Kwa kweli tuchukue tahadhari, huyu ni "malaika" asiye na huruma wala mzaha toka kitambo

Kwa uandishi wa makala unastahili 100% MARKS, ila kuhusu uhalisia wa ulichoongea sijui tukupe ngapi?.

Namaanisha tukiorodhesha madhambi ya maraisi wote watano waliotangulia kabla ya awamu hii madhambi yao kabla hawajawa Wakuu wa nchi hii, kiukweli wa sasa hivi anaweza kuwa MALAIKA kweli vinginevyo ujifanye hujui.

Kwenye zile mada zinazohusu mambo ya ndege na maswala ya anga ndo huwa unaongea ukweli tupu na kwa ile knowledge unayoonyeshaga hapa inaonekana wewe ni msafiri unayejua yanayoendelea ulimwenguni. Ulivyoelezea hapa leo ni as if Tanzania ya leo tupo Reo De Janeiro, Johannesburgh ,Columbia, California na miji mingine ambayo kwa siku ni kawaida wastani wa watu 6 hadi 8 hupigwa risasi au kupotea kila siku iendayo kwa Mungu.

JPM sio Mungu ana madhaifu yake ila hali halisi na hali mnayojaribu kuonyesha kwenye mitandao ni vitu viwili tofauti. Watu wanaendelea na maisha yao mitaani kama kawaida huku mitandaoni mkijitahidi kuelezea kama vile mnakufa usiku huu huu. Hakuna mtu anayepotea tu bila sababu, hata uswahilini watu wanapotea kwa kupotezana baada ya kudhulumiana pesa, kufumaniana au sababu zipo nyingi. Wengine waweza kuwa wanapotezwa na system kama unavyosema ila narudia hakuna mtu anapotea tu, lazima kuna kitu kakifanya.. Wewe mbona hujapotea upo hapa unabwabwaja maneno kibao ukiwa huru?, ni kwasababu umelelewa kwa nidhamu na unajua mipaka yako ndo maana hata kwenye huu uzi wako pamoja na maelezo yote bado umezingatia nidhamu,hujamtukana kiongozi yoyote wala kumkwaza mtu, ila upo hapa unatetea walopokaji hovyo huku ukieleza maelezo kibaoo eti hatupo salama???...

Ni kama yule jamaa yenu jana alikuwa BBC.. ana akili nyingi za darasani lakini kuna elimu inaitwa ELIMU DUNIA, kichwani mwake ni 00% ndo maana dunia inamfundisha ukubwani.Atazunguka duniani koote mwisho wa siku atarudi nyumbani na atajiona mjinga tu.Ila kanuni za kidunia zipo na zinafanya kazi. Na kuna kitu anaendelea kukitafuta muda sio mrefu atakipata iwe nchini au hukohuko aliko.

Nimalize kwa kukwambia TANZANIA bado ni mahali salama sana,tena zamu hii hata zile bunduki ndogo kwa kubwa ndugu zetu walikuwa wakionyeshwa ili watoe hata laki 2 mapema kweupe kwenye mabanda ya tigopesa siku hizi zimepotezwa kabisa, hadi wale wanasiasa waongo waongo wapo bize majimboni.

Endeleeni kuimba nyimbo za uongo ila TUKUTANE 2020 ndo utajua kama JPM anapendwa na wananchi wake au LA.

Mkuu BARAFU hizi CHEAP(politics) propaganda waachie akina SALARY SLP & CO.LTD,. wewe uelewa wako ni mpana zaidi ya hapo.Ni hayo tu.
Umeanza lini uji.nga?au wewe in tiss feki??
 
Huyu mtu ni hatari sana!

Ni mtu popular kwa watu wenye sifa hizi:
1.Wenye uwezo mdogo wa kuona mbali
2.Wasiotazama mbali
3.Wenye uwezo mdogo wa kumsoma mtu
4.Wanaodanganyika na kupumbazwa na vitu vya kuonekana machoni
5.Wavivu wa kufikiri na wenye uwezo mdogo wa kupima kauli na matendo ya mtu.
6.Wanaoabudu watu kwa wadhifa au cheo na hawatazami matendo na dhamira ya muhisika.
7.Watu ambao sio wafuatiliaji wa mambo

Hawa watu wakuja kuelewa when it is already too late huku baadhi yao nao wakiwa teyari ni wahanga.
Umeongea vyema

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Mkubwa sana,hii siyo Mama Tanzania niliyokulia na kuishi.

Kuna mabadiliko makubwa sana ya kihisia katikati ya jamii na wanajamii.Kuna kakitu fulani ka chuki na tuhuma za chuki zinajengeka.

Kwa miaka mitatu niliyokuwa mbali,mabadiliko ni makubwa sana katikati ya watu wengi.

Usiishie kwenye gari binafsi,jipe muda na recorder yako,panda Mwendo Kasi ya jioni toka K'koo mpaka Kimara,rudi nayo Kkoo,panda kesho yake daladala za Kkoo-G'Mboto,tena panda Kkoo-Tandika...malizia na Kkoo Tegeta.Utapata hisia halisi ya Watanzani,kama una hulka ya utafiti,utarudi hapa na kusema bila unafiki.
Naam

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Ha ha haaa...kitakachofanyika siku yakutua LISU ataokotwa Airport kukutanishwa na Joka lenye njaa....kitu watu tunatakiwa kujua waliomchagua huyu bwana na wapuuzi wanaomshangilia wanaboa hii Nch kumbuka hata ikitokea bahati mbaya akaondoka mamlakani atatuachia watu hatari sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu alimsaidia yuko salama na anampa jiwe wakati mgumu

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom