Kwa ‘ Maandalizi ‘ haya mazuri tayari Taifa Stars imeshabeba Kombe la AFCON 2019 huko Egypt

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,865
Nianze kwa kutoa pongezi zangu za dhati kabisa kwa Watanzania wote Kuanzia kwa Serikali na hasa hasa TFF kwa kuiandaa vyema kabisa Timu yetu ya Taifa kiasi kwamba ‘ Maandalizi ‘ yake ya awali tu yamekuwa ni mazuri, yanatia matumaini kuliko hata Timu za Taifa za Majirani wetu Kenya na Uganda.

Wakati ‘ Maandalizi ‘ mazuri ya Taifa Stars yakiwa Boko na Uwanja wa Taifa huku Wachezaji wake muda mwingi tukipishana nao Mitaani na Vijiweni hadi maeneo ya Kula ‘ Bata ‘ wenzao wasiojua mpira na wabovu Timu ya Taifa ya Kenya ( Harambee Stars ) wao wapo Kambini sasa nchini Ufaransa huku Timu ya Taifa ya Uganda ( Uganda Cranes ) wao wakiwa Kambini huko Falme za Kiarabu.

Nichukue tu nafasi hii kuwaomba Watanzania wote tujiandae Kuipokea Timu yetu ya Taifa Stars pale itakaporudi na Kombe la AFCON 2019 huku tukiwa tumejazana Barabara zote za Jiji la Dar es Salaam kwani siyo Siri kwa ' Maandalizi ' haya mazuri na ya Kisayansi kabisa huku Wachezaji Wetu muda mwingi wakipiga ' Story ' Vyumbani na Koridoni pale White Sand Hotel na Mabinti wa Mjini kubadilishana Kuingia Vyumbani mwao ni hakika kama kuna mwaka ambao Tanzania kupitia Taifa Stars yetu tunaenda Kufurahi basi ni huu.

Hongereni sana Taifa Stars, Benchi la Ufundi na Shirikisho la Soka Tanzania ( TFF )

Nawasilisha.
 
Si mchawi tu kwamba kaonekana ila tayari tumechemka mapemaaaa...

Mkuu mbona tayari tumeshabeba hilo Kombe? Kwanini una wasiwasi? Wewe huoni wasiojua na ambao wala hawako ' Serious ' kabisa na AFCON 2019 akina Harambee Stars ya Kenya wameenda kupoteza muda kwa kuweka Kambi nchini Ufaransa na The Cranes nao kutoka Uganda nao wameenda Kupoteza muda kwa kuweka Kambi huko nchi ya Falme ya Kiarabu ( Abu Dhabi ) au United Arab Emirates?
 
Mbona unakata tamaa mapema aiseee
Sii unajua Taifa star ni Underdog mzeee watakuja kwa kutuzalau tutashinda inshaallah kuwa na imani
 
Tutajuta kushiriki afcon

Kwanini Mkuu wakati ' Maandalizi ' yetu ni ' Kabambe ' hata kuliko hao Majirani zetu wakubwa Kenya na Uganda? Wao wakiwa Kambini huko Ufaransa na Abu Dhabi Sisi Taifa Stars tupo Boko, Taifa na White Sand Jijini Dar es Salaam huku Wachezaji wetu wakionyesha Ushirikiano mzuri kabisa katika Mazoezi?
 
Kwanini Mkuu wakati ' Maandalizi ' yetu ni ' Kabambe ' hata kuliko hao Majirani zetu wakubwa Kenya na Uganda? Wao wakiwa Kambini huko Ufaransa na Abu Dhabi Sisi Taifa Stars tupo Boko, Taifa na White Sand Jijini Dar es Salaam huku Wachezaji wetu wakionyesha Ushirikiano mzuri kabisa katika Mazoezi?
Tutashughulikiwa kama chama la wana
 
Mbona unakata tamaa mapema aiseee
Sii unajua Taifa star ni Underdog mzeee watakuja kwa kutuzalau tutashinda inshaallah kuwa na imani

Wala sijakata Tamaa Mkuu ila Mimi nimewaonea mno Huruma hao Uganda na Kenya kwa kuweka Kambi zao huko UAE na Ufaransa wakati wabeba Kombe hili la AFCON 2019 kwa Mwaka huu Taifa Stars kutoka nchini Tanzania tumeweka Kambi yetu Wilaya ya Kinondoni hapa hapa Jijini Dar es Salaam huku tukiwa tunazunguka tu maeneo ya Boko na Uwanja wa Taifa kwa Mazoezi yetu asubuhi na jioni.
 
Tutashughulikiwa kama chama la wana

Usiwe na Hofu Mkuu kwani Timu iko vizuri kabisa na hata Wachezaji wake hadi mida ya Usiku huwa wanafanya Mazoezi yao mengine ya ' Kibaiolojia ' ambayo Kocha hakuwapa na Alfajiri wanarudi kwa ' Kujiiba ' Kambini ili waweze Kuendelea na ' Session ' ya Kocha Mkuu Amunike. Hapo White Sand Hotel sasa hivi kuna ' Warembo ' wengi tu wanapishana asubuhi na jioni na nadhani nao pia ni sehemu ya Kamati ya Ufundi ya Taifa Stars ili waweze kuwapa Mazoezi ' Maalum ' kabisa Wachezaji wetu ambao kwa sasa wanajiona wapo juu Kimpira na Kiuwezo hata kuliko akina Messi, Ronaldo na Salah.
 
usipo jiandaa kushinda jiandae kushindwa, kama ni kwel haya tunawashiriki.

Acha Uwoga Mkuu Ubingwa wa AFCON kwa 2019 Tanzania kupitia Taifa Stars yetu tunalibeba kwani ' Maandalizi ' yetu ni mazuri kupita maelezo kiasi kwamba hadi tumeyazidi ya nchi Jirani Uganda ambao wameenda zao Abu Dhabi ( UAE ) na Kenya ambao wameenda zao nchini Ufaransa kwa Kambi zao.
 
Nianze kwa kutoa pongezi zangu za dhati kabisa kwa Watanzania wote Kuanzia kwa Serikali na hasa hasa TFF kwa kuiandaa vyema kabisa Timu yetu ya Taifa kiasi kwamba ‘ Maandalizi ‘ yake ya awali tu yamekuwa ni mazuri, yanatia matumaini kuliko hata Timu za Taifa za Majirani wetu Kenya na Uganda.

Wakati ‘ Maandalizi ‘ mazuri ya Taifa Stars yakiwa Boko na Uwanja wa Taifa huku Wachezaji wake muda mwingi tukipishana nao Mitaani na Vijiweni hadi maeneo ya Kula ‘ Bata ‘ wenzao wasiojua mpira na wabovu Timu ya Taifa ya Kenya ( Harambee Stars ) wao wapo Kambini sasa nchini Ufaransa huku Timu ya Taifa ya Uganda ( Uganda Cranes ) wao wakiwa Kambini huko Falme za Kiarabu.

Nichukue tu nafasi hii kuwaomba Watanzania wote tujiandae Kuipokea Timu yetu ya Taifa Stars pale itakaporudi na Kombe la AFCON 2019 huku tukiwa tumejazana Barabara zote za Jiji la Dar es Salaam kwani siyo Siri kwa ' Maandalizi ' haya mazuri na ya Kisayansi kabisa huku Wachezaji Wetu muda mwingi wakipiga ' Story ' Vyumbani na Koridoni pale White Sand Hotel na Mabinti wa Mjini kubadilishana Kuingia Vyumbani mwao ni hakika kama kuna mwaka ambao Tanzania kupitia Taifa Stars yetu tunaenda Kufurahi basi ni huu.

Hongereni sana Taifa Stars, Benchi la Ufundi na Shirikisho la Soka Tanzania ( TFF )

Nawasilisha.
Naona unawananga kidizaini TFF.
 
D
Nianze kwa kutoa pongezi zangu za dhati kabisa kwa Watanzania wote Kuanzia kwa Serikali na hasa hasa TFF kwa kuiandaa vyema kabisa Timu yetu ya Taifa kiasi kwamba ‘ Maandalizi ‘ yake ya awali tu yamekuwa ni mazuri, yanatia matumaini kuliko hata Timu za Taifa za Majirani wetu Kenya na Uganda.

Wakati ‘ Maandalizi ‘ mazuri ya Taifa Stars yakiwa Boko na Uwanja wa Taifa huku Wachezaji wake muda mwingi tukipishana nao Mitaani na Vijiweni hadi maeneo ya Kula ‘ Bata ‘ wenzao wasiojua mpira na wabovu Timu ya Taifa ya Kenya ( Harambee Stars ) wao wapo Kambini sasa nchini Ufaransa huku Timu ya Taifa ya Uganda ( Uganda Cranes ) wao wakiwa Kambini huko Falme za Kiarabu.

Nichukue tu nafasi hii kuwaomba Watanzania wote tujiandae Kuipokea Timu yetu ya Taifa Stars pale itakaporudi na Kombe la AFCON 2019 huku tukiwa tumejazana Barabara zote za Jiji la Dar es Salaam kwani siyo Siri kwa ' Maandalizi ' haya mazuri na ya Kisayansi kabisa huku Wachezaji Wetu muda mwingi wakipiga ' Story ' Vyumbani na Koridoni pale White Sand Hotel na Mabinti wa Mjini kubadilishana Kuingia Vyumbani mwao ni hakika kama kuna mwaka ambao Tanzania kupitia Taifa Stars yetu tunaenda Kufurahi basi ni huu.

Hongereni sana Taifa Stars, Benchi la Ufundi na Shirikisho la Soka Tanzania ( TFF )

Nawasilisha.

Mkubwa sie kukanyagaa Misri tu tayari ni over and above targets na sherehe zinaendelea tumemaliza za futari sasa wachezaji kupewa mitaa DAB ameanza na keptenyo Diego, sherehe katika media ni kutafuta nani anaenda kushangilia nani anasubiri luninga Pierre tayari anayo ticket.

Pongezi nyingi kwa serikali na mzee baba, Kenya wao serikali ilisema watakaowakilisha taifa lao serikali itabeba gharama huku tunasubiri events labda DAB anamihela atatoa manake sponsors wanapumulia mashine kama sie tu manake kambi yenyewe Patel amejitolea sijui logos wanazovaa hela kapokea nani.

Kudos Genta kwa kutuandaa kisaikolojia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom