Kwa kitendo hiki nasema Hongera JK

Mugishagwe

JF-Expert Member
Apr 28, 2006
300
58
Baada ya kusoma hii habari kweli nimesisimka mwili kwa moyo huu nasema Hongera JK na wako wengi wenye matatizo ila ndiyo hivyo wako zaidi ya Sikonge .

2006-09-10 09:55:19
Na Mwandishi Maalum


Rais Jakaya Kikwete, ameahidi kusaidia kutafuta wafadhili wa kuwezesha upatikanaji wa mashine katika Idara ya Upasuaji Bandia katika hospitali ya Taifa Muhimbili.

Rais Kikwete ametoa ahadi hiyo baada ya kufurahishwa na namna madaktari wa hospitali hiyo walivyomtibu mtoto Bakari Hamis Katumbaku, mkazi wa Sikonge, mkoani Tabora.

Aliushukuru uongozi wa hospitali hiyo, hususan Profesa Atef Amin na Dk. Laurean Rwanyuma kutokana na kufanikisha upasuaji kwa mtoto huyo na hivyo kumrejesha katika hali yake ya kawaida.

Rais Kikwete alisema kutokana na furaha yake hiyo na kuridhishwa na kazi kubwa inayofanywa na madaktari katika hospitali ya Taifa Muhimbili, anauagiza uongozi wa hospitali hiyo, kufanya utafiti wa kina wa gharama za baadhi ya mashine muhimu zinazohitajika katika Idara ya Upasuaji Bandia (Plastic Surgery).

Alisema yeye atawatafuta watu wenye mapenzi mema ili wagharamie mashine hizo.
Alitoa shukrani hizo na agizo hilo juzi jioni wakati akimkaribisha mtoto Bakari Ikulu kwa lengo la kumjulia hali na kuagana naye baada ya kukamilika kwa matibabu yake.

Mtoto huyo alifika Ikulu akifuatana na mama yake, Bi. Aziza Katumbaku, Daktari wake, Laurean Rwanyuma na Muuguzi, Bi. Ritha Kitama.

Profesa Atef Amin ambaye ni raia wa Misri hakuweza kufika kutokana na majukumu hospitalini hapo.

Rais alimuona mtoto Bakari akitembea vizuri bila dalili zozote za kujikunja au maumivu kama alivyomuona mara ya kwanza kule Sikonge.

’’Nashukuru sana, umepona kabisa? Daktari nashukuru sana. Nilipomuona mara ya kwanza Sikonge, hali yake ilikuwa mbaya, alikuwa akitembea kwa kuinama na akajitahidi kunikimbilia kama watoto wenzake lakini kwa taabu sana. Nikasema Mungu akijalia nitakusaida, Mungu mkubwa, nimefurahi sana,’’ alisema.

Akitoa shukrani zake kwa Rais, mtoto Bakari ambaye alikumbatiana kwa furaha na Rais kama Baba na mwanae, alisema; ’’nakushukuru sana, Rais, Mungu akujalie, sina cha kusema nakushukuru sana. Nimefurahi sana,’’

Naye Mama wa Bakari alisema ’’Nakushukuru sana na kukupongeza kwa kutimiza ahadi yako, haikuwa rahisi kwangu kuamini pale nilipoletewa taarifa kwamba umeagiza tuje Muhimbili kwa matibabu. Sikutegemea kama mtoto wangu leo angeweza kutembea vizuri kama watoto wenzake,’’ alisema.

Katika maelezo yake kwa Rais kuhusu upasuaji aliofanyiwa mtoto Bakari aliyeungua moto wakati akiwa na umri wa miaka sita na kumsababishia maumivu makali yaliyomfanya ashindwe kutembea vizuri, alisema, Idara ya Upasuaji katika hospitali hiyo, haina mashine muhimu ambazo zingesaidia sana kuokoa maisha ya Watanzania wengi hususan wale wanaopata ajali za kuungua moto na kupoteza asilimia kubwa ya ngozi zao.

Dk. Rwanyuma alisema Idara hiyo ambayo hadi miaka ya hivi karibuni ilikuwa haina wataalamu wa upasuaji bandia, isipokuwa wale wa kutoka nchini Misri, inahitaji mashine zinazoweza kuotesha ngozi au kuitanua hususan pale mgonjwa anapokuwa amepoteza asilimia zaidi ya 80 ya ngozi yake.

Aidha, alisema pamoja na kupatikana kwa mashine hizo, pia mafunzo yanahitajika ili kuweza kupata wataalamu wengi zaidi katika idara hiyo.

Alisema hali hiyo itasaidia mno katika si tu kuokoa maisha ya Watanzania bali pia kurekebisha viungo.

