Kwa kutumia namba ya kitambulisho cha Utaifa (pasipo kitambulisho chenyewe) naweza kufuatilia international passport?

kambagasa

JF-Expert Member
Aug 18, 2014
2,241
1,748
Wakuu wahenga walisema mvumilivu hula mbivu mie msemo huu uko kinyume means yamenishinda. Naweza kutumia namba ya kitambulisho cha Taifa vinavyotolewa na NIDA nikapata passport ambayo itanisaidia kuvuka border za watu?
 
Haswa. Na ndicho wanachotaka pale Uhamiaji, namba ya NIDA wala sio kadi. Kamwe hutaulizwa kitambulisho chenyewe ili kupata passport yoyote hata diplomatic passport, namba ya NIDA tu ndio inahitajika.
 
Wakuu wahenga walisema mvumilivu hula mbivu mie msemo huu uko kinyume means yamenishinda. Naweza kutumia namba ya kitambulisho cha Taifa vinavyotolewa na NIDA nikapata passport ambayo itanisaidia kuvuka border za watu?
Usipate tabu kijana fanya hivi nenda www.nida.go.tz kisha nakala ya kitambulisho kisha weka namba ya nida kisha jibu maswali yote utakayopata baada ya hapo download nakala ya kitambulisho peleka huko uhamiaji mambo yatakuwa poa sana hao wanaosubiri hard copy wacha waendelee wewe panda pipa kaongee Kichina huko Bejing
 
Back
Top Bottom