barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Huyu ni mtu mwenye kisasi na roho ngumu sana.Amekunywa damu ya mwana wa Saa8 na yule "SHIHATA" wa Kibiti.Hii imekuwa tabia yake,hajatosheka na kiwango cha bilauli za damu alizokwisha chota na kunywa.
Raha yake ilikuwa apate bilauli ya damu ya Lissu juu ya meza yake,ili anywe na kusuuzika roho,bahati mbaya damu ile imekuwa ngumu kuipata,ngamia amegoma kupiga goti ili achinjwe,sasa anataka kumchinja ngamia kwa shuruti,yupo radhi kunywa damu chungu ya ngamia inayotokana na ngamia kugoma kuchinjwa.Huyu ni mnywa damu,hajaanza jana wala juzi.Alianza na damu za familia,sasa amehamia kwenye damu za walio nje ya familia.
Mwaka 2005,Kaskazini Magharibi mwa Tanganyika,jimbo la Ziwa(LakeProvince),Mkoa wa Ziwa Magharibi (West-Lake Region)aligombea na kijana toka chama cha Upinzani.Aliona tishio la yeye kupata upinzani,yeye huwa hapendi kukosolewa wala kupigwa,ni mpenda sifa,hujiona kama malaika.Msifie utakuwa wake,mkosoe upasuliwe.Hii ni hulka yake iliyo ndani ya damu.
Hajaanza jana wala leo,2005 hakutaka tabu,alimtumia watu mgombea wa chama cha pili,akaagiza asafirishwe mpaka Makao Makuu ya Nyanza Province,pale akakatiwa tiketi ya Community Airline,wakati huo ipo juu ya ramani zaidi ya Kasuku aliyefurushwa kumpisha Twiga,breki ya kwanza ikawa bandari ya Salama,na moja kwa moja mpaka JB Belmond wakati huo.
Pale alihudumiwa kila kitu,kwa mpango kuwa aachie nafasi kupunguza ushindani,na hakika kwa zawadi ya kutunukiwa cheo kwa wakati ufaao.Huduma zote zilitoka kwa "Malaika",mkuu wa "watakatifu" na "wenyeheri" wasio na mawaa.Kipindi hicho makao ya "malaika" yalikuwa jengo moja na Kibubu cha Ushirika na Maendeleo Vijijini,mkabala na Mkaguzi na Kituo cha kujua lugha ya Hard-Talk ya Steve,pale kwenye jina la "God Made the World,The Dutch Made Holland".
Baada ya mchakato wa tume kupita,na "malaika" kuchukua ushindi wa team kutokufika uwanjani,walituma maafisa wa "kukodi" wa wakati huo Physics,Chemistry na Biology kabla ya kuongezewa C moja katikati,"Malaika" akamtengenezea mchezo mgombea kuwa anamuomba mlungula ili amuachie nafasi ya ukuu wa kitalu.
Hii ni baada ya kupita siku tatu,"malaika" anapigiwa simu bila kupokea maana alishamaliza kazi yake ya kupita bila kuwa na kizuizi cha ukuu wake.Kwa hiyo,huyu ni "malaika" ambaye hutumia mbinu zote ili kuhakikisha anadumisha ukuu wake,wakati akiwa bila majeshi ya mbingu na ardhi,alitumia nafasi na dinari,huyu hawezi kubadili hulka,iwe kwa fimbo au kwa rungu.
Ni aina ya "malaika" wasiotaka kugusika,ana sifa,kiburi na roho mbaya inayojificha katikati ya maneno ya uwongo na lugha za kutaka kuonekana ni wa watu wa chini.Ni hulka ya kisaikolojia mtu wa chini kuona anaambiwa anapendwa kuliko tajiri.Ni tabia za masikini wote duniani,masikini hupenda faraja tupu isiyo na mkakati,tajiri hupenda mkakati usio na faraja,ndio maana wale "interepirinuwaa" walikuja na msemo wakasema "An Interpreneur is a risk taker".
Ni kweli tulipenda kumpa ukuu wa himaya,na wengine hatukulala,usiku na mchana,maana tuliona ni ufadhali huyu kuliko yule mwenye unga kichwani.Tulijipa matumaini nankuchukua hatari kama kucheza bahati nasibu.Lakini,hapana,hakuna maendeleo bila amani na upendo,hakuna maendeleo yenye raha katikati ya chuki na visasi,maendeleo ndani ya zimwi la husuda na machozi ni sawa na nyumba nzuri yenye giza wakati wa mwanga.
Tunapokwenda ni mbali,sio tena salama kwa vizazi vyetu vijavyo.Mchonga alisurubu ndio,lakini hakufika huko,Mzee wa pwani alikuwa swala 5 sana,mengi alisema hewala,nitamaliza na kuondoka,Chinga mwanzo wake alikuwa muoga na kauli na jicho la mchonga,alipofukiwa Mchonga akakosa washauri,akaangukia kwa ambao mpaka kesho anawasikitikia.Handsome wetu hata wale wa mfumo walipomsaidia bila kumpa taarifa,aliwaambia waacheni hao,watasema watachok.Huyu "Malaika" anaagiza na kuomba kikombe na yeye aonje.Ni hatari sana.
Alipokumbwa na skendo ya kuuza mapango ya serikali kwa mipango ya kando na wadogoze,umalaika wake ukapungua nguvu,ikaonekana kuwa kumbe hata malaika wana tamaa kama biandamu.
Marehemu Gavana wa Makete na baadae Handeni akiwa mwandishi mkongwe wa gazeti moja pale Sinza Kijiweni aliandika mambo mengi ya kweli kumuhusu Malaika,kashfa nyingi ambazo mpaka leo zinaishi za malaika ziliwekwa peupe.
Malaika akaenda kituo cha polisi Mabatini,akafungua kesi kuwa marehemu anataka kumuuwa,kamtishia maisha,watu wakashangaa,malaika unatishiwaje kifo na binadamu??Binadamu akawekwa ndani baada ya polisi kurambishwa asalai ya nyika,siku kadhaa malaika haonekani kufuatilia kesi yake,lengo si kutishiwa bali kumnyamazisha binadamu asimseme malaika.
Hajaanza jana wala juzi,ndio maana wengi wanamuogopa,sababu hana mzaha.Ukibisha wewe kiongozi wa watunga sheria,anakuondoa kwa kutumia idadi ya vimalaika vipenda vyeo na pesa mle jengoni,na ili ulijue hilo,chini yako kakuwekea mtu ambaye kamteua kwa nguvu ya cheo chake cha umalaika mkuu.
Tunavunja misingi ya amani,tunavunja nguzoza upendo na amani.Tunaviziana,tunauwana,tunajeruhi na kutesa.Hatujaanza jana,roho hizi zina miaka mingi kati damu na jasho la watu.
Tunamtengeneza malaika mdogo,ili jae kulinda ya malaika mkuu,hata ile ya kusema natamani siku moja niwe kama malaika mkuu,na malaika mkuu kujibu kuwa ninapenda malaika mdogo siyo tu aje awe kama mimi,bali awe zaidi yangu,ni mpango mkakati wa malaika mkuuna malaika mdoo kuwaandaa watu kisaikilojia.
Tusikubali kugawanywa sababu ya udhaifu wa watu kulemewa na madaraka,hizi ni dalili kuwa kuna malaika tuliwapa madaraka bila wao kujiandaa,yamewazidi,hawana namna zaidi ya kutoa upanga wao alani na kucharanga bnadamu kama wanyama.Na hakika,kuna wakati wanatuaibisha,maana wanasema kazi hii ya umalaika mkuu,kwao ni mzigo,walikuwa wanabisha kwa kusabahi tu,lakini wamekaribishwa toka upenuni mpaka chumbani.Hawakutegemea!!
Amini,amini nawaambia...tunakwenda kubaya sana sana,fukuto la chuki na kisasi ni kubwa sana.Kanuni ya kimaumbile ya kumruhusu aliye na tumbo lenye gesi kupumua,ni kanuni hiyohiyo inaruhusu aliye na lake aseme na mwishowe atachoka au atapata ahueni .Kumziba mweye gesi kwa gunzi au kiwiko,ni kuruhusu gesi kupitia mahali pengine penye upenyo.
Nimepita huko na huko,nimeiona gesi ya chuki na malalamiko,si kwa sababu malaika hafanyi lolote,ila lolote analofanya linaweza kufunikwa na matendo yanayojenga sura ya ukatiri katikati ya watu.Ni sawa na dhana ya mashabiki kumshangilia na kumpa pole msakata kabumbu asiye na njumu dhidi ya yule emye njumu na ustadi wa mavazi uwanjani.Kanuni ya maisha ni huruma dhidi ya anaydhaniwa kuonewa.
Sisi wengine si malaika,lakini tunaona wapi malaika unaweza kuwa unakosea.Malaika anayehubiri upendo bila matendo,ni tafsiri ya malaika feki.Hata wafuasi wa malaika,kuna misingi iliyotukuza na kutulea tumeanza kuona inapotea na kumomonyoka.
