Kwa kuwa CHADEMA imepoteza dira, Watanzania twendeni na ACT Wazalendo

Kwa kuwa serikali iliyopo madarakani inahitaji chama cha upinzani chenye maadili na miiko ya kimaadili ili kuisimamia na kuikosoa inapokosea serikali, nawashauri watanzania twendeni na Act wazalendo.

Chadema sasa hivi imekengeuka kimaadili, inatetea wauza madawa ya kulevya, mafisadi, wakwepa kodi na wachawi. Kwa hiyo chadema ya leo haina moral authority ya kuikosoa serikali wala kuishauri.

Hivyo basi watanzania wenye kupenda nchi yao lazima tujenge chama kingine chenye nguvu mbadala wa ccm, tunachoweza kukikabidhi nchi na kila mtu akawa na imani kwamba nchi ipo kwenye mikono salama.

Chadema hii inayotetea kila aina ya uchafu na kimbilio la mafisadi na wauza madawa ya kulevya, haiwezi kuwa chama salama cha kukabidhi nchi yetu.

Kuwakabidhi nchi chadema, ni sawa na kuwapa nchi mafisadi, wauza madawa ya kulevya, majizi na wakwepa kodi.

Chadema ya leo haina kanuni taratibu wala miiko ya chama, hivyo haifai kukabidhiwa nchi.

Twendeni na Act wazalendo angalau kina miiko na azimio la Tabora.
Ccm sasa hivi wanatembea na mitutu
 
Back
Top Bottom