Kwa kauli ya Rais Samia Tanzania ya viwanda imeota mbawa

Kinuju

JF-Expert Member
Mar 20, 2021
2,390
5,310
Tangu aape kuwa Rais wa sita wa Tanzania ni kama hajui kuwa ilani ya CCM inataka Tanzania iwe ya viwanda mpaka kufikia mwaka 2025 ili kuongeza ajira na uzalishaji nchini.

Kwa sasa umeme unasuasua na kuongeza gharama za uzalishaji je nani ataanzisha kiwanda?

Ameruhusu ungizwaji wa bidhaa holela bila kulipiwa kodi, wafanyabiashara wakwepa kodi waliokuwa wanapitishia bidhaa zao bandari ya Zanzibar sasa hivi wamekimbilia bandari ya Dar es Salaam kwa sababu swala la kodi halitiliwi mkazo tena.

Bandari ya Zanzibar sasa hivi chini ya rais Mwinyi huwezi kupitisha bidhaa bila kulipa kodi ndiyo maana wamekimbilia huku bara.

Kauli ya Rais Samia kwamba Tanzania imefunguliwa na bidhaa mbalimbali ziingie tu kutoka kokote hailindi viwanda vya ndani na ni mwiba mchungu kwa waliojenga viwanda.

Ikumbukwe viwanda vilivyoachwa na Nyerere vilikufa baada ya Rais Mwinyi kusema sasa Tanzania ni ruksa kwa kila kitu.

Je, Rais Samia anafuata falsafa za mr ruksa?
 
Acha upotoshaji wa kijinga, nchi hii iliwahi kuwa na viwanda vya kueleweka kipindi cha Nyerere tu, wakati wa Magufuli hiyo Tanzania ya viwanda ilikuwa ni porojo ya kufurahishia genge.

Hakuna popote mama wa kambo aliposema bidhaa ziingie bila kulipiwa kodi.
 
Mtoa mada unaifahamu vizuri historia ya uchumi wa tanzania miaka ya 1981 hadi 1984? Ikiwa jibu ni ndio unaweza kulinganisha ,aelezo yako ktk kipindi hiki na miaka hiyo ambapo tulisita kuagiza bidhaa kutoka mataifa ya nje?
 
Mtoa maada acha kuongea uwongo, Mama amesisitiza sana watu kulipa kodi!

Pamoja na kauli yake kuwaita wawekezaji kuja kuwekeza nchini Tanzania huku akiwahakikishia mazingira rafiki ya uwekezaji, lakini hakuwahi hata siku moja kusema wawekezaji au wafanyabiashara wasilipe kodi.

After all mimi bnafsi sioni sababu sioni ya kuhainga na viwanda kama hatuwezi kuviendesha kwa faida au kwa kuleta unafuu wa maisha kwa wananchi, mfano mzuri ni viwanda vya sukari, Sukari inayozalishwa hapahapa nchini tunauza bei kubwa wakati sukari inayotoka nchi jirani ya Zambia inauzwa bei rahisi kabisa.

Si hilo tu hata mafuta ya petroli, Wazambia na Warundi wanapitishia bandarini kwetu hapa Dsm lakin wanauza bei rahisi kuliuko sisi, kama hivi ndivyo si bora tununue na kuagiza au tukajifunze kwa wenzetu kuliko kung'ang'ania miradi tusiyoiweza!
 
Acha upotoshaji wa kijinga, nchi hii iliwahi kuwa na viwanda vya kueleweka kipindi cha Nyerere tu, wakati wa Magufuli hiyo Tanzania ya viwanda ilikuwa ni porojo ya kufurahishia genge.

Hakuna popote mama wa kambo aliposema bidhaa ziingie bila kulipiwa kodi.
Mimba ya Magufuli itakutesa sana usipokula ndimu na malimao.

Hapa hatuzungumzii mimba yako tunazungumzia Tanzania ya viwanda na ilani ya CCM
 
Shida kubwa waliyonayo wafuasi wa Magufuli wanataka Rais Samia afanye kila kilichokuwa kikifanywa na Magufuli ndio watamuona anafaa,hilo haliwezekani.
Tanzania ya viwanda ni ilani ya ccm
 
Shida kubwa waliyonayo wafuasi wa Magufuli wanataka Rais Samia afanye kila kilichokuwa kikifanywa na Magufuli ndio watamuona anafaa,hilo haliwezekani.
Tena mbaya zaidi wanataka aendeleze matendo ya rohombaya kuliko maendeleo!
Mfano wanataka abambikize wafanyabiashara kodiumiza, na awafungie na kuchua fedha kwenye akaunt zao ndipo wao waridhike!
 
Hiyo Tanzania ya viwanda wajinga ndio walikuwa wanaamini, ila wenye akili zetu tulikuwa tunajua ni utapeli wa mchana kweupe, na ukweli umedhihirika kuwa ni utapeli.

Hiyo unayoita ilani ya CCM sio chochote wala chochote zaidi ya utoto wa uzeeni. Walichofanya hao ccm kwenye ilani yao ni kuweka list ya mahitaji yote ya nchi, kisha chochote watakachofanikisha waseme wanatekeleza ilani. Ule ni uhuni kama uhuni mwingine. Na kwa bahati mbaya sana, uhuni huu unafanywa na chama kilichopoteza mwelekeo na ushawishi kwa umma.
mba ya Magufuli itakutesa sana usipokula ndimu na malimao.

Hapa hatuzungumzii mimba yako tunazungumzia Tanzania ya viwanda na ilani ya CCM
 
Mbawa zenyewe ni kama hizi hapa 👇

Screenshot_20211123-111621.png


Screenshot_20211123-111536.png


Screenshot_20211117-134136.png


Screenshot_20211128-174543.png
 
Hiyo Tanzania ya viwanda wajinga ndio walikuwa wanaamini, ila wenye akili zetu tulikuwa tunajua ni utapeli wa mchana kweupe, na ukweli umedhihirika kuwa ni utapeli.

Hiyo unayoita ilani ya CCM sio chochote wala chochote zaidi ya utoto wa uzeeni. Walichofanya hao ccm kwenye ilani yao ni kuweka list ya mahitaji yote ya nchi, kisha chochote watakachofanikisha wasema wanatekeleza ilani. Ule ni uhuni kama uhuni mwingine. Na kwa bahati mbaya sana, uhuni huu unafanywa na chama kilichopoteza mwelekeo na ushawishi kwa umma.
Maneno yalikuwa mengi Sana harafu hakuna kilichofanyika
 
Back
Top Bottom