MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,171
Kwa miaka mingi CCM kimejivuna kwamba ni chama kikubwa na chenye wanachama wengi zaidi ya vyama vingine, lakini ktk chaguzi hizi zilizopita, Ktk majimbo yote hakuna hata jimbo moja lililokuwa na wanachama wapiga kura wanaofikia 20,000! Baadhi ya majimbo idadi iliishia 7,000 tu! Hii inanipa ishara kwamba idadi kubwa ya wapiga kura wako nje ya CCM.
Naelewa pia kwamba idadi hiyo ilifikiwa baada ya kadi mpya kutolewa kwa kasi sana, ina maana hapo nyuma idadi ya wana-CCM wenye kadi ilikuwa ndogo sana.
Hakuna haja ya kuwashawishi wajiulize ni kwa nini Wananchi wengi hawavutiwi kujiunga na chama hicho lakini Kama CCM haitabadili mtindo wa kuomba kura kwa kutumia chama, kumbe wale ambao siyo wanachama wake wana nguvu ya kukiondoa madarakani.
Tuombe uchaguzi wa haki usiokuwa na kura za bandia.
Naelewa pia kwamba idadi hiyo ilifikiwa baada ya kadi mpya kutolewa kwa kasi sana, ina maana hapo nyuma idadi ya wana-CCM wenye kadi ilikuwa ndogo sana.
Hakuna haja ya kuwashawishi wajiulize ni kwa nini Wananchi wengi hawavutiwi kujiunga na chama hicho lakini Kama CCM haitabadili mtindo wa kuomba kura kwa kutumia chama, kumbe wale ambao siyo wanachama wake wana nguvu ya kukiondoa madarakani.
Tuombe uchaguzi wa haki usiokuwa na kura za bandia.