Kwa kiufupi sana Mbowe hana njaa na hajawahi kuwa na njaa, wenzetu wanazitumia kanuni hii something kupata viongozi

mr mkiki

JF-Expert Member
Sep 22, 2016
5,583
11,659

Wakati mwingine nadhani hata katiba mpya haitotusaidia sana, hii nchi wajinga ni wengi sana kiasi kwamba hata tukiandikiwa katiba kutoka mbinguni hatutoweza kusimama

Kinachohitajika ni mass education kwa umma huu ambao una utapiamlo wa maarifa

Elimu Elimu Elimu is what we need.

Nashawishika kusema tunahitaji kuwa makini na kauli & matendo katika kuchagua viongozi. Hawa watu wanatuita majina mengi tu wanyonge, mara hakuna hela kwa sababu ya Corona na mishahara haiwezi kupanda wakati ni takwa la kisheria. Kwa sheria hizo hizo kama viongozi tunapeana anasa & zawadi za kisheria etc

Hii kwetu kama mada ya kufikiria nchi yetu , hatuwezi kuwapa watu masikini nchi kuligana na nature za binadamu kwasasa. Ndio maana kwa kanuni hii wenzetu waliliona hili na kulifanyia kazi.


Kinachouma ni kuona walio wengi wanashindwa kujua kuwa kilichofanyika pale ni abuse of power na unjustifiable uses of taxpayer's money.

Elimu yetu ilivurugwa purposely ili kuwafanya watu washindwe kuwaza critically, haya ndio madhara yake sasa.

Huwezi kumpima kiongozi kwa kutaja jina Mungu kila wakati hakuna narudi hakuna , eti kiongozi kila wakati anataja vifungu vya bibles ndio nipate jiba kuwa huyu ndio kiongozi!! Ni ujinga narudi ni ujinga.

Tuna viongozi wengi walioweza kufanikiwa katika maisha hawa kwasasa tunapaswa kuwangeukia na kuwapa nchi. Mfano Mbowe..Kwa kiufupi sana Mbowe hana njaa na hajawahi kuwa na njaa

1980s Mbowe anasafirisha matunda nje ya nchi kwa Gulf Air.wakati wewe na babako mkipanda basi mnatapika.

1985, Freeman MBOWE ana boti la uvuvi, anaenda deep sea... sidhani kama DC Sabaya, yule mtangazaji mwenye kitambi clouds au Simalenga walikuwa wamezaliwa.hawa wanatumika tuu, Mbowe hayupo kwenye league yao

Kama haitoshi gari La mbowe La kwanza alipewa kibali na nyerere ili aingize nchini na ni BMW enzi hizo.


Hoja ya kupeana muda ni hoja mfu, siipendi na siikubali kamwe. Hakuna muda wa kupena wakati viongozi wakigawana zawadi na anasa nyingine za kisheria huku wavuja jasho wakiambiwa wasubirie stahiki zao za kisheria. Sasa wanasubiri nini haswa? Watumishi wa Umma wasubiri hadi lini? Hawa viongozi tuliokuwepo nao wana NJAA JAMANI HAKUNA KIONGOZI HAPA.

Mwaka 1967, Nyerere alikataa kutumia gari la Rolls Royce akidai kuwa lilikuwa ni anasa tupu. Akaenda mbali zaidi mpaka kwa Mlinzi wake, Peter Bwimbo, aliyekuwa anatumia Mercedes Benz 190 na kumshawishi aliuze ili ajenge nyumba yake huko Mara! Leo, Samia anagawa Benz! Ujinga! Japokuwa wakati huo kweli idadi ilikuwa ndio so siwezi kupiga lakini kwa wakati huu tunapaswa kubadili direction mapema.

I totally agree with you kwamba viongozi wanaojali maisha ya watu should walk the talk. Na hawa lazima wawe mfuko wana hela sio za kukopa ili upate uongozi ziwe inner money.

Hapo tunaweza kutoka katika maji haya.

mr mkiki.
 
Jakaya Kikwete na Benjamin Mkapa waliuziwa nyumba za serikali kwa bei ya kutupa.

Bado tumewajengea tena mahekalu ya Bure. Huu ni umasikini wa viongozi wetu
 
Kama mtu anakuwa Rais wa nchi hii kwa miaka 10 bado hawezi kujijengea nyumba yenye hadhi yake mimi wa kima cha chini mnatarajia nijenge kwa muujiza gani?
Nchi hii ni zaidi ya unavyoifahamu.

Hawa watu tunapa Nchi ni masikini sana tutoke huku jamani
 
Huyo mbowe mbona hajengi ofisi ya chama wala hatumi mishahara ya wafanyakazi mikoani?
 
Wenzetu waliona mbali huwezi ukapewa leseni ya udereva kama wwe ni masikini.Hofu utawaletea itikadi za kimasikini.Umasikini ni roho kamili inarithishwa.
 
Jakaya Kikwete na Benjamin Mkapa waliuziwa nyumba za serikali kwa bei ya kutupa.

Bado tumewajengea tena mahekalu ya Bure. Huu ni umasikini wa viongozi wetu
Laiti tungapata viongozi kama wakoloni tungekuwa mbali sana
 
Nani mwenye njaa au asiye na njaa asiyetafuta ziada.wengi hatujaridhikiwa kiuchumi
 
Ivi marekani walishawahi kumpa nchi masikini???


Maana trump kila mtu anajua balaa lake
 
Back
Top Bottom