Kwa hili mnaojiita wasomi udom mmepotoka

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
Kwa kweli sasa elimu yetu ya kibongo nayo imeingiliwa na wachakachuwaji,mi sikutegemea kama hawa wanaojiita wasomi kutoa tamko la upande mmoja,nadhani wakati wa uchaguzi kulikuwa na matatizo mengi sana juu ya utoaji wa matokeo ambao mwishowake ilibidi nguvu ya wananchi iingilie kati mfano mwanza,lakini wasomi hawa na ccm yao hawakutoa tamko lolote hata la kulaani ucheleweshaji wa matokeo hayo,wakati chadema wanalalamika juu ya tume ya uchaguzi kutokuwa huru na kupendelea upande mmoja hawa wanaojiita wasomi wa ccm hawakutoa tamko la kulaani hilo ambalo ndilo lingeweza kuleta machafuko ktk nchi yetu,lakini kinachoniuma zaidi ni pale issue ya udini ilivyotumika ktk kampeni za baadhi ya wanasiasa sijaona hawavibaraka wasomi wanaotumia maji kufikilia na sio ubongo kutoa tamko juu ya hila hiyo mbaya,
leo hii wanatoa tamko ktk issue ambayo wabunge wa chadema wamejaribu kufikisha ujumbe kwa jamii juu ya kile kinachowasumbuwa na wasichokubaliana nacho ktk yote yaliyotokea tangu mwanzo wa uchaguzi,
mi nadhani tukiwa kama wasomi tunahitaji hii nchi isonge mbele kimaendeleo na kuwa huru katika maswala ya kisiasa,ningefurahi sana kama hawa wanaojiita wasomi wa udom wangetowa tamko juu ya katiba iliyopitwa na wakati na isiyo na msaada wowote ktk mstakabali wa taifa letu.
Kwa hili mnaojiita wasomi udom mmepotoka acheni siasa ifanye kazi yake na nyinyi mnaojiita wasomi mkate kitabu kwani utaliwa kichwa na tafsli ya usomi ikapotea
mapinduziiiiiiii daimaaaa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom