Kwa hili mb. Lekule Laiza ameiweka uchi serikali yake inayoongozwa na CCM

HGYTXK

Senior Member
Oct 3, 2011
194
70
kupitia taarifa ya habari iliyorushwa na kituo cha ITV nimemsikia Mbunge huyo akitoa maneno yafuatayo ktk harakati zake za kuomba kura kwa wanaCCM ktk ngazi ya uenyekiti anayoigombea.Namnukuu.

"Wananchi wa Longido mnatakiwa mtambue kuwa nafasi hii ninayoigombea haina maslahi kwangu kimaslahi ila ninachokihitaji ni kurudisha hadhi ya chama ambacho ni mimi ndiye niliyekifikisha hapa kilipo,Mnakumbuka kuwa hata hii wilaya ya Longido ni mimi ndiye niliyeipigania mpaka tumepata halmashauri hapa ata kama HAIKUWA NA VIGEZO VYA KUWA HIVYO".

MY TAKE: Hii ndio serikali yetu,hautaji Degree kuamini kuwa mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo yanayofanyika hayazingatii vigezo bali ni utashi tu wa watawala ktk kuangalia ni jinsi gani watatoa fadhira zao kwa watu fulanifulani ktk chama chao.Kuna sehemu nyingi sana hapa nchini zina kila vigezo zinazostahili kuitwa wilaya,mkoa ama Manispaa lakini hazifanywi hivyo kutokana na kutokuwa na makada ama viongozi maarufu wanaotokea sehemu hizo.Tumekusikia Leiza na asante kwa kuonyesha madudu ya serikali yetu.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TZ.
 
Hili mbona liko wazi ndugu yangu, huoni nasi huku Katavi ndio tunakumbukwa kwa kuwekea barabara ya lami na zaidi tumepata mkoa mpya hii yote ni kwa sababu ya Pinda. Bila yeye haya maendeleo tunayoyashuhudia huku hivi sasa tungekuwa tunayasikia tu.
 
Kwa maana hiyo basi, yale majimbo yanayoongozwa na wapinzani wasahau maendeleo hata kama wamefikisha vigezo stahiki.
 
kupitia taarifa ya habari iliyorushwa na kituo cha ITV nimemsikia Mbunge huyo akitoa maneno yafuatayo ktk harakati zake za kuomba kura kwa wanaCCM ktk ngazi ya uenyekiti anayoigombea.Namnukuu.

"Wananchi wa Longido mnatakiwa mtambue kuwa nafasi hii ninayoigombea haina maslahi kwangu kimaslahi ila ninachokihitaji ni kurudisha hadhi ya chama ambacho ni mimi ndiye niliyekifikisha hapa kilipo,Mnakumbuka kuwa hata hii wilaya ya Longido ni mimi ndiye niliyeipigania mpaka tumepata halmashauri hapa ata kama HAIKUWA NA VIGEZO VYA KUWA HIVYO".

MY TAKE: Hii ndio serikali yetu,hautaji Degree kuamini kuwa mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo yanayofanyika hayazingatii vigezo bali ni utashi tu wa watawala ktk kuangalia ni jinsi gani watatoa fadhira zao kwa watu fulanifulani ktk chama chao.Kuna sehemu nyingi sana hapa nchini zina kila vigezo zinazostahili kuitwa wilaya,mkoa ama Manispaa lakini hazifanywi hivyo kutokana na kutokuwa na makada ama viongozi maarufu wanaotokea sehemu hizo.Tumekusikia Leiza na asante kwa kuonyesha madudu ya serikali yetu.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TZ.

Lakini upeo wake wa kuelewa unaweza kuwa chanzo cha kutojua kama Londigo ilikuwa na vigezo vya kuchaguliwa kuwa Wilaya. Nadhani tatizo hapa si Serikali kuifanya Longido kuwa Wilaya bali ni mawazo duni tu ya mwanasiasa huyo kuwa yeye ni chanzo cha wilaya hiyo kupata hiyo hadhi. Suala la eneo fulani kupewa hadhi ya wilaya si la wanasiasa pekee, linapitia mchakato mkubwa, hushirikisha wataalamu wa ardhi, wanasiasa, wachumi na wengine wengi.
 
sasa kama yeye alifikisha hiyo wilaya hapo,kwan hakuna wakuipeleka zaid ya hapo?
 
Kwa maana hiyo basi, yale majimbo yanayoongozwa na wapinzani wasahau maendeleo hata kama wamefikisha vigezo stahiki.
Mkuu ungetaja majimbo ambayo yanaongozwa na wapinzani na siyo wilaya la sivyo mchango wako huu unaweza kukushushia hadhi ya kuwa GT. Hili linaweza kusaidia pia kutazama hali za majimbo hayo kimaendelea ukilinganisha na yale ambayo ni Wilaya.
 
sasa kama yeye alifikisha hiyo wilaya hapo,kwan hakuna wakuipeleka zaid ya hapo?

Teh teh, Vijana wamewakamata hao wazee, hadi sasa wanaongea vitu ambavyo vinawashushia hadhi. Mimi ninachoamini ni kwamba hoja za kuomba kupata wilaya si za siri na huwa zinawasillishwa kwenye vikao mbalimbali na hata katika vikao vya Bunge, hivyo sijiaminishi kabisa kuwa kuna Wilaya inapitishwa kisiasa hata kama hazina vigezo. Namshangaa sana huyu mzee kama alikuwa anajua kabisa kuwa anaongoza jimbo ambalo halina vigezo vya kuwa wilaya na akakaa kimya. Ni dhahiri kabisa kuwa kwa kauli hiyo yeye ndiye hana vigezo vya kuwa kiongozi wa juu wa CCM.
 
Lakini upeo wake wa kuelewa unaweza kuwa chanzo cha kutojua kama Londigo ilikuwa na vigezo vya kuchaguliwa kuwa Wilaya. Nadhani tatizo hapa si Serikali kuifanya Longido kuwa Wilaya bali ni mawazo duni tu ya mwanasiasa huyo kuwa yeye ni chanzo cha wilaya hiyo kupata hiyo hadhi. Suala la eneo fulani kupewa hadhi ya wilaya si la wanasiasa pekee, linapitia mchakato mkubwa, hushirikisha wataalamu wa ardhi, wanasiasa, wachumi na wengine wengi.

Mkuu, inaonekana wewe umesoma vitabu vinavyo onesha taratibu za kupata manispa, halmashauri, mkoa, wilaya n.k, hizo ni theories, practically huwa haiko hivyo kwa magamba, mwana siasa alioko sehemu fulani inategemea anamvuto na ushawishi kiasi gani kwa wakuu wa magamba, rejea yafuatayo, hivi ule uwanja wa ndege wa kimataifa pale Arusha enzi za Sumaye, uliishia wapi? nakumbuka enzi hizo watu walipiga kelele, kwamba huo ni upotezaji wa pesa cause kama kuna KIA, ambao upo jirani sana na Arusha, kuna sababu gani ya kujenga huo mwingine tena, watawala wakakomaa, serikali ipobadirika, kimya, hii ndio Bongo bana!
 
usishangae mkuu, ndiyo maana kuna pendekezo la kuiweka Tanzania chini ya CCM kwenye maajabu ya dunia. we fuatilia watakuelekeza namna ya kuipigia kura ili iingie kwenye maajabu ya Dunia.
 
Hili mbona liko wazi ndugu yangu, huoni nasi huku Katavi ndio tunakumbukwa kwa kuwekea barabara ya lami na zaidi tumepata mkoa mpya hii yote ni kwa sababu ya Pinda. Bila yeye haya maendeleo tunayoyashuhudia huku hivi sasa tungekuwa tunayasikia tu.
Vipi sisi ambao hatuna viongozi wa juu serikalini?
 
kupitia taarifa ya habari iliyorushwa na kituo cha ITV nimemsikia Mbunge huyo akitoa maneno yafuatayo ktk harakati zake za kuomba kura kwa wanaCCM ktk ngazi ya uenyekiti anayoigombea.Namnukuu.

"Wananchi wa Longido mnatakiwa mtambue kuwa nafasi hii ninayoigombea haina maslahi kwangu kimaslahi ila ninachokihitaji ni kurudisha hadhi ya chama ambacho ni mimi ndiye niliyekifikisha hapa kilipo,Mnakumbuka kuwa hata hii wilaya ya Longido ni mimi ndiye niliyeipigania mpaka tumepata halmashauri hapa ata kama HAIKUWA NA VIGEZO VYA KUWA HIVYO".

MY TAKE: Hii ndio serikali yetu,hautaji Degree kuamini kuwa mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo yanayofanyika hayazingatii vigezo bali ni utashi tu wa watawala ktk kuangalia ni jinsi gani watatoa fadhira zao kwa watu fulanifulani ktk chama chao.Kuna sehemu nyingi sana hapa nchini zina kila vigezo zinazostahili kuitwa wilaya,mkoa ama Manispaa lakini hazifanywi hivyo kutokana na kutokuwa na makada ama viongozi maarufu wanaotokea sehemu hizo.Tumekusikia Leiza na asante kwa kuonyesha madudu ya serikali yetu.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TZ.

Kama ningekuwa mmoja kati ya wana Longido ningecomment kuwa.,kama anaweza kupigania vitu visivyo na vigezo na kuiingiza nchi katika kugharamia wilaya mpya isiyo na vigezo haoni kwamba hiyo ni sababu tosha ya kumnyima madaraka ayatakayo!
 
kupitia taarifa ya habari iliyorushwa na kituo cha ITV nimemsikia Mbunge huyo akitoa maneno yafuatayo ktk harakati zake za kuomba kura kwa wanaCCM ktk ngazi ya uenyekiti anayoigombea.Namnukuu.

"Wananchi wa Longido mnatakiwa mtambue kuwa nafasi hii ninayoigombea haina maslahi kwangu kimaslahi ila ninachokihitaji ni kurudisha hadhi ya chama ambacho ni mimi ndiye niliyekifikisha hapa kilipo,Mnakumbuka kuwa hata hii wilaya ya Longido ni mimi ndiye niliyeipigania mpaka tumepata halmashauri hapa ata kama HAIKUWA NA VIGEZO VYA KUWA HIVYO".

MY TAKE: Hii ndio serikali yetu,hautaji Degree kuamini kuwa mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo yanayofanyika hayazingatii vigezo bali ni utashi tu wa watawala ktk kuangalia ni jinsi gani watatoa fadhira zao kwa watu fulanifulani ktk chama chao.Kuna sehemu nyingi sana hapa nchini zina kila vigezo zinazostahili kuitwa wilaya,mkoa ama Manispaa lakini hazifanywi hivyo kutokana na kutokuwa na makada ama viongozi maarufu wanaotokea sehemu hizo.Tumekusikia Leiza na asante kwa kuonyesha madudu ya serikali yetu.

MUNGU IBARIKI AFRIKA,MUNGU IBARIKI TZ.

Mh. Lekule Laizer amesema kweli kwani Longido ni kama kijiji vile! Mji hauna hadhi ya kuitwa Makao Makuu ya Wilaya.
 
Huyu bwana yeye kaamua tu kuweka wazi lakini hivi ndivyo vitimbi vilivyo kithiri katika majimbo ya uchaguzi 2010 eg, ILEMELA namengine mengi tu!
 
ndio viongozi wetu hawa kupitia chama magamba sampuli ya Dk. Bana na wengineo wengi wenye kufikiri kwa kutumia sehemu za kupumzikia chini mwilini mwanadamu anapochoka kusimama ama kutembea.
 
Hili mbona liko wazi ndugu yangu, huoni nasi huku Katavi ndio tunakumbukwa kwa kuwekea barabara ya lami na zaidi tumepata mkoa mpya hii yote ni kwa sababu ya Pinda. Bila yeye haya maendeleo tunayoyashuhudia huku hivi sasa tungekuwa tunayasikia tu.
mkoa wenye wilaya mbili tena baada ya wilaya ya mpanda kukatwa....katavi ishaongezeka wilaya nyingine kweli...kwa tz hii ni kawida sana
 
ndio viongozi wetu hawa kupitia chama magamba sampuli ya Dk. Bana na wengineo wengi wenye kufikiri kwa kutumia sehemu za kupumzikia chini mwilini mwanadamu anapochoka kusimama ama kutembea.
ndo sehem gani hiyo...mwamba usemao ukweli apa unaogopa kusema ukweli
 
Back
Top Bottom