Kwa mahitaji ya nyumba au chumba cha kupanga Mwenge, Sinza, M/nyamala na Mbezi

Hapa huwaoni wakichangiia ila ulichosema ni ukweli mtu sekta hii imeficha mengi na sijui why serikali inashi dwa kuchukua kodi yake hapa inahangaika na magari tu.

usijali mkuu tumeshajisajili na ofisi tunayo! karibu Sinza kwa Remi ulizia IMMY Brokers
tuko karibu kabisa na barabara ya shekilango road dakika 3 tu umefika
 
VP maeneo ya Kimara suka,over,Kimara,korogwe,bucha,baruti naweza kupata chumba na sebule kwa bei gani
Mkuu inategemea na ubora wa nyumba oia umbali toka morogoro road! ila nyingi nzuri na sio mbali sana na barabara zinaanzia 200k
 
Wakuu hebu mnapokuja na Budget muangalie na maeneo husika na nyumba unayoitaka, Hivi kweli mtu unakuja na budget ya 100,000 mpaka 150,000 unataka nyumba ya vyumba viwili au vitatu iwe na geti la kujitegemea, maji yawepo, iwe na madirisha ya alminium,gypsum, na mashari kibao, maeneo ya sinza,knyama, mwenge au mbezi,
Unategemea kweli upate nyumba?
 
Sawa kwa kinyerezi sina mkuu ila nitakuulizia, mimi nipo zaidi mwenge, sinza na mbezi beach
View attachment 513789 Kama unahitaji nyumba maeneo hayo ya chumba au nyumba ya kuanzia chumba na sebule au kuanzia vyumba viwili na kuendelea usisite kunitafuta, maeneo ni hayo ya Mwenge, Kinondoni, Sinza, Kijitonyama na Mbezi Tangibovu mpaka Makonde na Makongo juu, Tabata, Tegeta, Bunju, wazo,

Pia Shekilango, Urafiki na Ubungo maziwa zipo, Baruti, kimara, temboni, Mbezi mwisho goba wote karibuni

Chumba kimoja moja kipo, chumba na sebule, master, nyumba nzima zipo karibuni.

Namba ni 0713415537 au 0684448888 (hii ipo whatsapp). Fremu za biashara zipo pia.

TUSOME HUU UJUMBE

Habari wana jamvi!

Nimeona leo kulizungumzia japo kwa ufupi kuhusu swala potofu juu ya madalali wa nyumba za kupanga, kumekua na malalamiko mengi kuhusu madalali wa nyumba/vyumba kupandisha bei halisi ya nyumba au chumba ili kupata cha juu, niwaambie tu dalali yoyote wa nyumba ya kupanga hahusiki kabisa kwenye bei ya pango, dalali wa kupanga si kama wa kiwanja, nyumba ya kuuza au magari nk. Dalali wa nyumba yakupanga anachoangalia ni mteja kuingia apate ile ya mwezi mmoja kulingana na bei ya nyumba kwa mwezi, wakati mwingine dalali anahusika kumshawishi mwenye nyumba ili ampunguzie mteja kama mteja kafikia kiwango flani, na wakati mwingine anamwambia mwenye nyumba kwa bei yako nyumba itaka sana ni heri upunguze, chukulia mfano nyumba ni ya 300k mteja ana 280k mimi ninachoangalia ni mteja kupanga ili nipate ile ya mwezi, hapo lazima nitaungana na mteja kumwambia mwenye nyumba hali ni mbaya mpunguzie mteja, kwaniyo nyumba ya 300k hata siku moja dalali hawezi kukuambia ni ya 400k hilo sahau, Dalali anatamani nyumba ya 300k mwenye nyumba ashushe 200k ili apate wateja haraka, kumbuka madalali wako wengi, kama ni mteja wa uhakika nisipomshawishi bosi apunguze mteja alipie, badae dalali mwingine akileta nakosa hata ile, kwahiyo swala la kwamba dalali anahusika kwenye swala la kupanga bei halipo, naamini wenye nyumba tunakibaliana na hili na madalali pia,

Wengi wamekua na kawaida sana ya kuwatukana na kuwaponda madalali ila kumbuka wengi wamekua msaada kwa watu kupata nyumba, kama hutaki kuwatumia madalali basi nyanyuka kwenye kiti chako ofisini hapo kazunguke mtaa kwa mtaa kutafuta nyumba ambayo ipo wazi upange,

Kumbuka nakubaliana sana na wazo kua ni lazima madalali wasajiliwe ili kufanya kazi kiufanisi na weledi, na pia kutafuta mfumo mzuri ambao hautaleta vikwazo kwa dalali, mpangaji na mwenye nyumba, kwahiyo nakubaliana kabisa na wazo la kuunda vyama vya madalali na kusajiliwa!

Pia nakubaliana na kuwapa pole waliosumbuliwa na madalali, kumbuka sijakataa kama ni kweli wapo matapeli, wazenguaji, pia waswahili, na ni kweli inasikitisha pale dalali anapompamba mteja kua nyumba kali ipo wahiii itaondoka, mteja akija anakuta banda la kuku, hii ni kwasababu wengi hawajaelewa kua wakifanya hii kazi kwa weledi ni manufaa kwao, wengi wamekua wanaangalia tu pesa ya hapa na pale ya kula na si kuboresha kipato!
Kumbuka si wote binadam wanafanyana, kila kitu kina changamoto zake, kikubwa ni kupunguza changamoto!
Mm nina nyumba yangu mbezi beach jogoo juu karibu na serikali ya mtaa, naiuza, wee Tunzo nitafutie mteja upate hela ndefu kama ya biko. Njoo pm kwa maelezo zaidi
 
Pia nina frem inapangishwa mwenge njia ya TRA, mwenye uhitaji anichek
 
vip maeneo ya k/ndoni biafra inaweza patikana "single room" bajet ni 35000-40000 kwa mwezi (kuwe na umeme na luku ya kujitegemea na fence)
 
Back
Top Bottom