Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
kauli mbiu ya "mapinduzi daima," pamoja na mambo mengine inawakilisha dhana kwamba madaraka ya kuongoza nchi, milele na milele yatabakia mikononi mwa kundi dogo la Wazanzibari waliotwaa madaraka kufuatia mapinduzi ya tarehe 12/1/1964, na kizazi chao. Jambo hilo linadhihirishwa na uamuzi wa kuendelea kuiita serikali ya visiwa hivyo,"Serikali ya mapinduzi." Katika hali halisi, serikali iliyowekwa madarakani kwa ridhaa ya wananchi wenyewe kupitia kura zao, haiwezi kuitwa serikali ya mapinduzi.lakini kwa upande wa Zanzibar, wameendelea kutumia jina hilo, pamoja na ukweli kwamba tangu mwaka 1984 serikali ya Zanzibar imekuwa ikipatikana kupitia kwa kura za wananchi. Kwa wadadisi wa mambo, kuendelea kutumika kwa jina hilo la "Serikali ya Mapinduzi" kunahashiria jambo moja tu, nalo ni kwamba; mfumo wa demokrasia ya kiberali ulioanzishwa hapo visiwani, na mabadiriko ya katiba ya mwaka 1984, ni mpakakazo usio na maudhui, zoezi zima likiwa ni kuhadaa jumuiya ya kimataifa, ili iweze kuamini kuwa katika visiwa hivyo uongozi wa nchi unaingia na kutoka madarakani, kupitia sanduku la kura.Hata hivyo katika halisi mambo hayako hivyo. kwakuwa Seif ni mwadhirika wa mpakazo huo kwa mara tatu mfululizo, safari hii ameona vema akasalimu amri na achie harakati za kuleta demokrasia pana visiwani hapo kwa vizazi vijavyo.