Kwa kweli tuchukue tahadhari, huyu ni "malaika" asiye na huruma wala mzaha toka kitambo

Kwa uandishi wa makala unastahili 100% MARKS, ila kuhusu uhalisia wa ulichoongea sijui tukupe ngapi?.Namaanisha tukiorodhesha madhambi ya maraisi wote watano waliotangulia kabla ya awamu hii madhambi yao kabla hawajawa Wakuu wa nchi hii, kiukweli wa sasa hivi anaweza kuwa MALAIKA kweli vinginevyo ujifanye hujui. Kwenye zile mada zinazohusu mambo ya ndege na maswala ya anga ndo huwa unaongea ukweli tupu na kwa ile knowledge unayoonyeshaga hapa inaonekana wewe ni msafiri unayejua yanayoendelea ulimwenguni. Ulivyoelezea hapa leo ni as if Tanzania ya leo tupo Reo De Janeiro, Johannesburgh ,Columbia, California na miji mingine ambayo kwa siku ni kawaida wastani wa watu 6 hadi 8 hupigwa risasi au kupotea kila siku iendayo kwa Mungu. JPM sio Mungu ana madhaifu yake ila hali halisi na hali mnayojaribu kuonyesha kwenye mitandao ni vitu viwili tofauti. Watu wanaendelea na maisha yao mitaani kama kawaida huku mitandaoni mkijitahidi kuelezea kama vile mnakufa usiku huu huu. Hakuna mtu anayepotea tu bila sababu, hata uswahilini watu wanapotea kwa kupotezana baada ya kudhulumiana pesa, kufumaniana au sababu zipo nyingi.Wengine waweza kuwa wanapotezwa na system kama unavyosema ila narudia hakuna mtu anapotea tu, lazima kuna kitu kakifanya.. Wewe mbona hujapotea upo hapa unabwabwaja maneno kibao ukiwa huru?, ni kwasababu umelelewa kwa nidhamu na unajua mipaka yako ndo maana hata kwenye huu uzi wako pamoja na maelezo yote bado umezingatia nidhamu,hujamtukana kiongozi yoyote wala kumkwaza mtu, ila upo hapa unatetea walopokaji hovyo huku ukieleza maelezo kibaoo eti hatupo salama???... Ni kama yule jamaa yenu jana alikuwa BBC.. ana akili nyingi za darasani lakini kuna elimu inaitwa ELIMU DUNIA, kichwani mwake ni 00% ndo maana dunia inamfundisha ukubwani.Atazunguka duniani koote mwisho wa siku atarudi nyumbani na atajiona mjinga tu.Ila kanuni za kidunia zipo na zinafanya kazi. Na kuna kitu anaendelea kukitafuta muda sio mrefu atakipata iwe nchini au hukohuko aliko.Nimalize kwa kukwambia TANZANIA bado ni mahali salama sana,tena zamu hii hata zile bunduki ndogo kwa kubwa ndugu zetu walikuwa wakionyeshwa ili watoe hata laki 2 mapema kweupe kwenye mabanda ya tigopesa siku hizi zimepotezwa kabisa, hadi wale wanasiasa waongo waongo wapo bize majimboni. Endeleeni kuimba nyimbo za uongo ila TUKUTANE 2020 ndo utajua kama JPM anapendwa na wananchi wake au LA.Mkuu BARAFU hizi CHEAP(politics) propaganda waachie akina SALARY SLP & CO.LTD,. wewe uelewa wako ni mpana zaidi ya hapo.Ni hayo tu.

Kwa kuwa mligawana 1.5 trilion unakuja na utetezi kuwa mfalme kawa malaika.Rubbish
 
Mmh amefanya vibaya kuandika mtazamo wake!?

Jr
Kwa mtu kama yeye nilitegemea angewasilisha kwa lugha ya staha, ila kwa vijana wa dot com nisingetia neno. Bado naamini kwa mtizamo wangu wa kipumbavu na ukosefu wa wakili wangu kuwa AMEPOTOKA.
 
Huyu mtu ni hatari sana!

Ni mtu popular kwa watu wenye sifa hizi:
1.Wenye uwezo mdogo wa kuona mbali
2.Wasiotazama mbali
3.Wenye uwezo mdogo wa kumsoma mtu
4.Wanaodanganyika na kupumbazwa na vitu vya kuonekana machoni
5.Wavivu wa kufikiri na wenye uwezo mdogo wa kupima kauli na matendo ya mtu.
6.Wanaoabudu watu kwa wadhifa au cheo na hawatazami matendo na dhamira ya muhisika.
7.Watu ambao sio wafuatiliaji wa mambo

Hawa watu wakuja kuelewa when it is already too late huku baadhi yao nao wakiwa teyari ni wahanga.
Wengine wana uelewa ila wamejivua huo ili wapate pa kupenya. Wakati malaika anatangaza watu wafyatue wanavyoweza, waziri wa afya si alikuwepo na akashangilia wakati ndiye ofisi yake inaomba msaada wa njiti na family palanning pills?

Watu wanaopotezwa ina maana polisi hawajui au ndo malaika kasema kimyaaaaa!
 
Kwa mtu kama yeye nilitegemea angewasilisha kwa lugha ya staha, ila kwa vijana wa dot com nisingetia neno. Bado naamini kwa mtizamo wangu wa kipumbavu na ukosefu wa wakili wangu kuwa AMEPOTOKA.
Naheshimu mawazo yako,kama ambavyo ungeweza kuvumilia yangu.Kusudi letu ni moja kufikia Tanzania tunayoipenda.Lugha hutegemea hadhira na wakati.
 
Naheshimu mawazo yako,kama ambavyo ungeweza kuvumilia yangu.Kusudi letu ni moja kufikia Tanzania tunayoipenda.Lugha hutegemea hadhira na wakati.
Sawa mkuu, humu JF ni wachache wenye ukomavu wa kifikra, hata walio wengi ni watu wazima ingawa mihemko imewatawala kutokana na kuwa wanaharakati. Bado wewe nakuweka katika kundi la wajengao hoja maridhawa. Naomba unikubalie mtizamo wangu katika andiko lako ingawa comment yako nakubaliana nayo kwa vile ulikuwa nie na uliporudi mambo yakawa ndivyo sivyo. Ukikaa nchini kwa muda utakubaliana nami kuwa pamoja na mapungufu alonayo, JPM anasimamia ya kesho kwa kutoangalia ya leo. Yeye anahangaika na mbegu za kupanda wakati tupo katika msimu wa njaa. Nina imani wakati wa mavuno tutamsifia kwani mwanadamu ameumbwa kusahau. Uwe na siku njema yenye baraka tele. Nyumbani kutanoga baada ya umeme na reli kukamilika
 
Naheshimu mawazo yako,heshimu na ya mwingine pia.Jikite katika kufanya utafiti tu hata mdogo juu ya hali ya Chuki na mawazo ya watu.Achana na haya tunayoita maendeleo.

Angalia maendeleo yanayoambatana na furaha na upendo katikati ya watu wanaoyapokea.Mfano wako wa hayo majiji haustahili...Maana sisi na wao si utamaduni mmoja.Sisi hakuzoea hayo,lkn sasa imekuwa kawaida,tulizoea vifo vya kuhusishwa na ugomvi wa ulevi na wivu wa mapenzi,sio vifo vya chuki za kisiasa na kisasi.

Fanya kautafiti kama kangu,panda usafiri wa umma katika maeneo niliyoorodhesha hapo juu,jifanye wewe ni kama wao,usikie mitazamo na hisia za watu.

Hoja si maendeleo na ushindi wa kurudi Ikulu 2020,hata mie ninajua mwakani Ikulu atarudi aliyepo,na bunge 98%itakuwa ni chama dola.

Kwetu sisi,uchambuzi wa ndege na anga si lolote,kama jamii ya watoto na ndugu zetu,na mahali tunapotegemea kuzikwa,kumetawaliwa na chuki inayopandwa sbb ya tofauti ya itikadi na mtazamo.
Unawashauri nini watanzania ili waepukane na kadhia unayoisema/iliyopo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo la muda ni kweli lakini si shida ya usafiri.
Mahali pa saa unasafiri kwa saa 2:30 sio tatizo kwako. Foleni sio shida kwani. Hata bei itashuka kwani mafuta yaliyokuwa yakitumika kwenye foleni burebure yatatumika kwenye Mwendo. Njia name si mchezo kusimamia hiari yako
 
Huyu mtu ni hatari sana!

Ni mtu popular kwa watu wenye sifa hizi:
1.Wenye uwezo mdogo wa kuona mbali
2.Wasiotazama mbali
3.Wenye uwezo mdogo wa kumsoma mtu
4.Wanaodanganyika na kupumbazwa na vitu vya kuonekana machoni
5.Wavivu wa kufikiri na wenye uwezo mdogo wa kupima kauli na matendo ya mtu.
6.Wanaoabudu watu kwa wadhifa au cheo na hawatazami matendo na dhamira ya muhisika.
7.Watu ambao sio wafuatiliaji wa mambo

Hawa watu wakuja kuelewa when it is already too late huku baadhi yao nao wakiwa teyari ni wahanga.

Kitabu kitakatifu cha Wakristu yaani BIBLIA kimewajumuisha aina ya watu wenye sifa hizo na kusema:

''WATU WANGU WANA ANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA'' Hosea 4:6
 
Kwa taarifa yako barafu ana weledi haokotezi mambo ya mtaani. Huyu ni member mwenye heshima hapa jukwaani, alichosema ndio hicho kilichopo.

Ni nani ambaye hasafiri kwenye vyombo vya usafiri akajionea anayohadithia hapa!!!???au nyinyi wenzetu mnaishi dar nyingine!!!
 
