Nimekuwa nikimuunga Obama toka siku ya kwanza. Lakini hili la kuanza kushikamana na upande mmoja linanikifu. Na siamini kama litakuwa na mwisho mzuri. Obama kutoa silaha kwa upande wowote katika mgogoro wowote Afrika ni kuanza kile ambacho Afrika inakiogopa kutoka kwenu. Ukifungua njia wewe basi wauza silaha wako wote ndio utakuwa umewaruhusu kumwaga silaha zao barani hapa na kutuachia kama yale mliyoyafanya kule Amerika ya Kati na Kusini, Vietnam na kwingineko Asia. Munge apishilie hilo mbali.
Dawa ya Somalia iko ndani ya Somalia yenyewe na ndugu zao Waislamu. Mkono wa Marekani Somalia nina hakika ni mkoma ambaye hakubaliki hata iwe nini. Unaowasaidia watashindwa na ndio mwanzo wa kuanza kujiaibisha Afrika na kwingineko.
Somalia ni moto wa kuotea mbali ndugu yangu. Hawa ni watu ambao kisasi chao hakiishi milele. Na hakuna adui mbaya kama mtu ambaye hajui kusahau ubaya aliofanyiwa na anataka revenge. Hukumbuki yaliyowapata Wamarekani Somalia mara baada ya kuondoka Siad Barre ndugu yangu. Na wewe hivi hivi unaona na unakubali kushauriwa na wajinga wanaodhani Somalia ni sawa na sehemu nyingine duniani na unakubali. Haya ngoja muanze kutumiwa salamu maana mmeyataka wenyewe wallahi.
Na nyie Waburundi na Waganda hivi mna njaa kali kiasi hicho hadi kukubali kutumika kama canon fodder ???
Dawa ya Somalia iko ndani ya Somalia yenyewe na ndugu zao Waislamu. Mkono wa Marekani Somalia nina hakika ni mkoma ambaye hakubaliki hata iwe nini. Unaowasaidia watashindwa na ndio mwanzo wa kuanza kujiaibisha Afrika na kwingineko.
Somalia ni moto wa kuotea mbali ndugu yangu. Hawa ni watu ambao kisasi chao hakiishi milele. Na hakuna adui mbaya kama mtu ambaye hajui kusahau ubaya aliofanyiwa na anataka revenge. Hukumbuki yaliyowapata Wamarekani Somalia mara baada ya kuondoka Siad Barre ndugu yangu. Na wewe hivi hivi unaona na unakubali kushauriwa na wajinga wanaodhani Somalia ni sawa na sehemu nyingine duniani na unakubali. Haya ngoja muanze kutumiwa salamu maana mmeyataka wenyewe wallahi.
Na nyie Waburundi na Waganda hivi mna njaa kali kiasi hicho hadi kukubali kutumika kama canon fodder ???