Kwa kweli wakati mwingine maisha ni ufala sana

Mzee mbona umetolea mfano wa stress za watu kundi la wavuta bhangi na watumiaji wa dawa za kulevya?
Yote uliyoyaandika yana mantiki ya msingi lakini hayana conclusion.
Umetamani kusafiri kukutana na marafiki zako, utasafirije bila pesa?
Mifano hiyo michache lakini ipo mingi sana katika maisha ambayo kuipata furaha yako mpaka uigharamie.
Hawa unaowaita waathirika pia walitumia pesa zao kununua sleeping pills, pain killers nk, kujipatia usingizi na kujisikia vizuri, na ghafla walijikuta kuwa hawawezi kushinda bila ya madawa!!!
Hujawahi kusikia kwamba mbuzi hula kulingana na urefu wa kamba yake!!! Watu wasiokuwa na pesa huwa wanatafuta furaha zao kwenye simple things zinazoendana na hadhi yao. Wahenga wameshasema "tamaa nyingi, mbele giza!" Nani hapa kwetu amesikia kuhusu caviar, chakula cha matajiri??! Hatujasikia kwa sababu haina uhalisia na maisha zetu. Maskini amejifundisha kufarahia ugali na mchicha, bora ushibe kuliko kushinda na njaa, huku ukiwaza biryani! Ukiishi kwa tamaa inayozidi kipato chako, unajiweka wazi kwa mambo kama rushwa, uwizi, uporaji nk!!
Halafu, angalia takwimu ya suicide rates duniani - nchi tajiri kama Sweden, South Korea, Japan ndio wanaongoza na hali imekuwa mbaya mpaka imetangazwa janga nchini mwao. Sasa jiulize, kwa nini kwenye nchi tajiri inazowapatia kila aina ya huduma kuanzia cradle to the grave, bado raia hawaoni furaha ya kuishi na wanaamua kujiua??!!
Pesa si kitu ya kudharau, lakini kuna vitu vingi - upendo, urafiki, afya, hekima, nk ukizinunua utagundua ni feki!!!! Ni vitu ambazo ni majaliwa ya Mungu na ndizo zinaongeza furaha kwenye maisha. Kama pesa ingekuwa kila kitu, basi kwa nini tunasema "Mungu akuongezee baraka" badala ya "Mungu akuongezee pesa" na "Ubarikiwe Sana!!" badala ya "Utajirike Sana!!"???
 
Pacha, unalala njaa, unakula mlo mmoja, mwenye nyumba kila asubuhi anakugongea kukusomea risala utasema umeridhika? Basi wenzetu mna roho nzuri
Kuna tofauti kati ya mtu asie na pesa na fukara. Unamzungumzia wewe ni fukara. Mimi sina pesa na nina furaha sana na maisha yangu.
 
Ni vigumu mno kuridhika katika limbwi la ufukara… amini usiamini ndoto (mawazo matamanio) ya binadamu karibia wote ni kupiga mkwanja mrefu wale raha.. Sasa kama miaka inasonga tu goma halisomeki leo bora ya jana unaridhikaje mkuu? Hapo ukipita maeneo eneo unakuta watu wanasukuma mikoko ya hatari mno…
Mimi sio fukara,sio tajiri. Huwezi kuniweka kwenye kundi la wenye pesa ila nayafurahia sana maisha yangu. Kifupi I'm very happy. Na point yangu haikuzungumzia fukara. Sio kila asie na pesa ni fukara. Mimi sina pesa but I'm very happy with my life. Sio lazima ukubaliane na mimi kila MTU ana mtazamo wake
 
Mimi sio fukara,sio tajiri. Huwezi kuniweka kwenye kundi la wenye pesa ila nayafurahia sana maisha yangu. Kifupi I'm very happy. Na point yangu haikuzungumzia fukara. Sio kila asie na pesa ni fukara. Mimi sina pesa but I'm very happy with my life. Sio lazima ukubaliane na mimi kila MTU ana mtazamo wake
ni mtizamo wangu mkuu si wako..sijakubaliana na wako..nadhani ndo maana ya demokrasia hiyo
 
Tunakua sawa ila vp mfano wewe n baba wa watoto watatu hata la saba hawajamaliza unakufa unawaacha kwenye nyumba ya kupanga wanalalia makusheni ya kupewa na mwenye nyumba. Sijui n uchungu gani utaupata utakapokua kweny hatua za mwisho kukata roho najua lazma utasema wanangu nawaacha mkiwa wadogo bila chochote cha kurithi mtaishi kwa shida na mateso ila msijali Mungu yupo atawasaidia ishini naisha ya kumpendeza Mungu siku moja tutaonana. Sikuunakata roho tu kale kabinti kako kakubwa kanaingizwa ukubwani rasmi ili kamudu kuwatunza wadogo zake. Sasa hapo maisha ya kumpendeza shetani ndio yanaanza.

Acheni wivu na kukariri misemo isiyo na tija eti sote tutakufa, ukifa huzikwi na gari wala ndani ya nyumba yako eti unazikwa nje!! Sawa tajiri atazikwa nje na masikini nje ila jiulize je, tajiri kafa kawaachia nini wanawe? Masikini nae je kawaachaje wapendwa wake? Kama ni faida kuishi kwenye ufukara endelea kupiga uvivu.
umetoa kamfano tu ila nimekasoma nikavuta picha,nimejikuta naskia uchungu sana..Tutafute Pesa nothing else.
 
Mungu ametupa utajiri ili iwe ni kama mtihani kwako,ndio maana kwa mfano,kwa waislamu kuna kitu kinaitwa ZAKA,hii hutolewa kila mwaka 10% (kama sijakosea) ya mali yako unasaidia masikini,je kama matajiri wote wangefuata hii,tungekua na watu wanaokufa kwa kukosa chakula?

Mungu humpa mtu utajiri ili iwe kama mtihani kwake,Labda cha kujiuliza hapa,lengo la maisha ni nini? kwa upande wa dini ni kumtumikia Mungu,na kumtumikia Mungu si kusali tuu,bali yapo mambo mengine ya kiibada kama vile kutoa zaka/kusaidia masikini,tajiri unapomuona masikini anateseka,unatakiwa umshukuru Mungu kwa neema alizokujaalia kisha umsaidie huyo masikini,hakuna kitu kinacholeta amani ya moyo/furaha kama unapomsaidia mtu jambo ambalo ni gumu kwake,

One Love
 
Mimi sio fukara,sio tajiri. Huwezi kuniweka kwenye kundi la wenye pesa ila nayafurahia sana maisha yangu. Kifupi I'm very happy. Na point yangu haikuzungumzia fukara. Sio kila asie na pesa ni fukara. Mimi sina pesa but I'm very happy with my life. Sio lazima ukubaliane na mimi kila MTU ana mtazamo wake
Mkuu, nakupongeza kuwa na ATTITUDE NZURI. Ni attitude ndiyo inayofanya mtu kufaulu au kufeli maishani. Kuwa na attitude ya shukrani, ya kutosheka na ya kuridhika, ni neema kubwa kuliko zote duniani. Ubarikiwe sana!
 
Tatizo la watu/maskini wengi wanadhani wapo kwenye hali hiyo kwa kusababishiwa na matajiri au wenye uwezo. Ni mawazo mgando sana.
Leo hii wape watanzania wote milioni kumi kila mmoja baada ya mwaka mmoja wafuate nakuhakikishia 90% utawakuta hawana hata senti tano na 5% pekee utakuta bado wanazofedha na wamezalisha Zaidi.
Tatizo kubwa la umaskini sio Mungu, sio Serikali, Sio chama chochote, wala sio kupanda wala kushuka kwa uchumi. Tatizo Binadamu(mtanzania) ameshindwa kutumia Mawazo(akili) yake, Nguvu zake, Hisia(emotion)chanya zake na mwili wake kutatua changamoto zake.
Mtaji wa mafanikio yako ni uhai peke yake. Acha kuwaza msaada/ufadhili wa bure, waza kufanya kazi yyt kwa kuanzia upate pa kuanzia hata kama kufagia barabara. Ishi kulingana na hali yako kula kulingana na kipato chako. Jieleze matatizo yako au mahitaji yako utasaidiwa kupata kazi.
Unasubiri kuonewa huruma mtu mzima una viungo vyote salama. Wanaokula chakula cha laki moja wametafuta fedha zao miaka mingi kwa jasho, wakati wenzio wanaamka saa 11 asubuhi ww unaamka saa 4 asubuhi. ana haki ya kwenda kutibiwa mafua uingereza, usion wivu, usiwe mvivu
Maisha yako yapo mikononi mwako, ww ndio utaamua kama yaweje. kwa kukusaidia amini usiamini ukivipangilia vizuri vipaji hivi ambavyo naamini kila mtu anavyo utafanikiwa kila utakacho fanya.
Your mind
Your body
Your Enegy
Your Emotion
ujieleze tu utapata kazi? Na hizo kazi zozote unazozungumzia watu wanatafuta na hawapati.tukubali maisha ni kama kiganja cha mkono hatuwezi kuwa sawa hata iweje.
 
Kuna tofauti kati ya mtu asie na pesa na fukara. Unamzungumzia wewe ni fukara. Mimi sina pesa na nina furaha sana na maisha yangu.
Sasa ufukara si maana yake huna pesa? Kwani fukara ni mtu asiye na wazazi?
 
Back
Top Bottom