SOURCE: Nipashe
 
Maswali yako duh !!!!
Swala si la wataalam husika swala ni umasikini uliokithiri maana huyo Mama alitaka kwenda hospital na nadhani alisha enda huko Tabora na madaktari wanajua hilo na watakuwa walimweleza kwamba inawezekana lakini pesa zinatakiwa .Sasa wataalam wa nini kwenye hili ? Hapa ni umasikini Mana kuweza kulipia matibabu.
 
tafiti,

nadhani hatuwezi kuwalaumu wataalam in this particular case. Maana wao wako Muhimbili na huyu kijana alikuwa Tabora. Hata hawawezi kujua of his case mpaka iwe referred kwao. Case ilipoletwa kwao, na gharama ikawa si issue, wamefanya vitu vyao! Pia imetuonyesha kuwa wataalam tunao nchini.

Yes, kwa hili JK anastahili hongera. It shows the kind of heart you have .. may the same spirit prevail in tackling matatizo na kero nyingine za wananchi. Yaani zikuguse kama lilivyokugusa hili na uwe na azma ya dhati ya kuzitatua. Penye nia ipo njia.

In your position, you should aim in changing the system in general ili hawa akina Sikonge iwe hawahitaji tena mpaka rais atoe agizo kuwa waletwe muhimbili kwa matibabu.
 
safi. Lakini sasa nahisi kuna kina-Bakari wengi sana ambao kamwe hawataweza kumuona Rais. Tatizo langu ni hii tabia iliyozuka ya kutatua matatizo kwa mtindo wa matukio. Nilifikiri angemtumia Rashid kama case study ili aibuke na sera ya kuboresha huduma zetu na namna ya serikali kugharamia matibabu kama haya kisera. Ili kwamba hata akija Rais asiye na 'huruma' kama yeye bado watu waendelee kupata huduma kwa mujibu wa sheria na sera zinaongoza sekta ya afya.
 
Ahadi nyingine ya JK...hivi hii ni ya ngapi vile tangu aingie madarakani?Mnapongeza ahadi au utekelezaji wa ahadi?Beware of populist politicians,they wont hesitate taking advantage of your problems in advancing their own populist agenda.
 
Baada ya kusoma hii habari kweli nimesisimka mwili kwa moyo huu nasema Hongera JK na wako wengi wenye matatizo ila ndiyo hivyo wako zaidi ya Sikonge .

2006-09-10 09:55:19
Na Mwandishi Maalum


Rais Jakaya Kikwete, ameahidi kusaidia kutafuta wafadhili wa kuwezesha upatikanaji wa mashine katika Idara ya Upasuaji Bandia katika hospitali ya Taifa Muhimbili.

Rais Kikwete ametoa ahadi hiyo baada ya kufurahishwa na namna madaktari wa hospitali hiyo walivyomtibu mtoto Bakari Hamis Katumbaku, mkazi wa Sikonge, mkoani Tabora.

Aliushukuru uongozi wa hospitali hiyo, hususan Profesa Atef Amin na Dk. Laurean Rwanyuma kutokana na kufanikisha upasuaji kwa mtoto huyo na hivyo kumrejesha katika hali yake ya kawaida.

Rais Kikwete alisema kutokana na furaha yake hiyo na kuridhishwa na kazi kubwa inayofanywa na madaktari katika hospitali ya Taifa Muhimbili, anauagiza uongozi wa hospitali hiyo, kufanya utafiti wa kina wa gharama za baadhi ya mashine muhimu zinazohitajika katika Idara ya Upasuaji Bandia (Plastic Surgery).

Alisema yeye atawatafuta watu wenye mapenzi mema ili wagharamie mashine hizo.
Alitoa shukrani hizo na agizo hilo juzi jioni wakati akimkaribisha mtoto Bakari Ikulu kwa lengo la kumjulia hali na kuagana naye baada ya kukamilika kwa matibabu yake.

Mtoto huyo alifika Ikulu akifuatana na mama yake, Bi. Aziza Katumbaku, Daktari wake, Laurean Rwanyuma na Muuguzi, Bi. Ritha Kitama.

Profesa Atef Amin ambaye ni raia wa Misri hakuweza kufika kutokana na majukumu hospitalini hapo.

Rais alimuona mtoto Bakari akitembea vizuri bila dalili zozote za kujikunja au maumivu kama alivyomuona mara ya kwanza kule Sikonge.

’’Nashukuru sana, umepona kabisa? Daktari nashukuru sana. Nilipomuona mara ya kwanza Sikonge, hali yake ilikuwa mbaya, alikuwa akitembea kwa kuinama na akajitahidi kunikimbilia kama watoto wenzake lakini kwa taabu sana. Nikasema Mungu akijalia nitakusaida, Mungu mkubwa, nimefurahi sana,’’ alisema.

