Balozi wa Dodoma
JF-Expert Member
- Dec 22, 2013
- 477
- 177
Aje washkaji zangu wa nguvu!?
Kuna jambo sijalipenda hata #Kidogo na sina budi niliweke wazi. wiki iliyopita Kampuni ya WCB iliingia kwenye headliness baada ya msanii wake Diamond platnumz kuzuia uzinduzi wa Singo yake aliyowashirikisha Psquare ili kuruhusu msanii chipukizi wa WcB harmonize kuachia singo yake mpya iitwayo matatizo.
Kiukweli ilikuwa ni jambo zuri sana kwa mondi kuonesha support kwa vijana wake lakini nimeshangazwa na kitendo cha WCB tena kumruhusu Mondi kuachia ngoma yake mpya huku ngoma ya Harmonize bado ipo "Yamoto" bado hata aijaanza kupoa. Hii itasababisha Watu kusahau singo mpya ya Harmo na kuipa nafasi kubwa zaidi singo ya mondi kutamba. Kibiashara kwa WCB ni faida kubwa sana bt kwa Msanii Harmonize ni unyonyaji.
Napenda kuwashauri WCB wawe na mpango maalum wa kuachia ngoma. Tujifunze kwa wenzetu wamarekani inapotokea msanii mmoja yupo kwenye Chat basi wasanii wengine humpa gap ili wasije wakafunikwa. WCB ni chama kubwa na natumaini hili mtalifanyia kazi.
Nawasilisha
Otherwise uwe hu ujui Muziki. nilitamani sana nikukumbushe enzi za Crew ya Junior Mafia ile crew iliyokuwa ikiongozwa na Rais Notorious B.I.G huku humo ndani kukiwa na wakali kibao km Puff Daddy a.k.a P Diddy, Lil Kim a.k.a Queen B, na Rap Master Lil Sizz.
lkn kwa kuwa umeonesha huujui ngoja nikukumbushe kuhusu Crew ya YMCB Chini ya lebo ya Young Money na Producer Young Muller wakiwa Chini ya Rais Birdman.
hii crew ilikua na Wanyama wakali km Vile Lil Wayne, Nicki Minaj , Drek, Birdman na Tyga.
hawa wote walikua wanaachia ngoma zao ndani ya mwezi mmoja na kila baada ya miez miwili wanaachia ngoma ya Kundi yaani YMCB.
Sasa kinachotokea kwa WCB leo sio kitu kipya. ni msingi tu wa kujiimarisha ktk Soko la ndani. na kutumia nguvu ya video zao kujiimarisha ktk soko la nje.
In case ulikua hujui. Soko la ndani linahitaji Cooperative Power ku Push kazi ya sanaa kuwafikia watu wengi. kwa hili WCB wako mbali sana.