Elections 2010 Kwa kumuapisha Shein Wamevunja Katiba ya Muungano?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:

Ibara 50:2(f) - atakapoapishwa Rais mwingine kushika nafasi ya
Rais pamoja na Makamu wake;

Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki


Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:


6) Makamu wa Rais hatakuwa kwa wakati huo huo Mbunge,
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, wala Rais wa Zanzibar.

Sijui inawezekana kuwa sasahivi:

JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?

Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.
 
The loophole is the 'huo huo' part.

I do agree though, CCM shouldn't be allowed to govern either territory.
 
Mkuu MM, ukiwabana sana watakuambia alishajiuzulu kwani kifungu cha 50: (2c) cha Katiba ya JMT kinaruhusu nafasi ya Makamu wa Rais kufikia ukomo kwa kujiuzulu.

Kwa kuzingatia kuwa umeibua hoja hiyo kwa sasa inawezekana barua ya kujiuzulu inaandaliwa haraka ili iingizwe kwenye file.
 
mmh.. mbona hawakutuambia kajiuzulu maana baada ya kujiuzulu Kikwete alitakiwa ateua Makamu mwingine..ambaye angetakiwa apitishwe na Bunge. Fikiria kwa mfano, Mahakama isitishe kutangaza matokeo ya Urais ili kesi iweze kuangaliwa... itakuwaje? Au labda mimi nimekosea kuwa Kikwete sasa hivi siyo Rais?
 
mmh.. mbona hawakutuambia kajiuzulu maana baada ya kujiuzulu Kikwete alitakiwa ateua Makamu mwingine..ambaye angetakiwa apitishwe na Bunge. Fikiria kwa mfano, Mahakama isitishe kutangaza matokeo ya Urais ili kesi iweze kuangaliwa... itakuwaje? Au labda mimi nimekosea kuwa Kikwete sasa hivi siyo Rais?

Watakuambia bado hajakiuka katiba kwani Kifungu cha 50:4 kinampa siku 14 kufanya uteuzi wa mtu mwingine. Kwa vyovyote kama wataandika barua ya kujiuzulu itakuwa siku moja ama mbili kabla ya kuapishwa kwake kuwa Rais wa ZNZ
 
Ndo tatizo la dhuruma wamemwapisha fasta fasta ili kufunika kombe mwanaharamu apite
 
Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:



Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki


Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:




Sijui inawezekana kuwa sasahivi:

JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?

Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.

Mwanakijiji. Heshima kwanza.

Hivi uliona Post iliyokuwa na "Orodha ya Wabunge Vihiyo wa CCM"?

Tuna aina ya viongozi ambao ni wakurupukaji na washauri ambao hawana shule.

Safari ni fupi. Tutafika tu.
 
Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:



Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki


Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:




Sijui inawezekana kuwa sasahivi:

JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?

Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.

sheria za katiba zina utaalamu wake. kmbuka hii si mara ya kwanza kuwa na situation kama hiyo.
 
Mgombea Ubunge.. kuwa "si mara ya kwanza" haina maana ni halali.. labda unisaidie kwa kutumia utaalamu wa Katiba uliopo kuelezea kilichofanyika kinakubalika kwa misingi ipi. Nataka kujifunza.
 
Mwanakijiji mambo ya Tanzania wewe acha tu. Niliwahi kuuliza kuwa mgombea mwenza wa Kikwete, Dr. Gharib Bilal anatumia kifungu gani cha katiba kutoa maagizo kwa vyombo vyetu vya dola na Usalama. Nilijiuliza ni vifungu gani vya katiba vinamruhusu kupata protokali alizokuwa anapewa kwenye kampeni, sikupata jibu. Kwa Tanzania CCM ni dola na ukishakuwa kiongozi ndani ya CCM, unakuwa kiongozi wa serikali na ukiwa kiongozi wa serikali moja kwa moja unakuwa msemaji wa CCM. Ndio maana Makame, JWTZ na sasa Usalama wa taifa nao wametumbukia wanapigana vikumbo katika kuwajibia CCM. KATIBA ?
Labda ya CCM na mafisadi.
 
Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:



Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki


Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:




Sijui inawezekana kuwa sasahivi:

JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?

Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.
Nadhani viongozi wetu wa siasa hawaaminiani kabisa ndio maana wanavunja baadhi ya sheria, kanuni na taratibu kama ilivyofanywa hapo.

Maana, si ajabu kulikuwa na hisia kuwa, endapo asipoapishwa mapema, wapinzani wangeweza kubadili msimamo na kudai kurudiwa kwa uchaguzi. Kwa kumuapisha mapema, wapinzani wanakosa uwezo huo kwakuwa Katiba zinazuia kumshitaki Rais.

Ndio maana huwa nasema kila mara kuwa, Katiba yetu haiwezi kutusaidia kabisa. Inatakiwa mgombea yeyote wa kiti chohcote cha kisiasa kuachia madaraka aliyonayo kwenye serikali mara baada ya kutangazwa kuwa mgombea wa kiti anachotaka kugombea. Hii iwe kwa kiti cha u-Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na unaibu waziri. Rais awe na jukumu la kuunda serikali ndogo ya kumsaidia kumaliza kipindi chake hadi atakapoapishwa Rais mwingine.
 
Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:



Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki


Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:




Sijui inawezekana kuwa sasahivi:

JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?

Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.

Jibu ni Yes, black & white:
Kama umechakachua kura, ustarajie utakuwa na muda wa kuangalia katiba. Uchakachuaji wenyewe ni kuvunja katiba, sasa hapo, msaada gani tutakupatia Mwanakijiji. Majibu yako obvious!!
 
Kwani wadau ni hapo tu ndio sheria inakiukwa,mbona ni kila mahali kwa kila kitu watawala wakitaka wao inakuwa tu.Mbona utawala wa sheria haupo,labda watatuletea sheria ya utawala na nina uhakika hiyo wataitii na kuiheshimu kwani itawasidia kwenye malengo yao ya kumdidimiza mwananchi.
 
Tatizo kubwa ni kwamba hatuna Mahakama ya Katiba, hivyo panapotokea uvunjifu wa katiba na viongozi wa serekali inakua kazi kubwa kushughulikia hilo swala, maana hata hiyo mahakama kuu bado haiko competent sana ukiangalia kesi ya Mtikila kuhusu mgombea binafsi.
 
Kwa vile Katiba ya Muungano inasema kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakoma kuwa Makamu kati ya sababu nyingi ni hii:



Kwa maana hiyo kwa vile hadi sasa Rais mpya na makamu wake hawajaapishwa na kwa vile sote tunakubaliana kisheria kuwa bado Kikwete ni Rais halali (kwani naye Urais wake wa miaka mitano unakoma pale atakapoapishwa kwa miaka mingine mitano) hivyo Dr. Mohammed Shein bado ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano - kwani namna nyingine zote za kuuondoa Umakamu kwa Mujibu wa Katiba hazihusiki


Na kuwa Katiba ya Muungano inatangulia kusema kuwa:




Sijui inawezekana kuwa sasahivi:

JMT - haina makamu wa Rais kwa vile aliyekuwa Makamu wa Rais ni Rais wa Zanzibar? Kama ni kweli, amepoteza umakamu wake vipi wakati Rais mpya na Makamu wake hawajaapishwa bado?

Kulikuwa na haraka gani ya kumuapisha Rais wa Zanzibar wakati bado ni makamu wa Jamhuri ya Muungano? Labda ninausingizi kuna kitu kimenipitia, naomba msaada.
Mzee Mwanakijiji, pole sana. Tanzania hakuna katiba. kama ingelikuwepo mambo mengi yangelikuwa sawa. Je wadhani kwa hali ilivokuwa Unguja wangelichelewesha masaa hata mawili pale? thubutuuu.... Punda afe mzigo wa bwana ufike.:thinking:
 
tatizo sheria zetu zina clw bck clauses, yaani we ukisema katiba, kumbe kuna ka Act suppliment kanampa pawa mtu kama huyo, yaani tumepewa na mkono wa kulia halafu wanakupora kwa mkono wa kushoto., ngoja niperuzi hako ka supliment nikikapata nitakupostia mzee mwanakijiji
 
Mwanakijiji. Heshima kwanza.

Hivi uliona Post iliyokuwa na "Orodha ya Wabunge Vihiyo wa CCM"?

Tuna aina ya viongozi ambao ni wakurupukaji na washauri ambao hawana shule.

Safari ni fupi. Tutafika tu.
i like this one .napata matumaini
 
Katiba ya JMT kwa masuala yanayoigusa Zanzibar imekuwa kama haipo vile. Wanaposema Zanzibar ni NCHI katiba ya JMT haisemi hivo. Walipompigia mizinga 21 Rais Karume kumuaga walikuwa na maana gani? Juzijuzi hapa tumeona Karume anawapa kamisheni wanajeshi wa vikosi vyake eti naye sasa Amiri Jeshi wa Vikosi vya Zanzibar! Makubwa zaidi yanakuja. Wewe subiri serikali mpya zianze kazi wiki ijayo.
 
Back
Top Bottom