Kwa uandishi wa makala unastahili 100% MARKS, ila kuhusu uhalisia wa ulichoongea sijui tukupe ngapi?.Namaanisha tukiorodhesha madhambi ya maraisi wote watano waliotangulia kabla ya awamu hii madhambi yao kabla hawajawa Wakuu wa nchi hii, kiukweli wa sasa hivi anaweza kuwa MALAIKA kweli vinginevyo ujifanye hujui. Kwenye zile mada zinazohusu mambo ya ndege na maswala ya anga ndo huwa unaongea ukweli tupu na kwa ile knowledge unayoonyeshaga hapa inaonekana wewe ni msafiri unayejua yanayoendelea ulimwenguni. Ulivyoelezea hapa leo ni as if Tanzania ya leo tupo Reo De Janeiro, Johannesburgh ,Columbia, California na miji mingine ambayo kwa siku ni kawaida wastani wa watu 6 hadi 8 hupigwa risasi au kupotea kila siku iendayo kwa Mungu. JPM sio Mungu ana madhaifu yake ila hali halisi na hali mnayojaribu kuonyesha kwenye mitandao ni vitu viwili tofauti. Watu wanaendelea na maisha yao mitaani kama kawaida huku mitandaoni mkijitahidi kuelezea kama vile mnakufa usiku huu huu. Hakuna mtu anayepotea tu bila sababu, hata uswahilini watu wanapotea kwa kupotezana baada ya kudhulumiana pesa, kufumaniana au sababu zipo nyingi.Wengine waweza kuwa wanapotezwa na system kama unavyosema ila narudia hakuna mtu anapotea tu, lazima kuna kitu kakifanya.. Wewe mbona hujapotea upo hapa unabwabwaja maneno kibao ukiwa huru?, ni kwasababu umelelewa kwa nidhamu na unajua mipaka yako ndo maana hata kwenye huu uzi wako pamoja na maelezo yote bado umezingatia nidhamu,hujamtukana kiongozi yoyote wala kumkwaza mtu, ila upo hapa unatetea walopokaji hovyo huku ukieleza maelezo kibaoo eti hatupo salama???... Ni kama yule jamaa yenu jana alikuwa BBC.. ana akili nyingi za darasani lakini kuna elimu inaitwa ELIMU DUNIA, kichwani mwake ni 00% ndo maana dunia inamfundisha ukubwani.Atazunguka duniani koote mwisho wa siku atarudi nyumbani na atajiona mjinga tu.Ila kanuni za kidunia zipo na zinafanya kazi. Na kuna kitu anaendelea kukitafuta muda sio mrefu atakipata iwe nchini au hukohuko aliko.Nimalize kwa kukwambia TANZANIA bado ni mahali salama sana,tena zamu hii hata zile bunduki ndogo kwa kubwa ndugu zetu walikuwa wakionyeshwa ili watoe hata laki 2 mapema kweupe kwenye mabanda ya tigopesa siku hizi zimepotezwa kabisa, hadi wale wanasiasa waongo waongo wapo bize majimboni. Endeleeni kuimba nyimbo za uongo ila TUKUTANE 2020 ndo utajua kama JPM anapendwa na wananchi wake au LA.Mkuu BARAFU hizi CHEAP(politics) propaganda waachie akina SALARY SLP & CO.LTD,. wewe uelewa wako ni mpana zaidi ya hapo.Ni hayo tu.
Kumbe bado mnaendelea na mipango ya Kummaliza?


Uzuri karibu wote wenye vinasaba na wasiojulikana hilo mnalikiri hadharani.


Cha kushukuru zaidi ni kwamba hata ninyi tunaishi wote katika ulimwengu huu huu hamna maduka yenu maalum wala masoko maalum so itafika point itakua ni tit for tat..


Endeleeni kudhani kwamba ninyi mna pumzi yenu maalum.
 
Tuombe Mungu,labda tutarudi njia kuu

Inshallah na Ameen...!!!
Hakika Mungu atasikia kilio cha Watanzania kutokana na manyanyaso haya...!
Leo Kiongozi wa KUB Mhe. Mbowe anamaliza miezi takribani 2 mahabusu kwa kesi isiyo na kichwa wala miguu...!!This is very sad...inasikitisha, inauma na inaudhi kupita maelezo....Hakika Mungu anaona na atawalipa hawa Makaburu wa Kitanzania kile kinachostahili kwa wakti wake...Amina.
 
Ni kweli tulipenda kumpa ukuu wa himaya,na wengine hatukulala,usiku na mchana,maana tuliona ni ufadhali huyu kuliko yule mwenye unga kichwani.Tulijipa matumaini nankuchukua hatari kama kucheza bahati nasibu.Lakini,hapana,hakuna maendeleo bila amani na upendo,hakuna maendeleo yenye raha katikati ya chuki na visasi,maendeleo ndani ya zimwi la husuda na machozi ni sawa na nyumba nzuri yenye giza wakati wa mwanga.
Haya ni maneno yanayoonyesha Majuto? Au kutotimia malengo?
 
Back
Top Bottom