe ni hiyo ambayo jamaa alikuwa ameikota.

Huku mtaani baada ya kusikia hivyo tulistuka sana kwani jamaa hanaga matukio yoyote ya uharifu, mpaka saizi tupo tunachangishana ili tuka mtoe sero jamaa.

Lakini saizi nasikia kuna mtindo umevuma wa kudondosha simu (aina ya smart phone) kwa makusudi alafu baadaye huyo aliye dondosha anaenda kuripoti police kuwa amevamiwa na kuporwa simu na fedha nyingi ( anataja kiasi anacho kijua yeye). Mwisho wa siku wewe kama uliokota hiyo simu na police waki itraki hiyo simu wanakuja kukukamata.


USHAURI: Kwa maisha tuliyo fikia sasa sio ya kuokota hizi simu za SMART PHONE, ukiokota/ kununua kwa mtu usiye mfahamu utakuwa unajitakia matatizo mwenyewe ni bora ukaokota NOKIA TOCHI lakini sio SMART PHONE.


....[HASHTAG]#SWIZZY[/HASHTAG]
kwani Nokia tochi hawawezi kuitraki?
 
aiseh!! vipi kwa upande wa PC (personal computer) nako kuna maujanja kama hayo maana kuna kisa kimoja kimewahi tokea huku mtaani kwetu, ilikuwa hivi:-

kuna jamaa wawili walikuwa wanafanya kibarua kwenye ujenzi wa barabara zinazo simamiwa na wachina (mkandarasi alikuwa ni mchina).

Wale jamaa walifanya tukio la wizi kwenye gari ya mchina, walifanikiwa kuiba PC (laptop moja) yenye data zote za barabara. Walishindwa kuitumia baadaye wakaenda kwa fundi Computer ili awatolee password na vitu vingine, yule fundi alifanikiwa lakini cha ajabu alipokuwa anaendelea kuitumia hiyo PC mara ghafla ikaanza kupiga picha yenyewe automatically, yule fundi ali haha nakuamua kuizima.

Kesho yake yule fundi hakuonekana kazini alafu siku hiyo hiyo wachina walikuja pale kwenye office ya yule fundi waki iulizia hiyo PC na kutangaza dau nono kwa watu walio kuwepo pale kuzunguka lile duka. Fundi alivyosikia habari hizo hakuonekana tena mahali pale. Mpaka leo sijui wale wachina kama walifanikiwa kuikuta ile PC.


Sasa wewe kama mtu wa IT naomba kujua wale wachina walitumia utalaamu gani hadi ile PC kuwa inapiga picha yenyewe then mwisho wa siku wakaja wachina eneo lilelile?
Hizo ni program tu mkuu ambazo unaziweka kwenye laptop. Hizo program zipo nyingi ila ni za kulipia ambapo baada ya kuinstall unajaza email (Hasa hasa email) na namba za simu. Kwahiyo ili upate taarifa zote lazima huyo muhalifu (aliekuibia PC) awe online yaan awe na internet access.
Hapa inategemea na program yenyewe.
1. Kuna zingine ukishawasha pc inaanza kupiga picha au ukifika stage ya kuweka password (Kusign in) yenyewe inapiga picha kimya kimya na nyingine inapiga mpaka ww unajua kuwa unapigwa picha.

2. Kuna program zingine mpaka u-log in kisha inapiga picha (Hasa pale unapokosea password)
Program zote zipo connected na email kwahiyo picha zote zinahifadhiwa kwenye hiyo program na unapokuwa online inatuma picha zote yenyewe km inavyofanya app za anti thief.
Kama hajaingia mtandaoni ni ngumu kumpata huyo fundi aliingia mtandao kwahiyo hiyo program ikatuma picha zote kwenye email.

3. Kuna zingine ukiwa online inapiga picha na inatuma wakati huo huo.


4. Njia nyingine ni through IP address kila pc ina IP address yake kwa hapa mtu akiingia mtandaoni unampata kirahisi ila akitumia VPN ( Hii ni program inayotumika kuficha IP address ) ni ngumu kumpata. Unakumbuka page ya TANZAGIZA? huyu alikuwa anatumia VPN kwahiyo ukimtrack itakuonesha yupo india, marekani, kwahiyo ni ngumu kumpata. Hapa kama hajatumia vpn na yupo online wanamtrack na unaicommand pc yako kupiga picha na kutuma inategemea na program au tracking device uliyonayo.

Watu wengi tumeshazoea kuinstall program kwenye local disk C ( Disk yenye window) kwahiyo program unaweza kuinstall hata kwenye disk zingine. Hata ukipiga window inakuwepo tu mpaka u-uninstall kwahiyo hapa unaificha program.
Alichokosea huyo fundi ni kubypass password ya hiyo pc na kuwa online hilo ni kosa kubwa sana alilolifanya ila kama angetumia offline asingekamatwa.


N.B
Kumtrack mtu aliyeiba PC ni ngumu siyo rahisi hata TCRA wanalijua hilo. Mtu akipoteza Laptop na Simu mwenye simu ni rahisi sana kuipata kuliko pc. Kingine ss wabongo huwa hatujali kuangalia IP address na kuweka hizo program (Hizo program ni ghari utakuta program mmoja unainunua kwa 70,000 mpaka laki 2 inategemeana na ubora wa program yenyewe Hebu jiulize PC yenyewe ya laki 4 utaweza kununua program ya laki 2? kwahiyo mtu akinunua pc hata hangalii IP adress yy anachokumbuka ni kuweka media player na kuangalia movie tu.
 
Ukibadili TCRA inaonekana fake. Kuna simu yangu nilishabadili baadaye ilifungiwa mpaka nikarudisha IMEI zake og.
Uliweka Imei ya simu iliyofungiwa. Je walikukamata? kukamatwa siyo rahisi
Unapoweka IMEI uangalie na aina ya simu siyo unaweka imei kwa guess unajikuta unachukua ya nokia ya tochi unaweka kwenye HUAWEI hapo lazima waifunge. IMEI inatambulisha aina ya simu .
Ndiyo maana unapotuma sms ya kuomba internet setting kwa nokia ya tochi watakuambia imei yako haisapport internet setting. Ushajiuliza kwann?
 
Unawezaje kuthibisha kwamba hata TCRA hawawezigundua?
Unapobadilisha IMEI lazima uangalie na aina ya simu. Siyo unachukua imei yyte au unachuka imei kutoka kwenye simu ya Button unaweka kwenye smartphone. Hapo lazima wagundue.
Unapochukua imei sharti iwe inafanana na simu yako. IMEI zinabadilishwa sana na TCRA hata hawagundui km umebadilisha
 
Hizo ni program tu mkuu ambazo unaziweka kwenye laptop. Hizo program zipo nyingi ila ni za kulipia ambapo baada ya kuinstall unajaza email (Hasa hasa email) na namba za simu. Kwahiyo ili upate taarifa zote lazima huyo muhalifu (aliekuibia PC) awe online yaan awe na internet access.
Hapa inategemea na program yenyewe.
1. Kuna zingine ukishawasha pc inaanza kupiga picha au ukifika stage ya kuweka password (Kusign in) yenyewe inapiga picha kimya kimya na nyingine inapiga mpaka ww unajua kuwa unapigwa picha.

2. Kuna program zingine mpaka u-log in kisha inapiga picha (Hasa pale unapokosea password)
Program zote zipo connected na email kwahiyo picha zote zinahifadhiwa kwenye hiyo program na unapokuwa online inatuma picha zote yenyewe km inavyofanya app za anti thief.
Kama hajaingia mtandaoni ni ngumu kumpata huyo fundi aliingia mtandao kwahiyo hiyo program ikatuma picha zote kwenye email.

3. Kuna zingine ukiwa online inapiga picha na inatuma wakati huo huo.


4. Njia nyingine ni through IP address kila pc ina IP address yake kwa hapa mtu akiingia mtandaoni unampata kirahisi ila akitumia VPN ( Hii ni program inayotumika kuficha IP address ) ni ngumu kumpata. Unakumbuka page ya TANZAGIZA? huyu alikuwa anatumia VPN kwahiyo ukimtrack itakuonesha yupo india, marekani, kwahiyo ni ngumu kumpata. Hapa kama hajatumia vpn na yupo online wanamtrack na unaicommand pc yako kupiga picha na kutuma inategemea na program au tracking device uliyonayo.

Watu wengi tumeshazoea kuinstall program kwenye local disk C ( Disk yenye window) kwahiyo program unaweza kuinstall hata kwenye disk zingine. Hata ukipiga window inakuwepo tu mpaka u-uninstall kwahiyo hapa unaificha program.
Alichokosea huyo fundi ni kubypass password ya hiyo pc na kuwa online hilo ni kosa kubwa sana alilolifanya ila kama angetumia offline asingekamatwa.


N.B
Kumtrack mtu aliyeiba PC ni ngumu siyo rahisi hata TCRA wanalijua hilo. Mtu akipoteza Laptop na Simu mwenye simu ni rahisi sana kuipata kuliko pc. Kingine ss wabongo huwa hatujali kuangalia IP address na kuweka hizo program (Hizo program ni ghari utakuta program mmoja unainunua kwa 70,000 mpaka laki 2 inategemeana na ubora wa program yenyewe Hebu jiulize PC yenyewe ya laki 4 utaweza kununua program ya laki 2? kwahiyo mtu akinunua pc hata hangalii IP adress yy anachokumbuka ni kuweka media player na kuangalia movie tu.
ahsante sana kwa kunielewesha mkuu, kuhusiana na PC sina swali majibu uliyonipa nime yapata vizuri.


ila hapo kwenye bei ya program ni kweli wabongo wengi hatuwezi, mbongo anunue program kwa Tsh 200,000/= hawezi
 
Ukibadili TCRA inaonekana fake. Kuna simu yangu nilishabadili baadaye ilifungiwa mpaka nikarudisha IMEI zake og.
vipi kwa ule mtambo wa tcra, unafanya kazi frequently? kwa mfano mtu akiingiza simu fake saizi hapa Tz itafanya kazi? au ndo huo mtambo unafanya kazi frequently
 
Ukibadili TCRA inaonekana fake. Kuna simu yangu nilishabadili baadaye ilifungiwa mpaka nikarudisha IMEI zake og.
vipi kwa ule mtambo wa tcra, unafanya kazi frequently? kwa mfano mtu akiingiza simu fake saizi hapa Tz itafanya kazi? au ndo huo mtambo unafanya kazi frequently
 
vipi kwa ule mtambo wa tcra, unafanya kazi frequently? kwa mfano mtu akiingiza simu fake saizi hapa Tz itafanya kazi? au ndo huo mtambo unafanya kazi frequently
Haitofanya kazi sbb wameset, simu ambazo imei yake haijulikani haiwezi kufanya kazi. Imei inatambulisha aina ya simu na kampuni kwahiyo ni ngumu lbd ubadilishe imei.
Ndiyo maana kwasasa simu km Oking, bluetooth n.k ni ngumu kuzipata. Ila simu iliyofungiwa bongo ukienda msumbiji inapiga kazi km kawaida sbb huko hawatumi system km yetu.
Jaribu kuomba setting za internet kwa nokia ya tochi km watakutumia. Hapo hata usubiri miaka 100 hawakutumii.
Hapo hujue imei ni muhimu.
 
Kuflash simu siyo kosa. Ingekuwa hivyo watu wengi sana wangekuwa wameshakamatwa. Kuna program na mabox mengi yanatumika kuflash simu. Hata hao wafanyakazi wa TCRA simu zao wanazipeleka kwa mafundi kwa ajili ya kuflashiwa. Juzi nimeflash nokia belle 500 na hakuna alyenikamata.
Kosa ni kubadilisha IMEI ila kurepair IMEI siyo kosa.
By flashing i meant changing the IMEI
 
Mimi naiyokota vizuri tu labda I phone kidogo lakini sitiyacha nitauza kama spare msiogope android phone no laisi Ku root unaifuta mpka IMEI number na inapiga mzigo fresh
 
Haitofanya kazi sbb wameset, simu ambazo imei yake haijulikani haiwezi kufanya kazi. Imei inatambulisha aina ya simu na kampuni kwahiyo ni ngumu lbd ubadilishe imei.
Ndiyo maana kwasasa simu km Oking, bluetooth n.k ni ngumu kuzipata. Ila simu iliyofungiwa bongo ukienda msumbiji inapiga kazi km kawaida sbb huko hawatumi system km yetu.
Jaribu kuomba setting za internet kwa nokia ya tochi km watakutumia. Hapo hata usubiri miaka 100 hawakutumii.
Hapo hujue imei ni muhimu.
nimekusoma mkuu, haukuenda shule kucheza mkuu, hongera sana kwa kutupa maelezo yaliyo nyooka
 
Mimi naiyokota vizuri tu labda I phone kidogo lakini sitiyacha nitauza kama spare msiogope android phone no laisi Ku root unaifuta mpka IMEI number na inapiga mzigo fresh
kuna mjumbe kasema ukiokota nenda kaipeleke police
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom