Kwa madada zangu wote wa mjini

belionea

JF-Expert Member
Mar 17, 2014
1,046
902
Jiepushe na wanaume za watu, onyesha heshima kwa wake zao. Ndoa ni taasisi iliyotengenezwa na Mungu mwenyewe tokea kuumbwa kwa misingi ya Dunia. Usiruhusu mwili wako utumike kuharibu ndoa ya watu.

Usiruhusu mwanamke mwenzako adondoshe chozi lake, alie na kujuta kwanini aliolewa hiyo ni laana kubwa. Najua maisha ni magumu na mnataka kitonga ila Haijalishi ni kiasi gani huyo mwanaume anakusaidia kimaisha, muepuke, sio wako. Tulia na wa kwako na Mungu wetu wa rehema atakubariki. "Karma is a bitch"- kuna wakati wa malipo!

Msije sema sikuwaambia!
 
1. Mpo wachache ndio sababu zenu
2. wanafahamu wana wake zao ndani kwanini wanawafata hao wanawake wengine????
3.
 
K-lyn angefata ushauri wako... sa hizi angekuwa anaendesha vits badili ya vogue!!! Ila ni ushauri mzuri
 
Kwani hiyo mume kasahau kwamba ameoa..ukute kamwambia hajaoa ndo maana bi dada kamkubali..

PIA Kuna ambao wanajua kabisa huyu Ni mume WA mtu lkn wanakomaa naye tu

lawama Ni kwa wote ke na me
 
NI DHAMBI MWANAUME KUWA NA MWANAMKE MMOJA
HATA Mungu hapendi
nahyo mwanamke anaedondosha chozi hyo mwanaume kamuumba?
siku ya mwisho sijui wanaume walio na mwanamke mmoja watajibu nini kwa Mungu ndo alichowatuma? ndo kazi aliyowapa kumtunza mwanamke mmoja tu?
ole wenu
 
Labda useme vibaya kuzini lakini oleweni hapo watakuelewa sanaaa tuu,na hao wanaume watafata kwa ridhaa zao au wanatiwa kamba kama mbuzi? wanakwenda huku wakiridhia,na wanawake wengine wanawatoa waume zao wenyewe
utamkuta mwanamke hana time na mumewe yeye kutwa na cm kutwa na harusi mara kigodoro,mara shogangu ana
tunzwa,chakula cha mume apike dada,nguo ya mume dada ndio anaijua ilipo sasa wewe uko uko nyumbani as what?
Na mume akienda nje ana enziwa tangua anaingia mpaka anatoka kwanini asiamishe kambi nje?
 
NI DHAMBI MWANAUME KUWA NA MWANAMKE MMOJA
HATA Mungu hapendi
nahyo mwanamke anaedondosha chozi hyo mwanaume kamuumba?
siku ya mwisho sijui wanaume walio na mwanamke mmoja watajibu nini kwa Mungu ndo alichowatuma? ndo kazi aliyowapa kumtunza mwanamke mmoja tu?
ole wenu

hahahahahahaha
 
NI DHAMBI MWANAUME KUWA NA MWANAMKE MMOJA
HATA Mungu hapendi
nahyo mwanamke anaedondosha chozi hyo mwanaume kamuumba?
siku ya mwisho sijui wanaume walio na mwanamke mmoja watajibu nini kwa Mungu ndo alichowatuma? ndo kazi aliyowapa kumtunza mwanamke mmoja tu?
ole wenu
hiyo dada haipo itakuwa ni u...m..a..l,.a...y..a sasa. Mm nna mke 1 tu na sijawahi kumcheat na wala sitegemei kucheat.
Mm ni mume wa mke 1 tu
 
Back
Top Bottom