Nimependezwa sana kwa kasi kubwa ya maendeleo katika nchi yetu ya Tanzania.Serikali ya JK kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kutuletea maendeleo makubwa.Hamna atakayepinga kwa upande wa miundombinu maboresho makubwa yamefanywa ktk uongozi wa JK.Kuanzia barabara,bandari,reli mpaka viwanja vya ndege.Kwa upande wa huduma za afya kuna mapinduzi makubwa katika sekta hii hasa kupunguza vifo vya watoto na akina mama.Hata elimu yetu imepanda ghafla,hii imedhihirishwa na matokeo ya kidato cha 6,kwani ufaulu umeongezeka kwa 95%.Haya ni mafanikio machache katika uongozi wa JK ingawa kuna kasoro chache katika uongozi wa JK hasa RUSHWA kuwa sehemu ya maisha ya Watanzania.Kwani hata kazi zenye mianya ya rushwa kubwa zimekuwa zikigombaniwa na watu wengi baada kuona watumishi wa kazi hizo kuishi maisha ya anasa baada ya kutajirika kwa kupokea rushwa.Hii imejidhirisha katika ajira za uhamiaji watu wengi walijitokeza kwenye usaili ili wapate kazi watajirike kwa RUSHWA.