"Kwa jina la....... Utafaulu", 'Mambongwa'

dalalitz

JF-Expert Member
Sep 6, 2013
3,332
1,861
Ni kauli ya Mama Mzazi kwa bintiye wa Darasa la Saba akiwa ndio anarejea kutoka Shule siku ambayo binti alipaswa kufanya Mtihani.

Na nukuu,
Mama,
".... Marahabaa mwanangu,
Pole kwa Uchovu,
Enhee, Vipi?
Mtihani ulikuwaje?

Mtoto,
" Mh, Kiasi mgumu Ila, nitafanya vizuri tu Mama.

-Ukakasi kwangu:

Mama,
"Kwa jina la..... ..... (akamtaja mchungaji mmoja maarufu),
Utafaulu tu,
Chezea............ (Akamtaja tena)
Si ulikumbuka kunywa yale Maji ya Uzima?
Utaona mwanangu, - Nambari- moja".
Mwisho wa kunukuu.

Sina ngendembwe na kuwajenga watoto kuwa na Imani.
Ila katika hili japo halinihusu limenifikirisha na kupata ukakasi kiasi.

Nimeamini kuwa kuna mambo na Mambongwa pia,
Sijui wewe mdau Unaonaje?
 
Back
Top Bottom