Robert S Gulenga
JF-Expert Member
- Jan 3, 2013
- 2,160
- 1,492
Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaendelea na uchaguzi wake wa ndani ili kuweza kupata viongozi watakao isimamia Serikali kwa umakini. Hakuna shaka kwa namna siasa za Tanzania zilivyo kwa sasa na mwenendo wa dunia nzima, CCM inahitaji kupata Viongozi makini na waadilifu, werevu, wasomi, wanaojua Tanzania inaelekea wapi na wale wanaoweza kujenga hoja na kujibu hoja za vyama pinzani.
Mkoa wa pwani ni moja ya mikoa iliyobarikiwa kuwa na ardhi ya kutosha na mabwawa ya kutosha, ni mkoa unaoweza kuwa kinara kwa kilimo cha kisasa na pia kuwa kinara wa Viwanda hapa Tanzania. Mkoa wa pwani ni mkoa wenye Historia toka enzi za kupigania Uhuru wa Tanganyika.
Mkoa wa pwani licha ya kubarikiwa mambo mengi bado ni mkoa unaozidiwa GDP na mikoa mingi ya Tanzania, Mkoa unahitaji watu wenye kuona mbali na kusimamia maono ya Kitaifa ili kuweza kubadilisha mkoa from Good to Great.
Wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Pwani- mnaochagua viongozi watakaowawakilisha katika kusimamia na kuleta mabadiliko ndani ya CCM, hakika msifanye makosa , chaguo sahihi kwa wakati sahihi kwa nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mkoa wa Pwani ni Mohamed Omary Mchengerwa.
Wajumbe, watendeeni haki kizazi cha leo na kizaji kijacho cha Mkoa wa Pwani kwa kuweza kuwachagulia mtu makini, mpenda maendeleo na Mzalendo halisi kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ambaye ni Mohamed Omary Mchengerwa.
Kwa kifupi, Mohamed Omary Mchengerwa
1. Mohamed Omary Mchengerwa ni Kijana Muadilifu , uadilifu wake sio wa kutiliwa shaka hata kidogo, ni muda sahihi sasa kwa Mkoa wa Pwani kuwa na muwakilishi katika chama ambaye hata akisimama na Wapinzani au akisimama kukisemea chama atasema bila woga kwasababu hana makando makando na wala hakuna mtu wa kumnyoshea kidole kuwa uadilifu wake ni wa mashaka.
2. Mohamed Omary Mchengerwa ni kiongozi msikivu, ni kiongozi mpenda haki na utu wa kila mtu, kwa Watu wote ambao wamefanya kazi na Mohamed Omary Mchengerwa watakwambia ukiwa na tatizo au una mawazo yako yakuwasilisha yenye manufaa kwa Taifa, hata kama watu wengine wote hawatakusikiliza lakini ukifika kwake mtakaa chini mtakubaliana kutokukubaliana kwa hoja. Wajumbe chagueni muwakilishi ambaye atasikiliza wana CCM wote bila ubaguzi. Mchengerwa ni mtu wa hoja na si mtu wa majungu.
3. Mohamed Omary Mchengerwa ni Kiongozi mwenye kipaji na ubunifu, kwenye Maisha ya kawaida lazima tukubali kuna watu wamezaliwa kuwa na vipaji vya uongozi kama ambavyo watu wengine wamekuwa na vipaji kwenye mpira etc.. Mohamed Omary Mchengerwa kwa muda mfupi aliokuwa kwenye Wizara inayoshughulia Utumishi amefanya mambo mengi kiasi hata pale Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Samia Suluhu Hassan alipoamua akamsaidie katika Wizara inayoshughulikia Michezo, Watumishi wengi walisikitika kwa namna alivyoweza kusikiliza na kushughulikia kero ambazo nyimngine hazikuhitaji fedha bali maamuzi tu. Wajumbe chagueni mtu huyu, CCM inahitaji watu kwa sasa wanaoweza kuwa wabunifu wa kujibu hoja za Wapinzani ambao baadhi yao ni Wasomi na wanauelewa.
4. Mohamed Omary Mchengerwa ni Msomi wa sheria, kwa namna Siasa za Tanzania na Dunia inavyoenda kwa sasa, Chama cha Mapinduzi kinahitaji kuwa na vijana wasomi wanaoweza kutetea hoja, kuelewa uchumi wa dunia, kuelewa nini Chama kinataka katika kukuza uchumi na kuweza kumsaidia Mwenyekiti wa Chama kutekeleza majukumu yake kiurahisi. Mohamed Omary Mchengerwa ni msomi ambaye anaweza kujenga hoja hata kwenye majukwaa ya Kimataifa, huyu ni msomii anayeweza kuzipangua hoja zote za Wapinzani bila kubabaika. Wajumbe huyu ndiye mtu sahihi wa kuwakilisha mkoa wetu wa Pwani.
Wajumbe, Kuna sababu nyingi sana za kusema juu ya kwanini Mohamed Omary Mchengerwa ndiye mgombea sahihi ya uwakilishi katika nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mkoa wa Pwani , itoshe kusema Mkoa wa Pwani unahitaji viongozi wa CCM watakaoutengeneza Mkoa from GOOD TO GREAT kwa kuweza kuisimamia Serikali vizuri ili kuwaletea Maendeleo Watanzania.
MUNGU IBARIKI TANZANIA,
MUNGU MBARIKI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SAMIA SULUHU HASSAN.
Mkoa wa pwani ni moja ya mikoa iliyobarikiwa kuwa na ardhi ya kutosha na mabwawa ya kutosha, ni mkoa unaoweza kuwa kinara kwa kilimo cha kisasa na pia kuwa kinara wa Viwanda hapa Tanzania. Mkoa wa pwani ni mkoa wenye Historia toka enzi za kupigania Uhuru wa Tanganyika.
Mkoa wa pwani licha ya kubarikiwa mambo mengi bado ni mkoa unaozidiwa GDP na mikoa mingi ya Tanzania, Mkoa unahitaji watu wenye kuona mbali na kusimamia maono ya Kitaifa ili kuweza kubadilisha mkoa from Good to Great.
Wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Pwani- mnaochagua viongozi watakaowawakilisha katika kusimamia na kuleta mabadiliko ndani ya CCM, hakika msifanye makosa , chaguo sahihi kwa wakati sahihi kwa nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mkoa wa Pwani ni Mohamed Omary Mchengerwa.
Wajumbe, watendeeni haki kizazi cha leo na kizaji kijacho cha Mkoa wa Pwani kwa kuweza kuwachagulia mtu makini, mpenda maendeleo na Mzalendo halisi kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ambaye ni Mohamed Omary Mchengerwa.
Kwa kifupi, Mohamed Omary Mchengerwa
1. Mohamed Omary Mchengerwa ni Kijana Muadilifu , uadilifu wake sio wa kutiliwa shaka hata kidogo, ni muda sahihi sasa kwa Mkoa wa Pwani kuwa na muwakilishi katika chama ambaye hata akisimama na Wapinzani au akisimama kukisemea chama atasema bila woga kwasababu hana makando makando na wala hakuna mtu wa kumnyoshea kidole kuwa uadilifu wake ni wa mashaka.
2. Mohamed Omary Mchengerwa ni kiongozi msikivu, ni kiongozi mpenda haki na utu wa kila mtu, kwa Watu wote ambao wamefanya kazi na Mohamed Omary Mchengerwa watakwambia ukiwa na tatizo au una mawazo yako yakuwasilisha yenye manufaa kwa Taifa, hata kama watu wengine wote hawatakusikiliza lakini ukifika kwake mtakaa chini mtakubaliana kutokukubaliana kwa hoja. Wajumbe chagueni muwakilishi ambaye atasikiliza wana CCM wote bila ubaguzi. Mchengerwa ni mtu wa hoja na si mtu wa majungu.
3. Mohamed Omary Mchengerwa ni Kiongozi mwenye kipaji na ubunifu, kwenye Maisha ya kawaida lazima tukubali kuna watu wamezaliwa kuwa na vipaji vya uongozi kama ambavyo watu wengine wamekuwa na vipaji kwenye mpira etc.. Mohamed Omary Mchengerwa kwa muda mfupi aliokuwa kwenye Wizara inayoshughulia Utumishi amefanya mambo mengi kiasi hata pale Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Samia Suluhu Hassan alipoamua akamsaidie katika Wizara inayoshughulikia Michezo, Watumishi wengi walisikitika kwa namna alivyoweza kusikiliza na kushughulikia kero ambazo nyimngine hazikuhitaji fedha bali maamuzi tu. Wajumbe chagueni mtu huyu, CCM inahitaji watu kwa sasa wanaoweza kuwa wabunifu wa kujibu hoja za Wapinzani ambao baadhi yao ni Wasomi na wanauelewa.
4. Mohamed Omary Mchengerwa ni Msomi wa sheria, kwa namna Siasa za Tanzania na Dunia inavyoenda kwa sasa, Chama cha Mapinduzi kinahitaji kuwa na vijana wasomi wanaoweza kutetea hoja, kuelewa uchumi wa dunia, kuelewa nini Chama kinataka katika kukuza uchumi na kuweza kumsaidia Mwenyekiti wa Chama kutekeleza majukumu yake kiurahisi. Mohamed Omary Mchengerwa ni msomi ambaye anaweza kujenga hoja hata kwenye majukwaa ya Kimataifa, huyu ni msomii anayeweza kuzipangua hoja zote za Wapinzani bila kubabaika. Wajumbe huyu ndiye mtu sahihi wa kuwakilisha mkoa wetu wa Pwani.
Wajumbe, Kuna sababu nyingi sana za kusema juu ya kwanini Mohamed Omary Mchengerwa ndiye mgombea sahihi ya uwakilishi katika nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mkoa wa Pwani , itoshe kusema Mkoa wa Pwani unahitaji viongozi wa CCM watakaoutengeneza Mkoa from GOOD TO GREAT kwa kuweza kuisimamia Serikali vizuri ili kuwaletea Maendeleo Watanzania.
MUNGU IBARIKI TANZANIA,
MUNGU MBARIKI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SAMIA SULUHU HASSAN.