Kwa hili Polisi Wasilaumiwe

Jul 28, 2013
72
17
Kwa kifupi napenda kutoa maoni na uzoefu wangu juu ya ripoti iliyotolewa kuhusiana na kunyanyaswa na kuteswa kwa wananchi katika opresheni TOKOMEZA iliyofanyawa na majeshi ya ulinzi na usalama.

kwa uzoefu wangu tangu, madhambi mengi yaliyoripotiwa kutendwa katika opresheni hiyo polisi hawakuhusika kutenda ufuska huo, polisi hawezi akabaka raia, kudhalilisha kwa kuwafanyisha ngono na mengineyo. Vitendo hivi vimetendwa na majeshi mengine. Chunguzeni hilo, mtaniambia. Jeshi la Polisi linaheshimu sana sheria za nchi, ila yapo majeshi ambayo hayatambui hilo. kwa kifupi, operesheni kama hizi ziwe zinaongozwa na Jeshi la polisi kwani ndiyo wasimamizi wa sheria za nchi. chunguzeni mtagundua hilo.
 
Sijaona hoja inayothibitisha kuwa polisi hawahusiki! "polisi hawawezi kufanya hivyo!" so, unamaanisha majeshi ndio wanaweza! Si ndio!
Kwani Jeshi waweze wananini na polisi washindwe wananini?
...
Tena unatupa na task ya kuchunguza!
Hivi umesahau 'He who asserts must proof'?
...
Katika nchi hii hakuna watu wazembe kama polisi!!!!!
basi tu!
 
Hakuna kitu kama hicho labda kama na wewe ni mmoja wao. na katika hili naomba tuelewane, POLISI wamekuwa mstari wa mbele katika kuvunja sharia za nchi hii. wananchi wamekuwa hawana imani nao. Naomba usijaribu kuingiza siasa katika hili... speak of the reality
 
WAZIRI MKUU ndiye wakulaumiwa na kuwajibika kwa madhila yote yaliyofanyiwa raia wa nchi hii ndio maana serikali haijachukua hatua dhidi ya Askari polisi na wanajeshi waliohusika ambao kimantiki ni watekelezaji wa amri. Tutegemee maafa zaidi hadi atakapotengua agizo lake "wapigwe tu"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom