nimetafakari kwa kina bado sijaona tatizo kwa kauli ya nassari, ikiwa kauli aliyotoa alikua kwy jukwaa ambapo munkari wake ukiwa juu we achaaaaaaaaaa tu.
Ndugu WanaJF,
swala la nasari kwa maono yangu nayachukulia ni mtaji wa Chadema tena mzuri tu.
1. PUBLICITY
katika hali ya kawaida CCM ilitakiwa iwaonyeshe watanzania kuwa chama chao kupitia serikali iliyopo madarakani kinawasikiliza wananchi ndio maana sasa wamebadilisha wawaziri(hata kama hoja ilianzishwa na wapinzani ni watanzania pia kwahiyo mesemo wa serikali sikivu ungekuwa wa kuweka ushawishi) na kuteua wakuu wa wilaya. jamabo la ajabu midomoni mwa makada wa CCM yanatoka maneno sita neno chadema manne yanaendelea kuilezea chadema.
Kwangu Nape anyokazi kubwa.
2. KUIMARISHA NGUVU YA UMA
Wakati CCM inaendelea na mtindo ulele ule wakushawishi dola ichukue hatua dhidi ya Chadema kwa kuonyesha imefanya jambo baya sana lisilokubalika, Chadema wao wanapita kwa wananchi na kuwaeleza shida wanazopata zinasababishwa na CCM na kuwapa matumaini ya kuwa wao ni mbadala hata kwa kukamatwa na kuwekwa rumande na ya kuwa wako tayari kwa hilo katika kutetea haki zao na sio kufumbia macho ufisadi.
Kwa stahili hii CCM haitawakonga moyo wananchi bali itazidi kuwasha moto.
3. HOJA NZURI KATIKA WAKATI USIO MWAFAKA
kutokana na ukweli kwamba asilimia kubwa ya watendaji wa serikali ni MAKADA WA CCM, watakapoendelea na makati huu wa kusimamia hoja isiyo na mashiko wala tija kwa taifa ni wazi makada hawa nao watalazimika kusimamia kauli za viongozi wao. hali hii itasababisha utendaji kuzorota na matokeo yake ni maisha kuendelea kuwa magumu na kwa hali hii mwananchi hatahitaji lolote kutoka kwa kada wa serikali iliyopo madarakani zaidi ya wanatatuaje matatizo yanayoendelea kuwakabili.
Wana CCM wakati umefika wa kuchagua viongozi wenu wanaojua siasa za ulimwengu wa leo.
nawakilisha, kupinga kwa hoja ni sawa.
shule ya vidudu hujamaliza unakimbilia mijadala ya kaka zako waliomaliza vyuo vikuu kwa degree kibao..!nimetafakari kwa kina bado sijaona tatizo kwa kauli ya nassari, ikiwa kauli aliyotoa alikua kwy jukwaa ambapo munkari wake ukiwa juu we achaaaaaaaaaa tu.
Mkuu Froida umesema kitu ambacho huwa nakisema kila wakati, ma strategist wa CCM huwa wanaenda na matukio hawaangalii impact ya muda mrefu. Mfano mdogo ni tarehe ya hukumu ya Lema ambayo ilipangwa makusudi haikupangwa kwa bahati mbaya lengo lilikuwa ku neutralize sherehe za ushindi wa AR lakini sasa wanajuta.Nassari amepata publicity ya hali ya juu na CCM wasichokijua ni kwamba wanampaisha huyu jamaa kwenye anga za kisiasa vibaya mno kauli yake imeshazubgumzwa na wanasiasa na wananchi wengi kwa nyakati tofauti kutoka maeneo tofauti nimeshasema mara nyingi Strategist party wa CCM mukichwa hamna kitu haoni hii nguvu inayowekwa na CCM kumnanga Nassari ndio inafanya watu wengi watake kumfahamu na chama chake
Ngumu kusahaulika kwa sababu inatenganisha umoja wetu ???
Hebu tujikumbushe kauli hii amabyo ndio kauli ya ukweli katika kutenganisha umoja wetu !!!
Ninyi wanawake wenzangu ambao waume zenu wapo katika vyama pinzani na mnajua wazi kuwa hawawapi ushirikiano wowote katika siasa ya CCM wanyimeni nonino, muone kama hawatarejea katika chama tawala, nonino nikiwa na maana ya tendo la ndoa,
alisema Sophia Simba (MB), huku akishangiliwa na wanawake wote kuonyesha kuwa alilolisema limewagusa.
Hii ilikuwa tarehe 20th June 2010.
Hapo Vipi ???? { Hii "Hapo Vipi" - ni kwa hisani ya Edward Lowassa}
Imepitwa na wakati sasA hivi tunachoangalia na kuzungumza ni VUA GAMBA VAA GWANDA NA M4C
Mkuu pamoja na hayo yote, Kuna ,a,mo yamepikwa sana, Nasari hakuzungumzia mikoa ya kaskazini pekee alitamka MIKOA YA MWANZA, SHINYANGA, MARA, KILIMANJARO, MANYARA, ARUSHA NA TANGA NA AKASEMA TUTAKUWA NA MADINI, MBUGA ZA WANYAMA,BANDARI NA KAZALIKA SASA IMEGEUZWA NA KUWA NI MIKOA YA KASKAZINI TU, MIMI NAZANI ILI KUKATA MZIZI WA FITINA ILETWE ILE RECODED, MSIKIE ALICHO SEMA,