Raha yake ilikuwa apate bilauli ya damu ya Lissu juu ya meza yake,ili anywe na kusuuzika roho,bahati mbaya damu ile imekuwa ngumu kuipata,ngamia amegoma kupiga goti ili achinjwe,sasa anataka kumchinja ngamia kwa shuruti,yupo radhi kunywa damu chungu ya ngamia inayotokana na ngamia kugoma kuchinjwa.Huyu ni mnywa damu,hajaanza jana wala juzi.Alianza na damu za familia,sasa amehamia kwenye damu za walio nje ya familia.
Mwaka 2005,Kaskazini Magharibi mwa Tanganyika,jimbo la Ziwa(LakeProvince),Mkoa wa Ziwa Magharibi (West-Lake Region)aligombea na kijana toka chama cha Upinzani.Aliona tishio la yeye kupata upinzani,yeye huwa hapendi kukosolewa wala kupigwa,ni mpenda sifa,hujiona kama malaika.Msifie utakuwa wake,mkosoe upasuliwe.Hii ni hulka yake iliyo ndani ya damu.
Hajaanza jana wala leo,2005 hakutaka tabu,alimtumia watu mgombea wa chama cha pili,akaagiza asafirishwe mpaka Makao Makuu ya Nyanza Province,pale akakatiwa tiketi ya Community Airline,wakati huo ipo juu ya ramani zaidi ya Kasuku aliyefurushwa kumpisha Twiga,breki ya kwanza ikawa bandari ya Salama,na moja kwa moja mpaka JB Belmond wakati huo.
Pale alihudumiwa kila kitu,kwa mpango kuwa aachie nafasi kupunguza ushindani,na hakika kwa zawadi ya kutunukiwa cheo kwa wakati ufaao.Huduma zote zilitoka kwa "Malaika",mkuu wa "watakatifu" na "wenyeheri" wasio na mawaa.Kipindi hicho makao ya "malaika" yalikuwa jengo moja na Kibubu cha Ushirika na Maendeleo Vijijini,mkabala na Mkaguzi na Kituo cha kujua lugha ya Hard-Talk ya Steve,pale kwenye jina la "God Made the World,The Dutch Made Holland".
Baada ya mchakato wa tume kupita,na "malaika" kuchukua ushindi wa team kutokufika uwanjani,walituma maafisa wa "kukodi" wa wakati huo Physics,Chemistry na Biology kabla ya kuongezewa C moja katikati,"Malaika" akamtengenezea mchezo mgombea kuwa anamuomba mlungula ili amuachie nafasi ya ukuu wa kitalu.
Hii ni baada ya kupita siku tatu,"malaika" anapigiwa simu bila kupokea maana alishamaliza kazi yake ya kupita bila kuwa na kizuizi cha ukuu wake.Kwa hiyo,huyu ni "malaika" ambaye hutumia mbinu zote ili kuhakikisha anadumisha ukuu wake,wakati akiwa bila majeshi ya mbingu na ardhi,alitumia nafasi na dinari,huyu hawezi kubadili hulka,iwe kwa fimbo au kwa rungu.
Ni aina ya "malaika" wasiotaka kugusika,ana sifa,kiburi na roho mbaya inayojificha katikati ya maneno ya uwongo na lugha za kutaka kuonekana ni wa watu wa chini.Ni hulka ya kisaikolojia mtu wa chini kuona anaambiwa anapendwa kuliko tajiri.Ni tabia za masikini wote duniani,masikini hupenda faraja tupu isiyo na mkakati,tajiri hupenda mkakati usio na faraja,ndio maana wale "interepirinuwaa" walikuja na msemo wakasema "An Interpreneur is a risk taker".
Ni kweli tulipenda kumpa ukuu wa himaya,na wengine hatukulala,usiku na mchana,maana tuliona ni ufadhali huyu kuliko yule mwenye unga kichwani.Tulijipa matumaini nankuchukua hatari kama kucheza bahati nasibu.Lakini,hapana,hakuna maendeleo bila amani na upendo,hakuna maendeleo yenye raha katikati ya chuki na visasi,maendeleo ndani ya zimwi la husuda na machozi ni sawa na nyumba nzuri yenye giza wakati wa mwanga.
