Uchaguzi 2020 Kwa jinsi ninavyomuona Mgombea CCM hataki kufanya kampeni ajue ni wakati wa kuomba Ajira

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,014
8,364
Uchaguzi wa mwaka huu sioni kama mgombea wa CCM anahitaji au kuonesha nia ya dhati ya kufanya kampeni za kuomba kibarua cha kulisha familia yake kwa miaka mitano tena. Ninachokiona naona mgombea kama kachoka na hataki tena sema analazimishwa utaratibu wa CCM kuwa lazima umalize miaka kumi.

Sioni sura ya bashasha waioneshayo wanafunzi waliotoka chuoni wajapo kufanya interview kuomba ajira.

Naiona sura iliyokunjamana, kiburi na majivuno mengi sishangai pengine ni maumbile yake lakini nadhani kipindi hiki ni kipindi muhimu sanaa kwake kuonesha sura ya Tabasamu kama wafanyavyo wanafunzi wajapo hapo ofisini kwangu Wizarani kuomba kazi.

Ninatambua anaumia sana kutumia Bilioni 300 na zaidi kwa ajili ya Uchaguzi ila hizo ni fedha zetu wote ziache zitafunwe.

Hivi zote za nini kununulia Makopo ya kutumbukiza makaratasi ya watu waliotiwa tiki au kosa?Mimi kama Waziri nasema ni nyingi sana tume itupe mchanganuo wa matumizi ya hizo fedha.

Wagombea tambueni mnaomba ajira habari za kuja mmenuna hatuzitaki.
 
Safari hii mzee hana pressure kabisa, nakuahidi wala push-up hutaziona, ujue yeye ni mgombea wakati huohuo anaendelea na majukumu ya kazi yake kama rais!
 
Uchaguzi wa mwaka huu sioni kama mgombea wa CCM anahitaji au kuonesha nia ya dhati ya kufanya kampeni za kuomba kibarua cha kulisha familia yake kwa miaka mitano tena. Ninachokiona naona mgombea kama kachoka na hataki tena sema analazimishwa utaratibu wa CCM kuwa lazima umalize miaka kumi...
Ila akipitishwa kwa mbinde, "mtarimia" meno kwa hiyo miaka 5.

Atakuwa hana cha kupoteza, maana lengo lake siyo kukijenga chama, ni kujijenga yeye mmwenyewe.Akiona ameharibu kabisa, hatoki, anabaki kwa nguvu. Na kila siku lazima ale kisusio ya damu ya mtu.
 
Ipo hivi
1.jpg
 
Aliumia sana na kuwalaani wasaidizi wake siku alipowasha bando na kuona watu wakimwita Lissu Rais Rais Rais . Akauliza wale watu wengi wanaomshangilia Lissu posho wamelipwa kutoka mfuko upi?

Akaambiwa wale hawajabebwa na malori na kupewa posho bali wamejitolea tu bure.
 
Moto upi? Hamna uchaguzi mwepesi kama huu subiri matokeo
Siyo mwepesi kama wengi tulivyodhani. Hali imekuwa tofauti kabisa. Lakini mwisho wa siku Magu atatangazwa mshindi. Tume ni yake na vyombo vya dola anavyo, hapo lazima ashindindishwe.
 
Tulisema mapema, uchaguzi 2020 CCM walishashinda kabla ya kampeni. Kufanya uchaguzi ni kuchezea pesa ya walala hoi bila sababu. Hakuna wakumshinda Magufuli uchaguzi huu. Hata kama ni chungu lakini ni dawa
 
Tulisema mapema, uchaguzi 2020 CCM walishashinda kabla ya kampeni. Kufanya uchaguzi ni kuchezea pesa ya walala hoi bila sababu. Hakuna wakumshinda Magufuli uchaguzi huu. Hata km ni chungu lkn ni daw
Na alitangaza mapema kabisa kuwa uchaguzi utakuwa wa haki na huru. Ndio maana hatuwahitaji hata waangalizi wa humu ndani kwetu, na hata mabeberu pia.
 
Siyo mwepesi kama wengi tulivyodhani. Hali imekuwa tofauti kabisa. Lakini mwisho wa siku Magu atatangazwa mshindi. Tume ni yake na vyombo vya dola anavyo, hapo lazima ashindindishwe.
Mitego karibia yote ya yule wa ubelgiji anairuka.......jamaa nilidhani atakuja kua tishio ila mweupe sana labda upepo unadirike mbeleni ila kwa sasa Magu bado hana mshindani
 
Wapo bize kutunga uongo ili kuonesha namna walivompa laptop kila mwalimu indirectly..... 🤣🤣
Maccm ng'ombe labisa
 
Back
Top Bottom