Kwa kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?

Wanabodi.

Kwa Kasi Hii ya Rais Wetu Mpendwa, Dr. John Pombe Joseph Magufuli na Falsafa yake ya "Hapa Kazi Tuu", na kama hiki tunachokiona sasa, sio nguvu ya soda tuu, yaani ataendelea kwa kasi hii hii hadi 2020, kuna haja kweli ya kufanya tena uchaguzi wa rais?, si tumwache tuu aendelee mpaka pale tutakaapoona tumetosheka?.

1. Pamoja na ukanyagaji wake wa katiba ya nchi, lakini kwa kazi hii nzuri anayoifanya rais wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, kuinyoosha nchi hii iliyopinda kupindukia kwa rushwa, uzembe na ufisadi, hivi kweli Tanzania, tuna haja tena ya kufanya uchaguzi wa rais kwa mwaka 2020?, au tumwache tuu aendelee mpaka 2025? na kama bado anatosha, aendelee tuu?.

2. Jee hatuwezi kufanya uchaguzi wa wabunge tuu na madiwani, bila kufanya uchaguzi wa rais, na kumwacha Magufuli kupita bila kupingwa, ili kuokoa muda, pesa na mali?, hivyo Magufuli apewe tuu a walkover ya kuendelea hadi 2025 and beyond?.

3. Au kwa vile Uchaguzi wa Rais ni takwa la kikatiba, hivyo uchaguzi huo lazima tuu ufanyike kwa mujibu wa katiba, hata kama uchaguzi huo ni wastage of time, money and resources?!. Kwani katiba ndio nini hata iheshimiwe hivyo?.

4. Na hiyo 2025 tukimuona Magufuli bado anaweza, na anatufaa, jee kuna ubaya kuibadili hiyo katiba yetu ili tumpatie extension of time ya kutosha kuinyoosha Tanzania hadi inyooke kabisa?!.

5. Kwani katiba ni nini?, si ni kipande tuu cha karatasi?!, ingekuwa katiba ni muhimu kihivyo kama ambavyo watu wanataka kutuaminisha humu, ingekanyagwa kirahisi rahisi na kupuuzwa, huku watu wakiangalia tuu?, nini muhimu zaidi kwa taifa letu Tanzania, kati ya katiba ambayo ni kipande tuu cha karatasi na maamuzi ya rais Magufuli ambaye ni rais wa nchi, aliyechaguliwa na watu, katika uchaguzi huru na wa haki?.

6. Na Katiba ni ya nani?!, ni yetu?!, na iko kwa manufaa ya nani?!, si ipo kwa manufaa yetu?!, hivyo sisi ndio muhimu kuliko katiba, hivyo kama sisi Watanzania, katika umoja wetu, tukiamua tunamtaka Magufuli aendelee tuu idefinately, si tunaweza kuiweka tuu pembeni hiyo katiba, na tukaendelea na Magufuli wetu mpaka tutosheke naye?!.

7. Sasa kama Magufuli anatufaa sana kuliko hata katiba na ndio maana anaweza hata kuikanyaga, na katiba haitamruhusu kuendelea baada ya 2025, kuna ubaya gani kuibadili katiba kwa manufaa yetu, na kumwacha aendelee tuu kama Kagame, Museveni na Mugabe?.

8. Au kwani Katiba ni Msahafu kusema haiwezi kubadilishwa?!. Kama katiba inakanywa na hakuna kinachofanyika, Jee kuna ubaya kama tutaibadili katiba na Magufuli akapatiwa muda wa kutosha kabisa wa kuinyoosha nchi yetu kama Kagame anainyoosha Rwanda, , Museveni anavyoinyoosha Uganda na Mugabe anavyoinyoosha Zimbabwe?.

9. Na baada ya katiba kukanyagwa, kwa mikutano ya siasa kuzuiwa, jee kuna ubaya wowote kama wapinzani wa Tanzania mkiamua kwa kauli moja msisimamishe tena mgombea urais, haswa kwa kuzingatia the playing field is not level, na badala yake CCM tuu ndio iwe pekee inatoa mgombea urais siku zote kufuatia long eksipirience ya uzoefu wa muda mrefu wa CCM wa kumtoa rais ambaye siku zote huchaguliwa kwa ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi huru na wa haki?.