Tunapokwenda ni mbali,sio tena salama kwa vizazi vyetu vijavyo.Mchonga alisurubu ndio,lakini hakufika huko,Mzee wa pwani alikuwa swala 5 sana,mengi alisema hewala,nitamaliza na kuondoka,Chinga mwanzo wake alikuwa muoga na kauli na jicho la mchonga,alipofukiwa Mchonga akakosa washauri,akaangukia kwa ambao mpaka kesho anawasikitikia.Handsome wetu hata wale wa mfumo walipomsaidia bila kumpa taarifa,aliwaambia waacheni hao,watasema watachok.Huyu "Malaika" anaagiza na kuomba kikombe na yeye aonje.Ni hatari sana.
Alipokumbwa na skendo ya kuuza mapango ya serikali kwa mipango ya kando na wadogoze,umalaika wake ukapungua nguvu,ikaonekana kuwa kumbe hata malaika wana tamaa kama biandamu.
Marehemu Gavana wa Makete na baadae Handeni akiwa mwandishi mkongwe wa gazeti moja pale Sinza Kijiweni aliandika mambo mengi ya kweli kumuhusu Malaika,kashfa nyingi ambazo mpaka leo zinaishi za malaika ziliwekwa peupe.
Malaika akaenda kituo cha polisi Mabatini,akafungua kesi kuwa marehemu anataka kumuuwa,kamtishia maisha,watu wakashangaa,malaika unatishiwaje kifo na binadamu??Binadamu akawekwa ndani baada ya polisi kurambishwa asalai ya nyika,siku kadhaa malaika haonekani kufuatilia kesi yake,lengo si kutishiwa bali kumnyamazisha binadamu asimseme malaika.
Hajaanza jana wala juzi,ndio maana wengi wanamuogopa,sababu hana mzaha.Ukibisha wewe kiongozi wa watunga sheria,anakuondoa kwa kutumia idadi ya vimalaika vipenda vyeo na pesa mle jengoni,na ili ulijue hilo,chini yako kakuwekea mtu ambaye kamteua kwa nguvu ya cheo chake cha umalaika mkuu.
Tunavunja misingi ya amani,tunavunja nguzoza upendo na amani.Tunaviziana,tunauwana,tunajeruhi na kutesa.Hatujaanza jana,roho hizi zina miaka mingi kati damu na jasho la watu.
Tunamtengeneza malaika mdogo,ili jae kulinda ya malaika mkuu,hata ile ya kusema natamani siku moja niwe kama malaika mkuu,na malaika mkuu kujibu kuwa ninapenda malaika mdogo siyo tu aje awe kama mimi,bali awe zaidi yangu,ni mpango mkakati wa malaika mkuuna malaika mdoo kuwaandaa watu kisaikilojia.
Tusikubali kugawanywa sababu ya udhaifu wa watu kulemewa na madaraka,hizi ni dalili kuwa kuna malaika tuliwapa madaraka bila wao kujiandaa,yamewazidi,hawana namna zaidi ya kutoa upanga wao alani na kucharanga bnadamu kama wanyama.Na hakika,kuna wakati wanatuaibisha,maana wanasema kazi hii ya umalaika mkuu,kwao ni mzigo,walikuwa wanabisha kwa kusabahi tu,lakini wamekaribishwa toka upenuni mpaka chumbani.Hawakutegemea!!
Amini,amini nawaambia...tunakwenda kubaya sana sana,fukuto la chuki na kisasi ni kubwa sana.Kanuni ya kimaumbile ya kumruhusu aliye na tumbo lenye gesi kupumua,ni kanuni hiyohiyo inaruhusu aliye na lake aseme na mwishowe atachoka au atapata ahueni .Kumziba mweye gesi kwa gunzi au kiwiko,ni kuruhusu gesi kupitia mahali pengine penye upenyo.
Nimepita huko na huko,nimeiona gesi ya chuki na malalamiko,si kwa sababu malaika hafanyi lolote,ila lolote analofanya linaweza kufunikwa na matendo yanayojenga sura ya ukatiri katikati ya watu.Ni sawa na dhana ya mashabiki kumshangilia na kumpa pole msakata kabumbu asiye na njumu dhidi ya yule emye njumu na ustadi wa mavazi uwanjani.Kanuni ya maisha ni huruma dhidi ya anaydhaniwa kuonewa.
Sisi wengine si malaika,lakini tunaona wapi malaika unaweza kuwa unakosea.Malaika anayehubiri upendo bila matendo,ni tafsiri ya malaika feki.Hata wafuasi wa malaika,kuna misingi iliyotukuza na kutulea tumeanza kuona inapotea na kumomonyoka.