Kwa kasi hii ya maendeleo mh rais Jakaya Kikwete unamaliza muda wako wa urais kama shujaa

mbeyaman

Member
Sep 28, 2013
97
28
Nimependezwa sana kwa kasi kubwa ya maendeleo katika nchi yetu ya Tanzania.Serikali ya JK kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kutuletea maendeleo makubwa.Hamna atakayepinga kwa upande wa miundombinu maboresho makubwa yamefanywa ktk uongozi wa JK.Kuanzia barabara,bandari,reli mpaka viwanja vya ndege.Kwa upande wa huduma za afya kuna mapinduzi makubwa katika sekta hii hasa kupunguza vifo vya watoto na akina mama.Hata elimu yetu imepanda ghafla,hii imedhihirishwa na matokeo ya kidato cha 6,kwani ufaulu umeongezeka kwa 95%.Haya ni mafanikio machache katika uongozi wa JK ingawa kuna kasoro chache katika uongozi wa JK hasa RUSHWA kuwa sehemu ya maisha ya Watanzania.Kwani hata kazi zenye mianya ya rushwa kubwa zimekuwa zikigombaniwa na watu wengi baada kuona watumishi wa kazi hizo kuishi maisha ya anasa baada ya kutajirika kwa kupokea rushwa.Hii imejidhirisha katika ajira za uhamiaji watu wengi walijitokeza kwenye usaili ili wapate kazi watajirike kwa RUSHWA.
 
Tumpime kiongozi kwa ahadi zilizomfikisha hapo.
Mm natamani kuona MV Bukoba mpya ziwa victoria.
Kipi ni kipimo bora kwa ufanisi wa huyu mkuu.
 
Pilau za Idd hizi watu wanabwabwaja tu,Ha ha haa,aaa ha ha ha haaa!uph uph uph aha haa haa ha haaa!mbavu zangu jamani ha ha haaa!hivi mshawahi kucheka huku mmejaa hasira!
 
Ndugu yangu unaongea na watu waliokwisha bugia gongo hawawezi kukuelewa.
 
kikwete namkubali sana kadhamiria kuhakikisha vijana wote wanafurahia nchi yao na nchi kupiga hatua kubwa kimaendeleo.
 
Mheshimiwa JK na serikali yake kwa haya mazuri aliyotufanyia WaTanzania yapaswa tumpongeze.Hata kwa upande wa demokrasia hawa waropokaji watamkumbaka sana JK,yawezekana rais ajaye atawaminya mbavu.Tumeshuhudia baadhi ya wabunge wakiropoka bungeni na kumshambulia mh.rais kana kwamba mtu wa Manzese.Hata hivyo JK akawavumilia sana ingawa ana uwezo wa kuwashughulikia.
 
Nimependezwa sana kwa kasi kubwa ya maendeleo katika nchi yetu ya Tanzania.Serikali ya JK kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kutuletea maendeleo makubwa.Hamna atakayepinga kwa upande wa miundombinu maboresho makubwa yamefanywa ktk uongozi wa JK.Kuanzia barabara,bandari,reli mpaka viwanja vya ndege.Kwa upande wa huduma za afya kuna mapinduzi makubwa katika sekta hii hasa kupunguza vifo vya watoto na akina mama.Hata elimu yetu imepanda ghafla,hii imedhihirishwa na matokeo ya kidato cha 6,kwani ufaulu umeongezeka kwa 95%.Haya ni mafanikio machache katika uongozi wa JK ingawa kuna kasoro chache katika uongozi wa JK hasa RUSHWA kuwa sehemu ya maisha ya Watanzania.Kwani hata kazi zenye mianya ya rushwa kubwa zimekuwa zikigombaniwa na watu wengi baada kuona watumishi wa kazi hizo kuishi maisha ya anasa baada ya kutajirika kwa kupokea rushwa.Hii imejidhirisha katika ajira za uhamiaji watu wengi walijitokeza kwenye usaili ili wapate kazi watajirike kwa RUSHWA.
Mimi nimependa sana mradi wa kiwanda cha Cement cha Aliko Dangote, hapo nakusifu.
 
Back
Top Bottom