10. Na kufuatia somo la demokrasia ya Kiafrika, na mfano hai wa matokeo ya urais wa Zanzibar, na kilichofanyika kwenye urais wa JMT, kweli wapinzani makini bado kweli watahitaji kusimamisha mgombea urais wa kushindana na mgombea wa chama dola, CCM?, yaani by now tumeishajua mgombea wa CCM kwa 2020 ni Magufuli?, kuna chama kiko tayari kumteua mgombea wake kushindana na Magufuli ambaye ni a sitting president, huku kutakuwa ni kugombea au kujifurahisha tuu?!, au hata ikitokea huyo mgombea wa upinzani ameshinda atatangazwa?!.

Hayo ni maswali tuu nimeanza kujiuliza aloud?!.

Jee wewe una maoni gani kuhusu hoja zangu hizi?!.

Paskali
Kwani hawezi kutokea a better person than him? Watu walisema haya haya kwa Mwinyi wakataka aendelee, isingekuwa mwalimu huenda Mwinyi angekuwa rais hadi leo, akaja Mkapa tukasema hayahaya, akaja JK watu wakata akae hadi katiba mpya ipatikane, uzuri JK ni mwanasiasa alijua amani ya Tanzania inasimama kwasababu ya term limit watu wakimchoka rais matumaini yanayobaki ni kusubiri muda wake uishe. Hivi tumeshawahi kujiuliza Mwinyi angeamua kubaki leo tungekuwa na JPM? Who knows what God has in stock for our nation? Huenda ajaye atakuwa bora zaidi ya huyu. Na kiongozi mzuri hufanya yale mazuri katika muda wake wa uongozi na kuwaacha wengine watende mengine mazuri, kiongozi mbovu huamini hakuna binadamu wengine wenye akili ila yeye tu, Na hupenda kung’ang’ania madarakani na mwisho wake huwa sio mzuri. Rais wetu keshatukumbusha mara nyingi tu kuwa hana mpango wa kuendelea muda wake ukiisha, wacha wapiga ramli waendelee ila yeye keshasema. Ikitokea akayageuka maneno yake na msimamo wake basi hatufai. Maana kiongozi mzuri ni yule anayesimamia maneno yake, a man of his words.
 
Umeandika vizuri sana, na umetoa mchanganuo kwa ufasaha, HONGERA.
Lakini ningependa sana kama ungejaribu kuangalia kwa upana mifumo ya watendaji wetu na experience of inefficiency ambayo wanaendelea nayo na imekuwa ngumu sana kuwatoka katika utendeji wao. Hali hiyo inakaribisha mwenye kutaka matokeo bora na sahihi wagombane nae mara kwa mara. Ni watendaji wachache sana ambao wamekuwa pro active na wanaendana na Mkulu. Kama Mkulu angebaki katika uongozi kwa miaka mingine ishirini yawezekana tungekuwa na one of the most efficient public service in Africa. watu kama Mkulu wamepita wengi na ndio walio badilisha mifumo ya uendeshaji na kuboresha katika nchi zao. Gen. Charles de Gaulle (France), Gen. Eisenhower(USA), Stalin (SOVIET UNION, Gen. Caetano (PORTUGAL), Gen.Titto (YUGOSLAVIA) . Kwa kumalizia, kila shilingi ina pande mbili, lakini kuwa efficient Public service ambayo Mkulu anaitaka na angekaa muda mrefu angeipata hata kama inge kuja kwa maumivu na machungu. Kuna maumivu tunayapita wakati wake lakini tutamkumbuka sana. UZEMBE HUWA HAUTETEWI , kuna tofauti ndogo sana kati ya mzembe na mwizi, Wote wazembe na wezi huleta HASARA.
Mkuu Gerald Magembe, kwanza naunga mkono hoja yako hii na kitu kama hiki niliwahi kukishauri humu katika uzi huu. Ili Tanzania tufanikiwe kweli na kuweza kusonga mbele, huyu mtu anahitaji kupatiwa muda wa kutosha, the minimum ya angalau miaka 20 kuinyoosha Tanzania.

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!

P
 
Wanabodi,
Hili ni swali la 5 years ago na sasa mwaka wenyewe wa uchaguzi ndio huu.

Hivi na hii Corona, huu ni mwezi May, uchaguzi ni October, kweli bado tunahitaji kufanya uchaguzi wa rais?.

P
 
Wanabodi,
Hili ni swali la 5 years ago na sasa mwaka wenyewe wa uchaguzi ndio huu.

Hivi na hii Corona, huu ni mwezi May, uchaguzi ni October, kweli bado tunahitaji kufanya uchaguzi wa rais?.

P
Mkuu P uko vizuri upstair na ni mwandishi kwa taaluma ila wakati mwingine unashangaza sana. Uko serious na ulichokiandika? na kama hauko serious kwa nini unaandika ulichokiandika. Kama uko serious basi kazi ipo kwelikweli.
 
Wanabodi,
Hili ni swali la 5 years ago na sasa mwaka wenyewe wa uchaguzi ndio huu.

Hivi na hii Corona, huu ni mwezi May, uchaguzi ni October, kweli bado tunahitaji kufanya uchaguzi wa rais?.

P
Uchaguzi ni takwa la Kikatiba, tukiangalia mtu akae madarakani kwa vigezo flani flani haiwezi kuleta maana wala ufumbuzi, mfano wewe umemuona kafanya vizr sekta flani, Je sekta ambazo kafeli atafutwe Rais mwingine awe msaidizi ili afanye hizo sekta nyingine? TUHESHIMU KATIBA NA TUWEKE MAPENZI BINAFSI KANDO, MAZURI YOTE ANAYOFANYA NDO LENGO LA YEYE KUOMBA KUONGOZA NA WALA SI HISANI, VP MABAYA ANAYOFANYA TUKITUMIA KIGEZO CHAKO ANAPASWA KUONDOLEWA?
 
Mkuu P ni mwandishi unashangaza sana. Uko serious na ulichokiandika?. Kama uko serious basi kazi ipo kwelikweli.
Mkuu Focal, niko very serious!.
Haya ni maoni yangu, pia humu jf ni rukhsa kushangaa!. Endelea kushangaa...
P
 
Mkuu Focal, niko very serious!.
Haya ni maoni yangu, pia humu jf ni rukhsa kushangaa!. Endelea kushangaa...
P
Nimekuelewa mkuu P, lakini uchaguzi ni takwa la kikatiba hata kama huyo Raisi kafanya makubwa kiasi gani. Tukianza haya mambo ya aendelee tu huko ni kuisigina katiba. Ni lazima uchaguzi ufanyike ili kama kawafanyia wananchi mazuri basi wampe kipindi kingine. Hayo ya propaganda tuwaachie wanasiasa kwa taaluma yao..
 
Wanabodi,
Hili ni swali la 5 years ago na sasa mwaka wenyewe wa uchaguzi ndio huu.

Hivi na hii Corona, huu ni mwezi May, uchaguzi ni October, kweli bado tunahitaji kufanya uchaguzi wa rais?.

P
Mungu akiamua lake Mwanadamu hawezi kulizuia. Najua kuna wale wala fedha za Bungeni hawautaku ukweli huu lakini muda ndio huo tena.

Na hata ikafanyika Uchaguzi tutawasikia Puppets wa mabeberu huko majukwaani wakisema "Kufanya uchaguzi ni kufuja hela bora bajeti ingeenda kwenye kuokoa Uchumi uliotetereka na janga la korona n bla bla km walivyozoea"
 
Wanabodi hili ni bandiko la 2015

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?
4. Na hiyo 2025 tukimuona Magufuli bado anaweza, na anatufaa, jee kuna ubaya kuibadili hiyo katiba yetu ili tumpatie extension of time ya kutosha kuinyoosha Tanzania hadi inyooke kabisa?!.

5. Kwani katiba ni nini?, si ni kipande tuu cha karatasi?!, ingekuwa katiba ni muhimu kihivyo kama ambavyo watu wanataka kutuaminisha humu, nini muhimu zaidi kwa taifa letu Tanzania, kati ya katiba ambayo ni kipande tuu cha karatasi na maamuzi ya rais Magufuli ambaye ni rais wa nchi, aliyechaguliwa na watu, katika uchaguzi huru na wa haki?.

6. Na Katiba ni ya nani?!, ni yetu?!, na iko kwa manufaa ya nani?!, si ipo kwa manufaa yetu?!, hivyo sisi ndio muhimu kuliko katiba, hivyo kama sisi Watanzania, katika umoja wetu, tukiamua tunamtaka Magufuli aendelee tuu idefinately, si tunaweza kuiweka tuu pembeni hiyo katiba, na tukaendelea na Magufuli wetu mpaka tutosheke naye?!.

7. Sasa kama Magufuli anatufaa sana kuliko hata katiba na ndio maana anaweza hata kuikanyaga, na katiba haitamruhusu kuendelea baada ya 2025, kuna ubaya gani kuibadili katiba kwa manufaa yetu, na kumwacha aendelee tuu kama Kagame, Museveni na Mugabe?.

8. Au kwani Katiba ni Msahafu kusema haiwezi kubadilishwa?!. Kama katiba inakanywa na hakuna kinachofanyika, Jee kuna ubaya kama tutaibadili katiba na Magufuli akapatiwa muda wa kutosha kabisa wa kuinyoosha nchi yetu kama Kagame anainyoosha Rwanda, , Museveni anavyoinyoosha Uganda na Mugabe anavyoinyoosha Zimbabwe?.

Jee wewe una maoni gani kuhusu hoja zangu hizi?!.

Paskali
Wanabodi, kwanza angalieni tarehe ya bandiko hili, kisha angalia hoja No. 4, 5, 6, 7 na 8 za bandiko hili, kisha sikiliza kilichozungumzwa jana Bungeni Dodoma kuhusu hoja hii.



P
 
Hili andiko linashusha heshima yako
Mkuu Screpa, it's true, linashusha heshima yangu kwa wasomaji wa viwango vyao, lakini kwa wenyewe wenye uwezo to read in between the lines, tunaelewa vizuri sana tuu.
P
 
Wanabodi.

Kwa Kasi Hii ya Rais Wetu Mpendwa, Dr. John Pombe Joseph Magufuli na Falsafa yake ya "Hapa Kazi Tu", na kama hiki tunachokiona sasa, sio nguvu ya soda tuu, yaani ataendelea kwa kasi hii hii hadi 2020, kuna haja kweli ya kufanya tena uchaguzi wa rais? Si tumwache tu aendelee mpaka pale tutakaapoona tumetosheka?

1. Pamoja na ukanyagaji wake wa katiba ya nchi, lakini kwa kazi hii nzuri anayoifanya rais wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, kuinyoosha nchi hii iliyopinda kupindukia kwa rushwa, uzembe na ufisadi, hivi kweli Tanzania, tuna haja tena ya kufanya uchaguzi wa rais kwa mwaka 2020?, au tumwache tu aendelee mpaka 2025? na kama bado anatosha, aendelee tu?

2. Je, hatuwezi kufanya uchaguzi wa wabunge tuu na madiwani, bila kufanya uchaguzi wa rais, na kumwacha Magufuli kupita bila kupingwa, ili kuokoa muda, pesa na mali?, hivyo Magufuli apewe tuu a walkover ya kuendelea hadi 2025 and beyond?.

3. Au kwa vile Uchaguzi wa Rais ni takwa la kikatiba, hivyo uchaguzi huo lazima tuu ufanyike kwa mujibu wa katiba, hata kama uchaguzi huo ni wastage of time, money and resources? Kwani katiba ndio nini hata iheshimiwe hivyo?

4. Na hiyo 2025 tukimuona Magufuli bado anaweza, na anatufaa; je kuna ubaya kuibadili hiyo katiba yetu ili tumpatie extension of time ya kutosha kuinyoosha Tanzania hadi inyooke kabisa?

5. Kwani katiba ni nini? Si ni kipande tuu cha karatasi? Ingekuwa katiba ni muhimu kihivyo kama ambavyo watu wanataka kutuaminisha humu, ingekanyagwa kirahisi rahisi na kupuuzwa, huku watu wakiangalia tu? Nini muhimu zaidi kwa taifa letu Tanzania, kati ya katiba ambayo ni kipande tuu cha karatasi na maamuzi ya rais Magufuli ambaye ni rais wa nchi, aliyechaguliwa na watu, katika uchaguzi huru na wa haki?

6. Na Katiba ni ya nani? Ni yetu? Na iko kwa manufaa ya nani? Si ipo kwa manufaa yetu? Hivyo sisi ndio muhimu kuliko katiba, hivyo kama sisi Watanzania, katika umoja wetu, tukiamua tunamtaka Magufuli aendelee tuu idefinately, si tunaweza kuiweka tuu pembeni hiyo katiba, na tukaendelea na Magufuli wetu mpaka tutosheke naye?

7. Sasa kama Magufuli anatufaa sana kuliko hata katiba na ndio maana anaweza hata kuikanyaga, na katiba haitamruhusu kuendelea baada ya 2025, kuna ubaya gani kuibadili katiba kwa manufaa yetu, na kumwacha aendelee tuu kama Kagame, Museveni na Mugabe?

8. Au kwani Katiba ni Msahafu kusema haiwezi kubadilishwa?!. Kama katiba inakanywa na hakuna kinachofanyika, Jee kuna ubaya kama tutaibadili katiba na Magufuli akapatiwa muda wa kutosha kabisa wa kuinyoosha nchi yetu kama Kagame anainyoosha Rwanda, Museveni anavyoinyoosha Uganda na Mugabe anavyoinyoosha Zimbabwe?

9. Na baada ya katiba kukanyagwa, kwa mikutano ya siasa kuzuiwa, jee kuna ubaya wowote kama wapinzani wa Tanzania mkiamua kwa kauli moja msisimamishe tena mgombea urais, haswa kwa kuzingatia the playing field is not level, na badala yake CCM tuu ndio iwe pekee inatoa mgombea urais siku zote kufuatia long eksipirience ya uzoefu wa muda mrefu wa CCM wa kumtoa rais ambaye siku zote huchaguliwa kwa ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi huru na wa haki?

10. Na kufuatia somo la demokrasia ya Kiafrika, na mfano hai wa matokeo ya urais wa Zanzibar, na kilichofanyika kwenye urais wa JMT, kweli wapinzani makini bado kweli watahitaji kusimamisha mgombea urais wa kushindana na mgombea wa chama dola, CCM, yaani by now tumeishajua mgombea wa CCM kwa 2020 ni Magufuli? Kuna chama kiko tayari kumteua mgombea wake kushindana na Magufuli ambaye ni a sitting president, huku kutakuwa ni kugombea au kujifurahisha tu? Au hata ikitokea huyo mgombea wa upinzani ameshinda atatangazwa?

Hayo ni maswali tu nimeanza kujiuliza aloud.

Je, wewe una maoni gani kuhusu hoja zangu hizi?

Paskali
Vijana wa CCM mnatumika vibaya sana, kama KONDOMU. Mwishowe mtatupwa huko kama GAMBO na MULONGO. Shauri yenu.
 
CCM wamefanya uungwana kumuachia JPM kuendelea kutuvusha, ni matumaini hata vyama vya upinzani waliokuwa wanafikiria fikiria kusimamisha wagombea wa Urais wapige mahesabu kama watapata kura. Ni vema wakahamishia Majeshi huku chini kwenye udiwani na ubunge ili wamwachie JPM aendelee kuijenga nchi.
Mkuu Elius Ndabila, naunga mkono hoja

P
 
Wanabodi.
10. Na kufuatia somo la demokrasia ya Kiafrika, na mfano hai wa matokeo ya urais wa Zanzibar, na kilichofanyika kwenye urais wa JMT, kweli wapinzani makini bado kweli watahitaji kusimamisha mgombea urais wa kushindana na mgombea wa chama dola, CCM, yaani by now tumeishajua mgombea wa CCM kwa 2020 ni Magufuli? Kuna chama kiko tayari kumteua mgombea wake kushindana na Magufuli ambaye ni a sitting president, huku kutakuwa ni kugombea au kujifurahisha tu? Au hata ikitokea huyo mgombea wa upinzani ameshinda atatangazwa?

