Kwa kufungwa JamiiForums, nimegundua blog nyingi za Tanzania ni wabaguzi

hazole1

JF-Expert Member
Jan 3, 2015
4,319
3,911
Siku zote imekuwa ni kawaida mitandao ya kijamii kubadilishana habari na ninadhani utamaduni wa habari ndio upo hivyo kwa sababu hii dunia ni kubwa sana kwahiyo chombo kimoja cha habari tu hakiwezi kujikamilisha.

Na ninawashukuru sana uongozi wa JF ukileta hapa habari lazima waombe na chanzo cha hiyo habari. Kufungwa kwa JF wengi tulipata tabu sana kutafuta habari na kuangalia kila mtandao wanasemaje kuhusu JF.

Na tunashukuru vyombo vya habari vikubwa kwa mfano kama BBC, Mwananchi na kadhalika walikuwa wanatueleza kila hatua waliyofikia uongozi wa JF. Wakati JF imefungiwa nilidhani hao walionesha ukomavu wao katika tasnia ya habari na walijua hili swala ni la kupita tu. Na lazima waoneshe mshikamano wa habari.

Lakini cha kunishanga kuna blog kama Muungwana na Mpekuzi n.k. ambazo zina wasomaji wengi na nilikuwa naziamini kwa kupata habari lakini sijawahi kuona wameandika kuhusu habari ya kufungwa JF au kufunguliwa. Na hapa ndipo nilipokuja kugundua hawa jamaa wanafanya habari kibaguzi halafu wameonesha usaliti kwa umoja wa vyombo vya habari.
 
Hili jukwaa ndilo kila kitu, niengi mno yametupita kwa kipindi hiki cha wiki 3! Hongera sana Jf na Max Mello na uongozi wote kwa ujumla! Binafsi nipo kijijini sana(kisiwani) kuna matokeo kadhaa ya kuuawa kwa wavuvi kwenye opetasheni ya Mpina inayoendeshwa na viongozi wa vijiji maeneo ya Sengerema na Nkome, lakini sikuweza kutoa taarifa kwenye majukwaa mengineyo kwa vile haya aminiki!
 
Hizo blog ndiyo kwanza naziskia leo, ndani ya mda wote ambao jf haipo hewani nilikuwa natembelea site ya xvid kila baada ya dk 15 na nimedownload video zisizo pungua elfu moja, kuondoka kwa jf imenisababishia addicted nyingne
 
Wamiliki wa hizo blog ni Masoud Saanani na zMuhidin Isa Michuzi, hawa wote ni watu wasiojulikana, kuipigania jf isiopendwa na jiwe ni kama kujichimbia kabuli
 
Back
Top Bottom