President Elect
JF-Expert Member
- Aug 9, 2011
- 693
- 212
Mazungumzo yaliyomalizika bungeni hivi karibuni, yalipelekea wawakilishi wa Z'bar kukanusha kwamba, kamwe hawawezi kuwa koloni la Tanganyika!
Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar ni 'sehemu' ya nchi ya Tanzania, ambapo visiwa vya Unguja na Pemba vinachangia mikoa mitano ndani ya serikali ya JMT.
Kwa vile katiba yetu pia haitambui kuwepo kwa nchi ya Tanganyika, ni kweli kuwa kamwe Z'bar haiwezi kuwa koloni la Tanganyika. Je, kwa vile iko chini ya Tanzania ndio tuseme kwamba Z'bar ni koloni la Tanzania?
Wazanzibari wana haki ya kudai utaifa wao. Ni vyema watumie mabadiliko ya katiba kuthibitisha hilo.
Na waende mbali zaidi, wadai kiti chao UN! Hapo muungano utakuwa wa maana kwao, kati ya nchi ya Z'bar na Tanganyika.
Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar ni 'sehemu' ya nchi ya Tanzania, ambapo visiwa vya Unguja na Pemba vinachangia mikoa mitano ndani ya serikali ya JMT.
Kwa vile katiba yetu pia haitambui kuwepo kwa nchi ya Tanganyika, ni kweli kuwa kamwe Z'bar haiwezi kuwa koloni la Tanganyika. Je, kwa vile iko chini ya Tanzania ndio tuseme kwamba Z'bar ni koloni la Tanzania?
Wazanzibari wana haki ya kudai utaifa wao. Ni vyema watumie mabadiliko ya katiba kuthibitisha hilo.
Na waende mbali zaidi, wadai kiti chao UN! Hapo muungano utakuwa wa maana kwao, kati ya nchi ya Z'bar na Tanganyika.