Hayo ni maswali tu nimeanza kujiuliza aloud.

Paskali
Nani kakuambia rais atakuwa John Magufuli?
Mtajinyonga bure baada ya kujua kuwa 28/10 ndio mwisho wa Giza la nchi hii maana mwanga, furaha, amani na heshima vinarudi tena.
Mkuu Chakaza, umeona hiyo sentence kwenye bold?.

2020 ni Magufuli 5 tena!.
P
 
Mkuu Chakaza, umeona hiyo sentence kwenye bold?.

2020 ni Magufuli 5 tena!.
P
Mkuu nimeiona, lakini kumbuka maneno aliyosema Tundu Lissu mgombea wa Chadema. Kuwa "tukishinda lazima tutatangazwa"
Hayo sio maneno mepesi kutoka kwa mgombea kaliba ya Lissu.
Angetamka Rungwe au Lipumba yangekuwa mepesi lakini sio Lissu.
Nakushauri kama mwandishi unayesomwa na hata hao wakubwa (tofauti na sie makapuku) andika makala za kuonya kuhusu hatari ya mgombea Y kushinda na kutangazwa X katika TZ ya Leo.
Pia matokeo ya jambo hilo ni vurugu na kusababisha vifo. Na jambo hilo katika dunia ya Leo halikubaliki ndio mwanzo wa safari ya The Hague sio kwa mkuu mwenyewe tuu bali hata kina Sirro, Mabeho (kama atajihusisha) na wengine wengi tuu
 
Mkuu nimeiona, lakini kumbuka maneno aliyosema Tundu Lissu mgombea wa Chadema. Kuwa "tukishinda lazima tutatangazwa"
Hayo sio maneno mepesi kutoka kwa mgombea kaliba ya Lissu.
Angetamka Rungwe au Lipumba yangekuwa mepesi lakini sio Lissu.
Nakushauri kama mwandishi unayesomwa na hata hao wakubwa (tofauti na sie makapuku) andika makala za kuonya kuhusu hatari ya mgombea Y kushinda na kutangazwa X katika TZ ya Leo.
Pia matokeo ya jambo hilo ni vurugu na kusababisha vifo. Na jambo hilo katika dunia ya Leo halikubaliki ndio mwanzo wa safari ya The Hague sio kwa mkuu mwenyewe tuu bali hata kina Sirro, Mabeho (kama atajihusisha) na wengine wengi tuu
Hata Lisu Mwenyewe na Chadema yao wanajua fika Magufuli kawaacha mbali na ushindi kwa CCM safari hii sio wa Mashaka Mashaka km ilivyozoeleka huko Nyuma. Hii ndio sababu tunashuhidia Kampeni za furaha na kiaina sherehe Fulani sababu Umma unamfurahia na kumpongeza Mgombea wa CCM kwa kazi nzuri zinazoonekana alizofanya ktk awamu Yake ya kwanza.

Narudia ushindi kwa CCM Mwaka huu sio wa Mashaka Mashaka sababu ile nguvu ya Umma ndio imemkubali Magufuli na ndiyo inayomtaka aendelee.
Hoja dhaifu aliyokuja nayo Lisu (km mesia wa kuikomboa Chadema toka shimo ilulokua inazama) ni kutafuta huruma ya Tatizo alilopata yeye kama yeye na Uchochezi ambao ndio unaomuangisha vibaya)

Naamini Mbowe na wenzake wanachofanya ni kumtumia Lisu kuokoa jahazi lililokwisha anguka.
 
Back
Top Bottom