Akitoa shukrani zake kwa Rais, mtoto Bakari ambaye alikumbatiana kwa furaha na Rais kama Baba na mwanae, alisema; ’’nakushukuru sana, Rais, Mungu akujalie, sina cha kusema nakushukuru sana. Nimefurahi sana,’’

Naye Mama wa Bakari alisema ’’Nakushukuru sana na kukupongeza kwa kutimiza ahadi yako, haikuwa rahisi kwangu kuamini pale nilipoletewa taarifa kwamba umeagiza tuje Muhimbili kwa matibabu. Sikutegemea kama mtoto wangu leo angeweza kutembea vizuri kama watoto wenzake,’’ alisema.

Katika maelezo yake kwa Rais kuhusu upasuaji aliofanyiwa mtoto Bakari aliyeungua moto wakati akiwa na umri wa miaka sita na kumsababishia maumivu makali yaliyomfanya ashindwe kutembea vizuri, alisema, Idara ya Upasuaji katika hospitali hiyo, haina mashine muhimu ambazo zingesaidia sana kuokoa maisha ya Watanzania wengi hususan wale wanaopata ajali za kuungua moto na kupoteza asilimia kubwa ya ngozi zao.

Dk. Rwanyuma alisema Idara hiyo ambayo hadi miaka ya hivi karibuni ilikuwa haina wataalamu wa upasuaji bandia, isipokuwa wale wa kutoka nchini Misri, inahitaji mashine zinazoweza kuotesha ngozi au kuitanua hususan pale mgonjwa anapokuwa amepoteza asilimia zaidi ya 80 ya ngozi yake.

Aidha, alisema pamoja na kupatikana kwa mashine hizo, pia mafunzo yanahitajika ili kuweza kupata wataalamu wengi zaidi katika idara hiyo.

Alisema hali hiyo itasaidia mno katika si tu kuokoa maisha ya Watanzania bali pia kurekebisha viungo.

SOURCE: Nipashe

Hii ahadi ilitekelezwa ama ilikuwa ahadi hewa?
 
safi. Lakini sasa nahisi kuna kina-Bakari wengi sana ambao kamwe hawataweza kumuona Rais. Tatizo langu ni hii tabia iliyozuka ya kutatua matatizo kwa mtindo wa matukio. Nilifikiri angemtumia Rashid kama case study ili aibuke na sera ya kuboresha huduma zetu na namna ya serikali kugharamia matibabu kama haya kisera. Ili kwamba hata akija Rais asiye na 'huruma' kama yeye bado watu waendelee kupata huduma kwa mujibu wa sheria na sera zinaongoza sekta ya afya.

Mimi naubgana na wewe kabisa.huwezi kumpongeza jk kwa particular case ya mtu 1 2 3 au 20 wakat ni rais wa watz wote.je aliyeko songea bk mwza etc siwanahitaji matibabu?kutibiwa haitakiwi kuwa huruma ya rahisi ni wajibu wa serikali kwa watu wake
 
tafiti,

nadhani
hatuwezi kuwalaumu wataalam in this particular case. Maana wao
wako Muhimbili na huyu kijana alikuwa Tabora. Hata hawawezi kujua of his
case mpaka iwe referred kwao. Case ilipoletwa kwao, na gharama ikawa si
issue, wamefanya vitu vyao! Pia imetuonyesha kuwa wataalam tunao
nchini.

Yes, kwa hili JK anastahili hongera. It shows the kind of heart you have
.. may the same spirit prevail in tackling matatizo na kero nyingine za
wananchi. Yaani zikuguse kama lilivyokugusa hili na uwe na azma ya
dhati ya kuzitatua. Penye nia ipo njia.

In your position, you should aim in changing the system in general ili
hawa akina Sikonge iwe hawahitaji tena mpaka rais atoe agizo kuwa
waletwe muhimbili kwa matibabu.

Angalau mwanzisha thread amekuwa muungwana kwa kuangazia mema ya
kiongozi huyu ambayo kwa kiasi kikubwa yanajaribu kufunikwa na watu
wachache wanaojitahidi kuyatafuta mabaya tu!
 
Mimi naubgana na wewe
kabisa.huwezi kumpongeza jk kwa particular case ya mtu 1 2 3 au 20 wakat
ni rais wa watz wote.je aliyeko songea bk mwza etc siwanahitaji
matibabu?kutibiwa haitakiwi kuwa huruma ya rahisi ni wajibu wa serikali
kwa watu wake

Ni vigumu kwa Rais kumhudumia kila Mtanzania moja kwa moja. Hiyo ni ngumu hata huko Marekani ambako uchumi uko juu zaidi yetu. Lakini mambo madogo kama hili alilofanya Rais yanasaidia kuona nia aliyonayo katika kusaidia pamoja na changamoto zilizopo katika taasisi husika pamoja na serikali kutokana na uchumi.
Rais kujitolea kumtibu, na pia kuagiza vifaa vya matibabu hayo viorodheshwe ili viletwe, huoni kuwa vitasaidia wengi angalau hata kama ni kwa gharama? Je kama angeamua kunyamaza, yote haya yangetokea? Lets view things from a positive perspective
 
Back
Top Bottom